FACTS: panga pangua ni wazi JPM kashindwa nchi imemuelemea na mambo hayaendi. Zile sifa sio za kweli uchumi unayumba

ichard, post: 29151363, member: 414"]Hivyo viwanda 3000+ mbona ni idadi ndogo sana ndugu yangu unaonekana hujatembea Tanzania sio?

Sasa, ukitaka kuthibitsha hivyo viwanda uende wizarani ila mimi nafahamu mkoa wa Pwani pekee una viwanda vidogo, vya kati na vikubwa.429 kwasababu mimi pia nina interest zangu huko.

Katika hivyo Kibaha pekee ina viwanda 76

Hiyo taarifa ipo mkoani nenda ukatembelee.

Sasa Tanzania ina mikoa mingapi? na ukifahamu hilo viwanda hivyo unavyotaja vinafika hiyo idadi.

Halafu, viwanda si tu vile unavyodhani kwamba ni lazima viwe viwanda vikubwa, kuna vidogo, vya kati na vikubwa.

Richard viwanda 3,000+ tunaambiwa viko mkoa wa Pwani peke yake. Tumewahi kuomba list yake hapa na mahali vilipo. Hilo halijawahi kutokea popote.

Kuna mtu anaitwa jingalao anajua nimeanza kufuatilia hili suala toka mwaka jana mwishoni na post zetu humu jukwaani za ufuatiliaji huo zipo. Nilimtaka aandae jedwali la hivyo viwanda 100@mkoa na vilipo ili tuhamasishe vijana wakaombe ajira. Na yeye amebaki kama ww kutaja idadi. Sikatai kwamba hakuna ujenzi wa viwanda, kwani ujenzi wa viwanda hakuanza enzi za Magufuli bali toka ukoloni. Ninachosema hivyo viwanda 3,000+ ni kweli vipo Pwani?.

Pwani hakuna viwanda 3000 ila kuna viwanda hivyo nilivyokutajia 429

Isipokuwa taarifa sahihi ya idara ya takwimu ambayo tulipewa na waziri Mwijage ni viwanda zaidi ya 50776 na hizo ni takwimu za 2015, vikijumuisha viwanda vidogo binafsi, vya kati na vikubwa.

Lakini tangu raisi Magufuli ameingia madarakani kuna viwanda zaidi ya 3000 ndo vimejengwa au kufufuliwa, na katika hivyo viwanda vikubwa ni 393 vyenye thamani ya dola 2,262 au trillioni shillings 5,198

Kuna viwanda vilivyofufuliwa kama kile cha Mang'ula na kile cha kuchambua Pamba huko Musoma na vingine kama cha MOPROCO na Morogoro Canvas Mills Ltd ambavyo viko Morogoro.

Viwanda vipya vinajengwa kama kile cha maziwa kule Simiyu na kiwanda cha chuma kule Kibaha.

Sasa ukitaka taarifa rasmi ingia wizarani au idara ya takwimu.

Au la tembea ujionee mwenyewe.

Mimi sasa hivi naelekea Dodoma kupata ule mvinyo wa Dodoma Wine made in Tanzania..
 
Hapa ndio utajua tuna rais muongo na huwezi kumuamini kwa lolote. Kila siku anasema tuna viwanda 3,000+, sasa kama waziri kasimamia ujenzi wa viwanda vingi hivyo unamtumbuaje? Alitegemea kupata viwanda 10,000? Simply idadi asemayo ya viwanda ni uongo wa wazi.

Waziri wa kilimo ni kama kamtoa kafara tu, bajeti ya wizara ya kilimo ni kiasi gani? Je kwa bajet hiyo alitarajia muujiza gani toka kwa waziri wa hiyo wizara? Hapo mwenye tatizo halisi ni yeye, ila ana uwezo wa kumuwajibisha huyo waziri.
Hahahahah umenifanya nicheke nyani hao ni kundule
 
Pwani hakuna viwanda 3000 ila kuna viwanda hivyo nilivyokutajia 297

Isipokuwa taarifa sahihi ya idara ya takwimu ambayo tulipewa na waziri Mwijage ni viwanda zaidi ya 50776 na hizo ni takwimu za 2015, vikijumuisha viwanda vidogo binafsi, vya kati na vikubwa.

Lakini tangu raisi Magufuli ameingia madarakani kuna viwanda zaidi ya 3000 ndo vimejengwa au kufufuliwa, na katika hivyo viwanda vikubwa ni 393 vyenye thamani ya dola 2,262 au trillioni shillings 5,198

Kuna viwanda vilivyofufuliwa kama kile cha Mang'ula na kile cha kuchambua Pamba huko Musoma na vingine kama cha MOPROCO na Morogoro Canvas Mills Ltd ambavyo viko Morogoro.

Viwanda vipya vinajengwa kama kile cha maziwa kule Simiyu na kiwanda cha chuma kule Kibaha.

Sasa ukitaka taarifa rasmi ingia wizarani au idara ya takwimu.

Au la tembea ujionee mwenyewe.

Mimi sasa hivi naelekea Dodoma kupata ule mvinyo wa Dodoma Wine made in Tanzania..


