IslamTZ
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 309
- 182
Wizi umetokea wa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni kumi za kitanzania ndani ya nyumba ya Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi. Wafanyakazi wa ndani ya nyumba ambao ni wa Serikali walikamatwa pamoja na wengine watatu ambao ni wajenzi wa kampuni moja binafsi waliokuwa wakifanya matengenezo madogo nyumbani hapo.
Wafanyakazi wa ndani waliachiwa huru na wale wa nje huenda watafikishwa mahakamani karibuni. Fedha hizo inasemekana ni za mtoto wa Mwinyi ambaye inasemekana ni daktari. Fedha hizo alishtukia tu hazipo hajui zilipotea lini na kwa namna gani.
Familia za waliowekwa ndani zinahangaika kuwatoa ndugu zao ambao hawana kabisa historia ya wizi na mmoja wapo ameshuhudiwa akilia kama mtoto.
Jambao la ajabu ni kwamba sheria za kiusalama ni kwamba wakati wa matengenezo mafundi hawaruhusiwi kuingia vyumbani bila mlinzi.
Katika mchakato wa dhamana pale mahakama ya Kinondoni Hakimu amelamba 100,000 kutoka kwa familia hizo tatu za watu masikini, huku afisa mzungusha faili akichukua 30,000.
Uonevu mtupu!!
Wafanyakazi wa ndani waliachiwa huru na wale wa nje huenda watafikishwa mahakamani karibuni. Fedha hizo inasemekana ni za mtoto wa Mwinyi ambaye inasemekana ni daktari. Fedha hizo alishtukia tu hazipo hajui zilipotea lini na kwa namna gani.
Familia za waliowekwa ndani zinahangaika kuwatoa ndugu zao ambao hawana kabisa historia ya wizi na mmoja wapo ameshuhudiwa akilia kama mtoto.
Jambao la ajabu ni kwamba sheria za kiusalama ni kwamba wakati wa matengenezo mafundi hawaruhusiwi kuingia vyumbani bila mlinzi.
Katika mchakato wa dhamana pale mahakama ya Kinondoni Hakimu amelamba 100,000 kutoka kwa familia hizo tatu za watu masikini, huku afisa mzungusha faili akichukua 30,000.
Uonevu mtupu!!