Nd. wana JF,
Naomba kidogo nitoe maoni machache kuhusu hoja zinazotolewa mara kwa mara na watu ambao wanashangazwa na manun'guniko ya Muungano. Kuna wale wanaodai kuwa bila ya Muungano Zanzibar itaangamia. Wanadai kuwa Zanzibar haiwezi kujitegemea na kwa hivyo haiwezi kusimama kama nchi huru.Wanadai Serikali ya Muungano(kwa maana ya Tanzania Bara) inapata hasara sana kuibeba Zanzibar na kulipa gharama nyingi zikiwemo za ulinzi na usalama na hata baadhi ya wakati kusaidia kulipa mishahara ya watumishi wa Serikali ya Mapindizi ya Zanzibar. Kwa madai yao, uhai wa Zanzibar unategemea kubebwa na Tanzania bara na Zanzibar inaihitaji zaidi Tanzania bara na sio Tanzania bara inaihitaji Zanzibar zaidi.
Sasa kwa nini wazanzibari wengi hawana shukrani na haweshi kuubugudhi Muungano?
Kwa maoni yangu ni kweli kuwa gharama nyingi za kuendesha Serikali ya Muungano zinabebwa na Tanzania Bara.Huu ni ukweli ulio wazi.Mchango wa Zanzibar kwenye kuendesha Serikali ya Muungano ni mdogo sana. Kwa upande mwengine mtu unaweza kusema ni sawa ndugu zetu wa Bara kulipa hizo gharama za kuendesha Serikali ya Muungano kwa sababu Serikali hiyo ndiyo inayoendesha na kusimamia shughuli zote za Tanzania Bara. Kwa maneno mengine,Serikali ya Muungano pia ni Serikali ya Tanzania bara.
Vile vile tuangalie maslahi yanayotokana na hiyo Serikali ya Muungano yanakwenda wapi.
Serikali ya Tanzania,kama zilivyo serikali zote masikini, imekuwa ikitegemea sana misaada kutoka nchi za nje kwa shughuli zake za kimaendeleo zikiwemo ujenzi wa barabara, mahospitali, vyuo vya elimu ya juu na mashule na hata huduma nyengine za kijamii kama vile maji,umeme na kupambana na maradhi.
Serikali ya Tanzania imekuwa ikiomba na kupokea misaada hii kila mwaka katika kipindi chote cha miaka arubaini na sita ya Muungano. Kila mwaka misaada hii imekuwa ikitiririka Tanzania na tunashuhudia jinsi inavyotumika kuendeleza hizo sekta nilizozitaja hapo juu kwa upande wa Tanzania bara. Sasa ikiwa Zanzibar ni sehemu ya Tanzania kama ambavyo wenzetu wa Tanzania bara hudai wanapoomba hiyo misaada ni kiasi gani hutengwa (kila mwaka) kwa ajili ya Zanzibar?
Nimeuliza suali hii kwa wanaojua wanasema kwa miaka mingi sana (mpaka katikati ya 1980's) Zanzibar ilikuwa hawapewi kitu. Na mpaka sasa hivi wanachoambulia Zanzibar ni kama pesa anazopewa mtoto kwenda kununua pipi tu ukilinganisha na pesa wanazopata Tanzania bara.
Hapa naomba kunukuu takwimu hizi chache zinazotokana na hotuba za bajeti za mawaziri wa fedha wa Tanzania.
B. Foreign Grants and Loans Tshs.2,549 billions
Naomba kidogo nitoe maoni machache kuhusu hoja zinazotolewa mara kwa mara na watu ambao wanashangazwa na manun'guniko ya Muungano. Kuna wale wanaodai kuwa bila ya Muungano Zanzibar itaangamia. Wanadai kuwa Zanzibar haiwezi kujitegemea na kwa hivyo haiwezi kusimama kama nchi huru.Wanadai Serikali ya Muungano(kwa maana ya Tanzania Bara) inapata hasara sana kuibeba Zanzibar na kulipa gharama nyingi zikiwemo za ulinzi na usalama na hata baadhi ya wakati kusaidia kulipa mishahara ya watumishi wa Serikali ya Mapindizi ya Zanzibar. Kwa madai yao, uhai wa Zanzibar unategemea kubebwa na Tanzania bara na Zanzibar inaihitaji zaidi Tanzania bara na sio Tanzania bara inaihitaji Zanzibar zaidi.
Sasa kwa nini wazanzibari wengi hawana shukrani na haweshi kuubugudhi Muungano?
