Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Facebook imeamua kutofungulia akaunti ya aliyekuwa Rais wa Marekani, Donald Trump baada ya kufungiwa kwa kudaiwa kuchochea vurugu katika Jengo la Bunge la Marekani Januari 6 mwaka huu.
Uamuzi huo unafuata baada ya Kampuni hiyo kuifungia akaunti za Trump za Facebook na Instagram kwa muda wa saa 24 baada ya Trump kuchapisha maudhui yanayoonekana kuwasifia wanaofanya vurugu katika Jengo la Bunge, kisha kampuni hiyo ikaendelea kuzifungia akaunti hizo hadi atakapoondoka madarakani.
Uamuzi wa Facebook wa kutoifungulia akaunti hiyo ulitajwa na Mkuu wa Kampuni hiyo, Mark Zuckerberg kuwa umechangiwa na kuona hatari kubwa ya kumwacha Trump kuendelea kutumia mtandao huo kwa wakati huo.
Uamuzi huu wa Facebook umelaumiwa na baadhi ya watu kwa kudai kuwa Facebook imeshindwa kuchukua hatua yenyewe hadi kutegemea uamuzi wa Bodi Huru.
Uamuzi wa leo unatokana na kikao cha marejeo cha Bodi ya Kujitegemea iliyoundwa mwaka 2020 kwa lengo la kufanya maamuzi kuhusu maudhui yaliyo katika majukwaa ya Facebook na Instagram, na inapaswa kufanya kazi bila ushawishi wa uongozi wa Facebook. Bodi hiyo ndiyo iliyotangaza kuwa itaangalia kuzuiwa kwa akaunti za Rais Trump na kuwa inapokea maoni ya umma kuhusu suala hilo.
Wakosoaji wanadai kuwa Bodi hiyo si huru kama inavyojiita, na kuwa imeundwa na kufadhiliwa na Facebook, wakitilia shaka utendaji wake wa kujitegemea.
Trump, hata hivyo, ametangaza kuanzisha mtandao wake wa kijamii, na amefungua tovuti yake kwa lengo la kuchapisha taarifa zake saa kadhaa kabla ya maamuzi ya Bodi hiyo ya Facebook.
Chanzo: The Guardian
Uamuzi huo unafuata baada ya Kampuni hiyo kuifungia akaunti za Trump za Facebook na Instagram kwa muda wa saa 24 baada ya Trump kuchapisha maudhui yanayoonekana kuwasifia wanaofanya vurugu katika Jengo la Bunge, kisha kampuni hiyo ikaendelea kuzifungia akaunti hizo hadi atakapoondoka madarakani.
Uamuzi wa Facebook wa kutoifungulia akaunti hiyo ulitajwa na Mkuu wa Kampuni hiyo, Mark Zuckerberg kuwa umechangiwa na kuona hatari kubwa ya kumwacha Trump kuendelea kutumia mtandao huo kwa wakati huo.
Uamuzi huu wa Facebook umelaumiwa na baadhi ya watu kwa kudai kuwa Facebook imeshindwa kuchukua hatua yenyewe hadi kutegemea uamuzi wa Bodi Huru.
Uamuzi wa leo unatokana na kikao cha marejeo cha Bodi ya Kujitegemea iliyoundwa mwaka 2020 kwa lengo la kufanya maamuzi kuhusu maudhui yaliyo katika majukwaa ya Facebook na Instagram, na inapaswa kufanya kazi bila ushawishi wa uongozi wa Facebook. Bodi hiyo ndiyo iliyotangaza kuwa itaangalia kuzuiwa kwa akaunti za Rais Trump na kuwa inapokea maoni ya umma kuhusu suala hilo.
Wakosoaji wanadai kuwa Bodi hiyo si huru kama inavyojiita, na kuwa imeundwa na kufadhiliwa na Facebook, wakitilia shaka utendaji wake wa kujitegemea.
Trump, hata hivyo, ametangaza kuanzisha mtandao wake wa kijamii, na amefungua tovuti yake kwa lengo la kuchapisha taarifa zake saa kadhaa kabla ya maamuzi ya Bodi hiyo ya Facebook.
Chanzo: The Guardian