Richard umeanza kufuatilia haya majigambo ya viwanda lini? Inaoneka idadi yako ni tofauti na ya rais. Hivi unafahamu hizo nyuzi ziko humu humu na nimesikia kwa masikio yangu akitamka hiyo idadi kwa mkoa wa Pwani tu? Safari hii watetezi mna kazi. Nikuambie brother Richard, hakuna jambo gumu kama kutetea uongo. Tupo hapahapa jukwaani nitakuonyesha tu.
 
Richard umeanza kufuatilia haya majigambo ya viwanda lini? Inaoneka idadi yako ni tofauti na ya rais. Hivi unafahamu hizo nyuzi ziko humu humu na nimesikia kwa masikio yangu akitamka hiyo idadi kwa mkoa wa Pwani tu? Safari hii watetezi mna kazi. Nikuambie brother Richard, hakuna jambo gumu kama kutetea uongo. Tupo hapahapa jukwaani nitakuonyesha tu.

Nasisitiza, Pwani hakuna viwanda 3000

Tena nakupa Update ya baada ya ziara ya makamu wa raisi Samia Suluhu Hassan , Mhandisi Ndikilo amesema hadi juzi viwanda vimeongezeka idadi vimekuwa 429 na hicho kilichofunguliwa juzi ni kile cha gypsum cha KNAUF.
 
'..we're in ze 'light track'...tembeeni kifua mbele ndugu zangu watz.!

Akitumbua shida,na akiwaacha hao wanaoharibu ni shida..

bora nitembee kifua 'mbere'..
Suala la korosho mharibifu ni yule mbabe aliyetishia kuwafumua ahangazi zake Majaliwa. Ajitumbue kwa sababu ameshindwa majukumu hata ya kuteua tu.
 
Viwanda zaidi 3000?
Hata kama vyote ni viwanda vidogo, wastani wa kodi kwa kiwanda kimoja kwa mwaka ni kiasi gani?
Kwa viwanda 3000 tunazungumzia kiasi gani?
 
Najiuliza, hivi tuna rejesta ya viwanda? TRA au Wizara husika?
Vipo wapi, vimeanza lini, vinaajiri watu wangapi, vinazalisha nini?
 
Watanzania wengi mpo kama malaya tu hamjui cha kushika(hasa ufipa), kila siku mmekuwa mkilalamika kwanini Mwijage hatumbuliwi leo katumbuliwa mnaanza kulia kishogashoga.
Hata siku atakayotumbuliwa Makonda mtalalamika tu.
 
Kilio ni zamu zamu na kila mtu ataonja ubaya wa Magu, maana Mwijage alivyo kuwa anaambiwa juu ya jiwe yeye alikuwa anaona kama zamu yake haiwezi kufika!.
Hivi kosa Mwijage ni lipi hasa? Je Tizeba?

Duuh...mimi naona kama Mwijage amejitahidi sanaa.
 
Japo rais kawateua pia anayo mamlaka ya kuwatengua,lakini frequency ya teua tengua ni kubwa mno inatisha.Kuna wasiwasi kuwa uongozi wake umegeuka shamba la majaribio.
Yawezekana itafika muda tukakodi mawaziri wazungu kutokeaJumuiya ya Umoja wa Ulaya EEC na hata marekani,ili waongoze wizara za Tanzania.
 
Kwa ukweli.na uwazi magufuli kachemka ila anaona aibu kusema ukweli.

Hii nchi kwa upnde wa uchumi ni mbaya na tumbua tumbua hii ni dalili tosha mambo hayaendi.

Kama Mwijage na viwnda vyake 3600 inauwaje natumbuliwa? Ajaye naye ataleta viwnda hivyo?

Hakuanzia hapa tumbua tumbua yaani miaka 3 ni panga pangua atamaliza mitano mambo ni hayajhaya ni dalili ya wazi kuwa nchi imemshinda na uchumi unakufa
Huna akili wewe. Kwa taarifa yako uchumi unakuwa kwa kasi sana.
 
Hivi kosa Mwijage ni lipi hasa? Je Tizeba?

Duuh...mimi naona kama Mwijage amejitahidi sanaa.
Embu kuwa serious mkuu, yaani viwanda vya vyerehani navyo una hesabu viwanda yule jamaa kazi alikuwa hawezi zaidi ya kuongea tu kama cherehani...
 
Hivi kosa Mwijage ni lipi hasa? Je Tizeba?

Duuh...mimi naona kama Mwijage amejitahidi sanaa.
kosa lao wamekuwa kimya muda wote swala hili limeshughulikiwa na Ikulu, na mwaijage kosa lake ni kwa miaka 3 ameshindwa kushawishi kujenga hata kiwanda kimoja cha kubanguankorosho, ila nadhani kwenye hili Makatibu wa kuu unawaachaje
 
Sasa kama nchi imemshinda mnashindwa nini kushinda Uchaguzi na kuichukuwa?
kwa akili zako wakiita nchi zinazofanya uchaguz utasema tanzania kuna uchaguzi au (UHUNI)???wakala anatoka na box la kupigia kura ndani ya kituo anaenda nalo uchochoroni tena akilindwa ,halafu analirudisha tena kwenye chumba cha kupigia kura na zoezi linaendelea kama kawaida!!!
 
Ukimuona kocha anapanguapangua safu ya wachezaji jua hana uhakika na ushindi
 
Analaumiwa kwa sababu ya kukosa umakini katika uteuzi wake. Kama ni kampuni au shirika binafsi lawama pia kwa organization kwa kutofanya recruitment nzuri!
 
Back
Top Bottom