Kwa maoni yangu ni kweli kuwa gharama nyingi za kuendesha Serikali ya Muungano zinabebwa na Tanzania Bara.Huu ni ukweli ulio wazi.Mchango wa Zanzibar kwenye kuendesha Serikali ya Muungano ni mdogo sana. Kwa upande mwengine mtu unaweza kusema ni sawa ndugu zetu wa Bara kulipa hizo gharama za kuendesha Serikali ya Muungano kwa sababu Serikali hiyo ndiyo inayoendesha na kusimamia shughuli zote za Tanzania Bara. Kwa maneno mengine,Serikali ya Muungano pia ni Serikali ya Tanzania bara.
Vile vile tuangalie maslahi yanayotokana na hiyo Serikali ya Muungano yanakwenda wapi.
Serikali ya Tanzania,kama zilivyo serikali zote masikini, imekuwa ikitegemea sana misaada kutoka nchi za nje kwa shughuli zake za kimaendeleo zikiwemo ujenzi wa barabara, mahospitali, vyuo vya elimu ya juu na mashule na hata huduma nyengine za kijamii kama vile maji,umeme na kupambana na maradhi.
Serikali ya Tanzania imekuwa ikiomba na kupokea misaada hii kila mwaka katika kipindi chote cha miaka arubaini na sita ya Muungano. Kila mwaka misaada hii imekuwa ikitiririka Tanzania na tunashuhudia jinsi inavyotumika kuendeleza hizo sekta nilizozitaja hapo juu kwa upande wa Tanzania bara. Sasa ikiwa Zanzibar ni sehemu ya Tanzania kama ambavyo wenzetu wa Tanzania bara hudai wanapoomba hiyo misaada ni kiasi gani hutengwa (kila mwaka) kwa ajili ya Zanzibar?
Nimeuliza suali hii kwa wanaojua wanasema kwa miaka mingi sana (mpaka katikati ya 1980's) Zanzibar ilikuwa hawapewi kitu. Na mpaka sasa hivi wanachoambulia Zanzibar ni kama pesa anazopewa mtoto kwenda kununua pipi tu ukilinganisha na pesa wanazopata Tanzania bara.
Hapa naomba kunukuu takwimu hizi chache zinazotokana na hotuba za bajeti za mawaziri wa fedha wa Tanzania.
'In 2009/10 government expenditure will stand at 9.51 trillion shillings.
'Aid from foreign donors will stand at 3.182 trillion shillings.'
Na katika bajeti ya 2007/2008'Aid from foreign donors will stand at 3.182 trillion shillings.'
A. Domestic Revenue Tshs.3,502billions
B. Foreign Grants and Loans Tshs.2,549 billions
Hizi ni bajeti za miaka miwili tu lakini katika kila mwaka mambo ni hayo hayo. Mtiririko ni huo huo. Asilimia kubwa sana ya bajeti ni misaada kutoka nje.Angalia hizo "trillions" ambazo Tanzania inapewa kila mwaka halafu tujiulize Zanzibar(kama sehemu ya Tanzania) inapewa kiasi gani.Wanaojua mambo wanasema wanachopata Zanzibar ni pesa ya pipi tu katika hizo na ndiyo maana Serikali ya Zanzibar haiwezi kufanya lo lote kubwa la kimaendeleo.
Kama Zanzibar ingekuwa inapewa haki yake ya hiyo misaada basi ingeweza kupiga hatua kubwa sana na haraka za kimaendeleo na pasingekuwa na haja ya kushindwa kulipa mishahara au kujitegemea Tanzania bara. Ukweli ni kuwa hicho wanachotoa bara kuisaidia Zanzibar ni kidogo mno ukilinganisha na hiyo haki yetu ya misaada ambayo wamekuwa wakitunyima kila mwaka kwa muda wa miaka 46 ya Muungano.
Wanaojua mahesabu watusaidie tuone ni trilioni ngapi wametudhulumu na Zanzibar ingekuwa wapi kwa trilioni hizo. Na jee kama Zanzibar ingekuwa huru na inapewa moja kwa moja hayo matrilioni ya misaada(kama wanavyopewa nchi zote maskini duniani), kweli barabara zetu zingekuwa na mashimo? Kweli hospitali zetu zingekuwa na magodoro yaliyooza na wagojwa kulala chini? Kweli tungekuwa na upungufu wa madaktari na wataalamu wengine?Kweli watoto wetu wangekuwa wanakaa chini maskuli?
Hapa nimegusia misaada ya pesa tu, sijaingia kwenye misaada mengine kama vile nafasi za mosomo nje (scholarships) ambazo kila mwaka humwagwa kwa maelfu na takriban zote hupewa watanzania bara. Ukitembea kwenye nchi nyingi wanafunzi watanzania waliojazana vyuoni ni vijana kutoka Tanzania Bara.Mzanzibari ni mmoja kwa elfu. Hili sitolijadili hapa. Ni mada nyengine.
Dalali