Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikifanya tafiti mbali ili kubaini mambo mbali mbali ambayo yanayochangia mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika. Nadhani wengi wetu tunatambua ya kuwa yapo mambo mengi sana yanachongia mahusiano mengi ya mapenzi kuvunjika ikiwemo usaliti. n.k. lakini tukiachana na yote hayo leo nitaongelea kitu kimoja ambacho kutokana na utafiti nioufanya nimegundua kuwa ni kitu kimoja wapo ambacho kinasabisha mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika nayo ni Facebook. Natambua ya kuwa zipo social network nyingi lakini hapa nitaongelea facebook kwa sababu ndiyo social network maarufu, inayoongoza, inayopendwa na kutumika na watu wengi duniani.
Utafiti nilioufanya unaonyesha kuwa facebook imekuwa ni chanzo kimoja wapo cha mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika na hii ni kutokana na sababu zifuatazo:-
Prepared by:
Young Master
Utafiti nilioufanya unaonyesha kuwa facebook imekuwa ni chanzo kimoja wapo cha mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika na hii ni kutokana na sababu zifuatazo:-
- Kutumia muda mwingi kuwa facebook - Sababu moja wapo ambayo inasababisha mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika ni kutumia muda mwingi kuwa facebook hali inayopelekea kujisahau, kuwasahau wapenzi wao na kutowajali wapenzi wao hali iliyopelekea wao kujikuta wakipoteza wapenzi wao kutokana na wao kutumia muda mwingi kuwa facebook na kuipa attention facebook zaidi kuliko wapenzi wao hali inayosababisha mapenzi kupungua kati ya hao wapendanao. Mfano: Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa na mpenzi wangu ambaye alipenda sana kutumia facebook mara kwa mara hata nyakati ambazo tulikuwa pamoja yeye alikuwa hapay antettion sana na mimi na badala yake attention yake yote ilikuwa kwenye facebook. Nilijaribu sana kumueleza kuhusu tabia yake hiyo lakini hakunisikia hali iliyopelekea kuchukua uamuzi wa kumkataza kutumia facebook na kuidisable account yake permanently. baada ya kufanya hivyo nilishangaa sana kwani mapenzi yake kwangu yaliongozeka ghafla kuliko siku za nyuma na akawa ananipigia simu na kunijulia hali hadi usiku wa manane tofauti na siku za nyuma ndipo nilipogundua kuwa kumbe facebook ndio ilikuwa inamkeep busy na kumfanya yeye aione facebook ni bora zaidi kuliko mimi.
- Kulewa sifa - sababu nyingine ambayo inapelekea mahusiano mengi ya kimapenzi kuvunjika kutokana na matumizi ya facebook ni kulewa sifa amabazo huzipata kutoka kwa watu mbali mbali jambo linalomjengea mtu kiburi na kujiona yeye yuko juu na hata kama akiachana na mpenzi wake leo kesho atapata mwingine
- Ku Flirt- Sababu nyingine ambayo inapelekea mahusiano mengi kuvunjika kutokana na matumizi ya facebook ni kuflirt. Kutokana na uchunguzi nilioufanya asilimia kubwa ya wanawake na wanaume wengi huwa na wapenzi zaidi ya mmoja kwenye mitandao na hii yote huchangiwa na kuflirt. Watu wengi husema kuwa eti kuflirt ni kitu cha kawaida na haiwezi kusababisha mpenzi wako kukusaliti jambo ambalo si la kweli. Kwa nini ninasema hivyo? Ngoja niwatoleeni mfano huu; Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kuflirt na msichana mmoja katika facebook ambaye alikuwa na mpenzi wake. At first nilichukulia kama utani but as time went on mapenzi yalizidi kunoga hadi siku ya siku tukakutana na kuvunja amri ya sita. Kutoka ma mapenzi mazito niliyompa, dada huyo alijikuta akimwacha mpenzi wake na kunifuata mimi pasipo kujali mwenzake anaumia vipi wala ametoka naye wapi.
Prepared by:
Young Master