Facebook account yangu ina msululu wa friend request za makahaba.

Hili tatizo liliwahi kunikumba Mimi. Nikawa-unfriend watu wengi sana, Facebook wakanifungia kwa sababu kuna matumizi yasiyo ya kawaida kwenye akaunti yangu, wakaomba vitambulisho nikawapa ila ndio nikafanya kama alivyosema mdau hapo juu kistaarabu, hapo ndio tatizo likaisha.
 
Wakuu hebu mwenye kufahamu anifahamishe, sijui account ya Facebook imekumbwa na jinamizi gani nilizoea kupokea friend request za watu intelectual lakini kwa siku za karibuni hali imebadirika, ninapokea request nyingi za warembo na nikiwascreen vizuri nagunduwa 90% ni wauza kummer tu.

Sasa nimeingiwa na madhaka hizi facebook account in future zinaweza hata kukuharibia maisha na kujulikana wewe ni mtu wa namna gani, sasa nimekuja jukwaa hili la watalaam ili kushare experince na kujuzana chimbuko la tatizo hili ni nini? Au wale friendlust wangu wengi wapo kwenye friendlist za hawa warembo wauza uchi? Ndio sababu na mimi napata request mfululizo za warembo hawa ambao wanauza uchi kwa style ya kisasa bila kujipanga barabarani?

Nimewaza mbali sana nimeona friend list yangu sasa inaelemewa na warembo na mimi ni marriage Man hii si ni shida?

Nawasilisha.
Usitie shaka jiandae kisaikolojia
 
Mkuu huyu bwana mdogo alikuwa na points ila njia aliyotumia kuzifikisha ndo imekuwa siyo ya kistaarabu,hilo tatizo limeanzia ktk hao hao marafiki zako mnaoheshimiana,iko hivi;

Mimi nikiwa rafiki yako Facebook kisha tena nikawa na urafiki na Hamida wa Kimboka,yeye Hamida kwenye profile yake kuna kile kipengele cha “people you may know" atakuona wewe ambapo akiifungua profile yako ataweza kuona una urafiki na watu gani anaowajua yeye nikiwemo mimi {mutual friends} sasa itakuwa ni uamuzi wake atume friend request au asitume,pia marafiki zake watakuwa wanakuona wewe pale tu unapomkubali Hamida kuwa rafiki yako ambapo nao watafanya the same kama Hamida so utajinasuaje?;

Kama unakumbukumbu ya ulimkubali nani awe rafiki yako ndo hili tatizo likaanza m-search ktk marafiki zako kisha fungua profile yake mu-unfriend,hata kabla ya kumtoa ukitafuta mlolongo wa huyu unayemkataa alikoanzia utajua wengi wa marafiki zake ni wale wote wanaokukwaza,kama hukumbuki basi hao hao uliowa-accept ukakuta ni watu wasiokufaa fungua profile zao angalia anajuana na marafiki zako wangapi kisha hao marafiki zako wa-unfriend pamoja na yeye,ktk hii case lazima kuna mmoja wa rafiki zako anahusika na hilo kundi.

Iliwahi kunitokea kila nikifungua app ya Facebook basi hapo kwenye kioo zinapita friend suggest/request za was*ng3 tupu wengine wamebinua makalio wengine wananyonya vidole alimradi vurugu nikatumia njia hii kuangalia wanatokana nanani?alikuwa pimbi mmoja nilipomtoa ktk kundi la marafiki ujinga ule ukaisha.

Note:usiwa-unfollow hivi utakuwa umenitoa tu mimi ila vitu vingine vyote kutoka kwenye kundi langu utakuwa unavipata wa-unfriend.hope nitakuwa nimesaidia kidogo wengine watajazia nyama nilikosahau.
Niliwahi kufungua akaunti fb miaka ya mwanzoni mwa 2000, nikaanza ku-add marafiki toka Brazil. Kilichonikuta ilibidi niitelekeze ile akaunti mpaka leo nimesahau hata login details zake maana kila habari na watu vyote vilikuwa vya Brazil na location yangu ikahamishiwa Brazil.
Nilijuuta kuifahamu FB
 
Back
Top Bottom