Ezra Chiwelesa: Natambua Juhudi za Hayati Magufuli Kututoa kwenye Pori la Burigi

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,799
Mbunge wa Biharamulo, Ezra Chilewesa akiwa Bungeni ametambua juhudi za Hayati Magufuli kwenye jimbo lake kwa kuhakikisha anawatoa kwenye pori la Burigi ambalo lilitumika kwenye utekaji na unyanyasaji wa watu wa Biharamulo kwa muda mrefu na kuwa sehemu ya kujivunia.

Mbunge Ezra amesema pamoja na hayo, hifadhi hiyo imekuwa na kelele kidogo kwa wakazi wa Biharamulo kutokana na jina la hifadhi. Amedai wakazi hao wameona jina limeifanya kuwa chini ya Chato ilhali sehemu ya mbuga hiyo iko Biharamulo.

Ameomba sehemu yenye neno Burigi ibadilike na liwepo neno Biharamulo na kusomeka Biharamulo-Chato Ntaional Park.

 
Kwa maoni yangu mh.mbunge mwenyewe haijui Biharamulo vizuri, wilaya ya Biharamulo ilikuwa na mbuga za Burigi game reserve pamoja na Biharamulo game reserve , jina Burigi ni jina la asili tangu tunapata uhuru mbuga hizo zilitambulika kwa majina hayo , jina CHATO ndio limekuwa geni na jipya katika mbuga hiyo hivyo ni vizuri kwa kuwa mbuga zilizounganishwa ni za Burigi na biharamulo ni vizuri iitwe BIHARAMULO -Burigi national park neno CHATO linachafua maana na uasili wa mbuga hiyo na ndio Kelele zinapoanzia na kuona mbuga hii ilianzishwa kisiasa na kufurahishana badala ya maslahi ya Taifa nafikiri ni ndio mbunge alichokuwa ana maanisha ila ameogopa kuwaudhi baadhi ya watu kwa kusema anachomaanisha.

Na ukweli ni kwamba hata wanyama waliopelekwa hawakuwekwa ndani ya Burigi na BIHARAMULO game reserve sbb mbuga hizo zina wanyama tangu dunia ilivyoumbwa , wanyama waliopelekwa waliwekwa ndani ya wilaya ya chato ku justify neno la Burigi Chato liwe na nguvu.

majina ya BURIGI na BIHARAMULO game reserve yapo kabla hajutapata uhuru na mbuga hizo zilianzishwa na serikali ya mkoloni chato ndio neno jipya kwenye historia ya Mbuga hizo.
 
Back
Top Bottom