Fahamu daraja lako la akili na nafasi yako katika mpango wa Ulimwengu

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,540
46,075
Uwezo wa akili kwa binadamu umetofautiana kwa viwango na hali mbalimbali, hili ni jambo linalotofautisha hali za maisha na nafasi zao katika mpango wa kijamii. Kuna madaraja kama manne ambayo binadamu wamegawanyika katika uwezo wa akili.

1. Daraja la juu kabisa,hawa mara nyingine huitwa ma-genius, ni watu wenye uwezo mkubwa sana ki akili, wanazaliwa wakiwa hivyo, hata wasiposoma sana wanaweza kufanya mambo ya kushangaza.

Wengi katika hili daraja ni wavumbuzi, composers, wachekeshaji nguli mfano wa George Carlin, waandishi nguli mfano Stephen King, waigizaji nguli mfani Mfano Morgan Freeman na DiCaprio,waandishi habari nguli mfano Mehdi Hasan na wanasayansi wote wakubwa. Wengine ni kina Newton, Galileo, Shaban Robert, Shakespeare, Mozart, Beethoven, Einstein, Bill Gates, Charlie Chaplin, Meryl Streep n.k

Wengi wao huwa hawajihusishi na siasa na vigumu sana kwao kuwa katika nafasi yoyote ya madaraka kwa sababu akili zao zimeegemea zaidi katika sayansi na facts na pia huwa ni vigumu kuvumulia uongo,vitu visivyo na logic, kujipendekeza na fitna za kisiasa.

2. Daraja la juu, hawa ni watu wenye akili za juu kupitia kujifunza na uzoefu, darasani ni wale ambao hupata ufaulu wa juu ya wastani mara nyingi. Huwa wana jitihada sana kupata maarifa zaidi na kujifunza mambo mengi. Uwezo wao mkubwa huwa unatokana na jitihada zao binafsi. Wanajua sana kusoma akili na moves za watu na kuzitumia kwa faida yao.

Wengi wao huwa na uwezo mkubwa wa kutengeneza connections na madili na mara nyingi huwa ndio wanaofanikiwa zaidi maishani. Wengi wao huwa ndio viongozi wa juu kama Marais, majaji na wabunge. Wengine ni wachambuzi na wafanyabishara wakubwa

3. Daraja la kati, hawa ni wale wenye uwezo kawaida tu,huwa hawana mambo mengi sana, wanahitaji kupata mahitaji ya kawaida tu ya binadamu na wakaridhika. Wengi katika kundi hili ni waajiriwa wanaohitaji nyumba ndogo,mke au mume mzuri na gari ndogo ya kutembelea kisha wafurahie maisha.

Wengi wao ni watu ambao huwa hawapendi sana au hawana uwezo wa kufikiri nje ya mfumo wa maisha walioukuta, waliouzoea, wanaoujua au unaowalisha.

4. Daraja la chini, hawa ni watu ambao mara nyingi huwa na uwezo duni sana kiakili na hutegemea hayo makundi mengi yote kuendesha maisha yao. Kwenye maisha wengi wao huishia kufanya kazi zote zile zinazodharaulika na pia hutumika kama pawns na daraja la pili.
 
Hivi akili inapatikana eneo gani la kichwa?
Hili swali ni mfano wa moshi kwenye gari unapatina wapi ule moshi kwenye injini..
 
Kwenye ubongo
Kwahiyo ukipasua kichwa kule kwenye ubongo utakutana na hako kadude kanakoitwa akili?
(Bado haujanipa jibu lenye mashiko)

Sasa katika andiko lako wewe umejiweka au umejiona uko daraja lipi kati ya 1-4?
 
Usichojua ni kwamba
Mtu au binadamu anapozaliwa anakuwa empty set kichwani hajui lolote.
Uwezo mkubwa au mdogo wa akili unatokana na vitu vikubwa vitatu tu.
1.kurithi kutokaa kwa wazazi waliomzaa.
2.Mazingira ya makuzi ya mtu husika.
3.ujuzi ,kujifunza na jitihada binafsi kwenye Mambo ya msingi.

Mtu aliyeyelewa na wazazi madaktari Kuna uwezo mkubwa wa yeye kuja kuwa daktari pia. Na ndivyo hivyo mwana wa mvuvi atakuwa karibu na uvuvi maana akili inajengwa na mazingira na shughuli mwanadamu azifanyazo kila siku.

Ulioutaja wewe 🙄 huo ni upeo wa kufikiri , speed ya akili katika kujaji Jambo. Ndo kuna hayo matabaka uliyoweka hapo juu.

Ni Mimi hushpuyy
 
Usichojua ni kwamba
.

Mtu aliyeyelewa na wazazi madaktari Kuna uwezo mkubwa wa yeye kuja kuwa daktari pia. Na ndivyo hivyo mwana wa mvuvi atakuwa karibu na uvuvi maana akili inajengwa na mazingira na shughuli mwanadamu azifanyazo kila siku.



