Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
Leo katika piata pita zangu nikiwa na mamaaa(mama kubwa) nikagongana na Ex wangu, nikasalimiana nae vizuri tu huku akitabasamu mpaka mamaa akashtuka na kutaka kuondoka akizani ni Nyumba ndogo, nikamtambulisha kuwa yule nilyenaye ni mke wangu na tuna mtoto mmoja, kasheshe ilianza mara baada ya kurudi nyumbani maana nilishagamwambia tangu niachane na ex wangu sijapata kumwona tena na sijui aliko, sasa mke wangu hajiamini kwa sasa akidhani mie nitaanza contact na yule ex wangu ingawa nimemwambia hilo kwangu halipo na wala asiwaze, jamani bibie hajiamini kwa sasa kila kitu anataja jina la ex wangu, kanitega swali moja, je alikuwa anakufanyia nini x wako wakati wa mechi? jamani niko stranded hapa msaada, na mjue huyo ex yuko fiti kila kona ila tabia yake kwangu haikunifurahisha so tukaachana kwa amani tuuu na sio ugomvi, bibie kauliza mliachana vipi? nani alimwacha mwenzake?haamini kweli tuliachana kwa amani, jamani kwa nini wanawake hawajiamini? nampenda mke wangu na hata number ya yule ex sina ila aliniambia anapofanya kazi kama na muda nimtembeleee....
Msaada jamani, preta, first lady na wengineo, wazee wa jukwaa la mapenzi mpoooooooooo....ndoa yangu jamani ni ya gharama sana maana ni mungu tu ndo anaweza tutenganisha kama kiapo chetu...
Msaada jamani, preta, first lady na wengineo, wazee wa jukwaa la mapenzi mpoooooooooo....ndoa yangu jamani ni ya gharama sana maana ni mungu tu ndo anaweza tutenganisha kama kiapo chetu...