Facebook yangu WAMEIFUNGA, MSAADA KUIFUNGUA WAJAMENI..

Hute

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,537
6,458
HABARI ZENYU wandugu,...nimepata tatizo moja, ukurasa wangu wa facebook haufunguki, nikijaribu kufungua wanadisplay maneno haya hapa.
"For security reasons your account is temporarily locked
Unfortunately, your computer appears to be infected with a virus,
Don't worry. we will help you find and remove any infected files right away."

ndio hivyo tu, sasa baada ya hapa wanakuletea sehemu ya kubonyeza "continue"ukicontinue wanakupeleka kwenye macfee website na download link wakati uko logged in, na hauwezi kuona ukurasa wako kwasababu umezuiliwa na maneno hayo hapo juu....ukibonyeza download inaanza kudownload macfee anti virus...tafadhalini jamani, how can i open my page kwasababu kule kuna watu wengi nawasiliana na kuchati nao sasaivi wiki sijachati alafu kuna picha zangu nyingi nilizisevu kule....asanteni...
 
chaajabu zaidi, computer yangu nimeweka anti virus mpya ya mwaka huu juzi...nimeacha computer yangu nikaenda internet cafe labda za huko zitakuwa hazijaathirika na kirusi, nikakuta yaleyale...chaajabu, account yangu inakataa, lakini account ya facebook ya wife inakubali..that means wameblock account yangu tu na si tatizo la computer kwasababu kila computer nitakayojaribu wanasema hivyohivyo kwenye page yangu, ila kwenye acocunt za wengine zinakubali bila matatizo....help please!
 
chaajabu zaidi, computer yangu nimeweka anti virus mpya ya mwaka huu juzi...nimeacha computer yangu nikaenda internet cafe labda za huko zitakuwa hazijaathirika na kirusi, nikakuta yaleyale...chaajabu, account yangu inakataa, lakini account ya facebook ya wife inakubali..that means wameblock account yangu tu na si tatizo la computer kwasababu kila computer nitakayojaribu wanasema hivyohivyo kwenye page yangu, ila kwenye acocunt za wengine zinakubali bila matatizo....help please!
Ebu nipe user name na password yako unayolog face book nikutatulie,its very simple ukinipatia hizo vitu!!
 
Ebu nipe user name na password yako unayolog face book nikutatulie,its very simple ukinipatia hizo vitu!!
SIDANGANYIKI, hata mtoto mdogo hawezi kukubali kitu kama icho...nipe wewe ya kwako kwanza afu na mimi nikupe yangu au vipi....kama huwezi kunisaidia chapa lapa!
 
Mkuu, hili jambo linatokea mara nyingi siku za karibuni, haswa baada ya update ya interface waliyofanya.

Ni jambo linalosababishwa na mengi, hivyo kama protection, wanaifunga account. Hii siyo kwamba wamekujua wewe in person na kukufatilia mienendo yako, bali ni process ambayo iko automated inayokuwa triggered na baadhi ya mambo wakati unatumia facebook.

Kama nilivyosema, ni mambo mengi yanayoweza kusababisha. Mojawapo ni kama:
-- multiple location simultaneous login - kutokana na features za kutunza location zilizopo kwenye fb, ikitokea kwamba account yako inaonekana kuwa logged on au kuna attempts za kulog in kutoka geographical location tofauti, kama hizo location zinatakuwa haziko kwenye surfing profile yako, au kuwa declared, basi system yao ina trigger account lock up kwa nia ya kukuprotect wewe (account yako na info).

-- multiple account login - hii inaweza kutokea pale wewe mwenyewe unapokuwa na account zaidi ya moja, au nduguyo kuwa logged in na kusahau kulog out. Pale unapokuja ku-access account yako na huku browser unayotumia inakuwa na info za account mbili tofauti zikiwa saved (non cleared cache and saved cookie session); basi yawezekana kabisa kutokea corruption katika browser ambayo inaweza kuwa interpreted kama violation katika kuaccess mojawapo ya account inayotaka kuwa accessed. Hivyo jambo hili kuweza ku-trigger system account lock-up.

-- Copying and pasting - hili lilishanitokea mimi. Hili linasababishwa na ku-copy links within private message kisha kutumia link hiyo (ambayo itakuwa na session time-stamp) kwenye login ya account yako utakayofanya kwenye computer hiyo hiyo wakati tofauti, au account nyingine yako. Au basi, kutumia link hiyo kwenye computer au device tofauti na kule ulikoitoa.

Lakini kwa vile umetaja element ya virus, kunaweza kuwa na sababu nyinginezo, lakini nilizoorodhesha hapo juu ni zile ninazoweza kufikiria personally kwa haraka haraka kama sababu zinazoweza kusababisha hilo jambo kutokea. Pia mbali na sababu ya virus na zile nilizotaja, pia kwaweza kuwepo na sababu nyinginezo nisizokuwa na ufahamu nazo.

Solution:

Naamini baada ya hilo kutokea watakuwa wamedokeza namna ya ku-resolve tatizo. Kuna link watakuwa wamekupatia, either via email au hapohapo kwenye notification.

-- Kama wamekupatia option ya ku-activate account hapo hapo kwenye notification (Kwanza kabisa hakikisha hiyo link iliyotolewa ni ya facebook kweli) Unaweza kuicopy yote na kupeleka kwenye computer nyingine kuona kama itakupeleka kwenye facebook ya ukweli. Nasema hili kwani kwa hiyo notification ya virus, yawezekana kuna phishing ya link inayoweza kuwa imetokea, hivyo unaweza kujikuta unapelekwa kwenye facebook magumashi. Ambako detail zako ndo zitathibitishwa na kuibiwa kabisa.

Kama link unauhakika nayo, watakupa option mbili: kuactivate account kwa wewe ku-identify picha za watu waliokuwa tagged kama moja ya rafiki zako kwenye account yako. Au uchague ku-reactivate kwa kujibu swali la kukumbushia kama utasahau password yako.

-- Mbinu zozote utakayochagua itaishia na wewe kuulizwa maswali mengi zaidi na kisha kubadili password yako. Hivyo kuwa na pen ili kama kuna kitu cha kuandika ukiandike ili usisahau baada ya reactivation kukamilika. Maana maswali na setting za fb zimebadilika na siku hizi wanauliza mambo mengi zaidi.

Kama activation itakuwa via a link ambayo watakutumia kwenye email, basi fata maelezo yao. Process haitotofautiana sana.

Good luck!!
 
chaajabu zaidi, computer yangu nimeweka anti virus mpya ya mwaka huu juzi...nimeacha computer yangu nikaenda internet cafe labda za huko zitakuwa hazijaathirika na kirusi, nikakuta yaleyale...chaajabu, account yangu inakataa, lakini account ya facebook ya wife inakubali..that means wameblock account yangu tu na si tatizo la computer kwasababu kila computer nitakayojaribu wanasema hivyohivyo kwenye page yangu, ila kwenye acocunt za wengine zinakubali bila matatizo....help please!

Anti virus inakaa mwaka mmoja tu we tangia mwaka juzi..kuna mtu ka bypass ua password subiri kwa siku 2 itakubali.
 
Back
Top Bottom