Ni Mimi hushpuyy

Muroto; Ko watoto wako watalima bangi?
Jamaa; Inawezekanika tu wakaiga mzee wangu
 
Usichojua ni kwamba
Mtu au binadamu anapozaliwa anakuwa empty set kichwani hajui lolote.
Uwezo mkubwa au mdogo wa akili unatokana na vitu vikubwa vitatu tu.
1.kurithi kutokaa kwa wazazi waliomzaa.
2.Mazingira ya makuzi ya mtu husika.
3.ujuzi ,kujifunza na jitihada binafsi kwenye Mambo ya msingi.

Unasema uwezo wa akili unaweza kurithiwa kwa wazazi, bado ukasema binadamu anazaliwa empty set..!!
 
Akili sio kadude,mfano rahisi ni software yako ya simu ya Android au Windows ya computer.
Unajua ipo inafanya kazi ila ukipasua simu au computer yako huwezi kuikuta software humo ndani yake.
Kwahiyo ukipasua kichwa kule kwenye ubongo utakutana na hako kadude kanakoitwa akili?
(Bado haujanipa jibu lenye mashiko)

Sasa katika andiko lako wewe umejiweka au umejiona uko daraja lipi kati ya 1-4?
 
Akili sio kadude,mfano rahisi ni software yako ya simu ya Android au Windows ya computer.
Unajua ipo inafanya kazi ila ukipasua simu au computer yako huwezi kuikuta software humo ndani yake.

Vipi wale walionyofoa na kuficha ubongo wa Einstein (ain’t sure) kwa ajili ya uchunguzi.?
 
Points zako tatu zina ukweli na maana kubwa sana ila umechanganya mno maelezo yake mwisho wake umekuwa mkanganyiko usioeleweka.
Usichojua ni kwamba
Mtu au binadamu anapozaliwa anakuwa empty set kichwani hajui lolote.
Uwezo mkubwa au mdogo wa akili unatokana na vitu vikubwa vitatu tu.
1.kurithi kutokaa kwa wazazi waliomzaa.
2.Mazingira ya makuzi ya mtu husika.
3.ujuzi ,kujifunza na jitihada binafsi kwenye Mambo ya msingi.

Mtu aliyeyelewa na wazazi madaktari Kuna uwezo mkubwa wa yeye kuja kuwa daktari pia. Na ndivyo hivyo mwana wa mvuvi atakuwa karibu na uvuvi maana akili inajengwa na mazingira na shughuli mwanadamu azifanyazo kila siku.

Ulioutaja wewe huo ni upeo wa kufikiri , speed ya akili katika kujaji Jambo. Ndo kuna hayo matabaka uliyoweka hapo juu.

Ni Mimi hushpuyy
 
Ubongo tofauti na viungo vingine vingi vya mwili hauwezi kuhifadhiwa muda mrefu hivyo bila kuharibika ila kuna tafiti nyingi zinazofanywa kuhusu ubongo wa binadamu na akili.
Vipi wale walionyofoa na kuficha ubongo wa Einstein (ain’t sure) kwa ajili ya uchunguzi.?
 
Ubongo tofauti na viungo vingine vingi vya mwili hauwezi kuhifadhiwa muda mrefu hivyo bila kuharibika ila kuna tafiti nyingi zinazofanywa kuhusu ubongo wa binadamu na akili.

Hujaelewa swali langu, kivipi wanachunguza ‘akili’ kwenye ubongo ikiwa ni ‘software’ na sio lidude.?
 
Usiishie hapo,endelea mbele utaelewa zaidi.
Kuna mtu mwenye akili ya daraja la chini kabisa kiakili ila anakuwa mfalme kutokana na kuzaliwa katika familia hiyo. Kuna watu wa daraja la chini kiakili ila wanajua kujipendekeza na wako loyal hivyo huishia kujipenyeza na kuaminiwa hadi kuketi mezani pa wakuu na wakati mwingine kufanyika wakuu kabisa ijapokuwa huishia kusababisha matatizo makubwa sana.
Nimesoma hadi pale umesema wabunge ni watu wenye akili daraja la juu, nikaishia hapo!
 
Akili sio kadude,mfano rahisi ni software yako ya simu ya Android au Windows ya computer.
Unajua ipo inafanya kazi ila ukipasua simu au computer yako huwezi kuikuta software humo ndani yake.
Mkuu unazidi kunipa maswali mengi.

Programu tete (kwa Kiingereza software ) ni mkusanyo wa maelezo yasiyo tendaji yaliyotunzwa katika kumbukumbu ya tarakilishi ili kuweza kuchakata takwimu fulani pindi itakapohitajika kufanya hivyo.

Mfano mzuri umesema software kama window ya kompyuta, maana yake akili umeifananisha na software, lakini kumbuka software ni file zinazoonekana kwa macho na huweza kuhamishika kwa kutumia flash,sd card, hard disk n.k

Swali linalokuja; Akili inahamishika? Je akili ni kitu unachoweza kukiona kwa macho mfano wa programu tete(software)?
 
Kwahiyo ukipasua kichwa kule kwenye ubongo utakutana na hako kadude kanakoitwa akili?
(Bado haujanipa jibu lenye mashiko)

Sasa katika andiko lako wewe umejiweka au umejiona uko daraja lipi kati ya 1-4?
Hapo ndio ukuu wa Sir Godi unaonekana....
hata ukipasua ubongo hutoweza kuona akili....
akili utaiona kwenye vitendo tu.....
 
Back
Top Bottom