Exclusive: Ripoti ya Uchunguzi wa Vifo Tarime - Marehemu walipigwa mgongoni wakikimbia

May Tundu Lisu's courage and character be a source of strength to all the oppressed in this country's mineral sites at this time.
 
Ingekuwa serikali yetu imetokana na wananchi basi tungeshuhudia sheria kuchukua mkondo wake ila kwa serikali imetokana na mtutu wa bunduki kupitia chakachua ni wazi serikali ipo kwa kuwa waliopewa silaha kutulinda kwa mujibu wa sheria, ndiyo walinzi wao wa madaraka na kuwachukulia hatua za kisheria walinzi wako wa madaraka ni kuwafanya next time wasivunje sheria ili kukulinda wewe na hivyo YOU WILL LOSE POWER. Hapa kuna MUTUAL BENEFIT kati ya polisi na serikali ya CCM. Wote wanalindana, Kamwe hutakuja sikia serikali ya CCM ikichukulia hatua askari wanaoua watu kwa makusudi.

Katika nchi za wenzetu hilo halipo, mfano ni kule UK yule askari aliyemsukuma mtu wakati wa mkutano wa G20 London na muda mfupi mtu huyo akapata heart attack na kufariki anapandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya kuua bila kukusudia, Iweje sisi polisi wanaowalenga watu wanaokimbia na kuwaangamiza kama waarab wanavyocheza mochezo ya uwindaji wa wanyama wetu kuwa kimilikishwa vitalo. Yaanii analenga mnyama pori kisha anaangalia kampiga risasi ya wapi moyo, mapafu, maini na kujipatia points. Leo hii Tanzania ina train KILLERS wa raia wema wasiokuwa na silaha za moto? Kisa kutoa demonstration kwa waliobaki waogope kurudia tena kitendo fulani?, Yaani mpaka leo bado wanatumia PAUL SOZIGWA'S THEORY, Kill the front liners as demo others will not repeat. Wajue kuwa Mwanadamu wa leo si nyani wala tumbili ambaye akiona mwenzake kauwawa kwenye shamba la mazao na mwili wake kuning'izwa basi hawarudi tena kwenye shamba hilo kuharibu mazao, mwanadamu anatakiwa kuwa unleashed, ajisikie yupo huru na hilo linaweza fanyika kidiplomasia badala ya kutumia risasi. The more you kill people the more strong the escaped ones will be, they will have revenge minds which are worse than bullets.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, UTUEPUSHE NA VIONGOZI WENYE UWEZO FINYU WA KUFIKIRI KWA NIABA YA MAJORITY ILI KULINDA, MAWAZO YA UPENDO NA KUSAIDIANA MIONGONI MWETU SI KUANGAMIZANA.
 
Kwa nukuu hii hapa chini umemaliza kila kitu:


1. Polisi walikusudia kuua na sio kudhibiti watu waliowaita wavamizi, kwani kwa mjibu wa force law, hawakutakiwa kupiga risasi sehemu yoyote tofauti na miguuni.

2. Polisi waliwapiga risasi watu waliokuwa wakikimbia kutoka eneo hilo, kwani risasi zote zimepenya kwa upande wa nyuma wa mwili na zikatokea upande wa mbele wa mwili.

Sasa kama taarifa hii ni sahihi nini kifanyike?
Ushauri wangu kama serikali na chama tawala kingekuwa kinasikia ushauri wa wananchi wake, Waziri na IGP wake wangekuwa wastaarabu
kama wangewajibika hata kabla hawajawajibishwa. kwani dhamana waliyopewa imewashinda, matukio ya aina hiyo yamekuwa mengi.

Nina sikitika kwani kwa sehemu ndogo ninavyomjua Said Mwema kiutendaje sijui nini kimemsibu.Amekuwa mtendaji mzuri tangu akiwa OC-CID pale Osterbay Police miaka ya 80s na akaja kuwa RCO hata kuwa RPC. Ni msomi mzuri na mtendaji mzuri. Lakini kwa vile cheo ni dhamana anabidi awajibike.

Tukumbuke mauaji ya Shinyanga ya kina Twiga Mazegenuka; Mzee Kawawa(waziri Mkuu),Mzee Mwinyi(waziri wa mambo ya ndani) Mzee Kigadye(mkuu wa usalama wa taifa) n.k waliwajibishwa wengine wakafungwa. Huo ndo ulikuwa wakati wa uwajibikaji. Tunahitaji kurudi kwenye zama hizo.

Matatizo makubwa abayo yanajitokeza sasa hivi ni kwa vile viongozi wanaoshindwa majukumu yao hawawajibishwi, jambo ambalo lina paka matope serikali na watendaji wake ambao ni waadilifu.
 
Hakuna mtu anaeshangilia mwenzie kufa lakini watu watajadili kifo chake,umesema unahisi kuwa alichomwa na singe na wakati huohuo unasema hakuna aliyepambana na polisi na kwamba walipigwa wakiwa mbali wanakimbia je hiyo singe unayoihisi ilifyatuka kama risasi? halafu haujawaeleza wana JF hilo tundu la "singe" lilikuwa upande gani wa mwili? na je mbona haujaonesha wasiwasi wako juu ya daktari aliyefanya hiyo post motum?kwani yeye ndio final say wa hiyo post motum na hakuona hiyo "singe" uliyoiona wewe.Palipo kweli ongea kweli na pale ambapo hapana ukweli usiongee.

Maswali yako Ziada yangekuwa na mantiki sana kama tu autopsy hiyo ingefanyika one day after shooting, kuzuia polisi kwenda mortuary na kumchoma singe maiti huyo ili baadae ionekane kuwa ilikuwa ni face to face fight baada ya kupata pressure ya kuanyika uchunguzi kabla ya kuzika. Labla swali lako lingekuwa na maana zaidi kama ungemuuliza Nyakarungu kuwa je, jeraha hilo linaoneka lilipatikana wakati mwili ukiwa bado unacirculate blood?, Kama jeraha hilo halioneshi damu kuganda inamaanisha kuwa lilitengenezwa wakati mwili ukiwa functionless.

Nyakarungu amesema kuwa jeraha hilo ni addition ya la awali la risasi, ni dhahiri kuwa risasi ilianza na baadae singe ikafuata na kama hivyo ndivyo basi polisi walikuwa ama wanammaliza marehemu afariki haraka(Dhamira ni kuua) au walifanya hivyo kwa makusudi kwenye dead body in Mortuary. Kama nguo za marehemu zingepatikana ni dhahiri zingekuwa zimetoboka ila kwa kuwa walimchomea singe ama mortuary amba muda mfupi baada ya kuanguka akiwa agony ni dhahiri mchomaji atapekenyua nguo au alifanya hivyo wakati nguo zikiwa zimetolewa mortuary walipohifadhiwa marehemu hao.
 
Naomba niwaulize wataalamu wa international and criminal law swali, hivi mtu au kikundi cha watu hakiwezi kupeleka mashtaka yao ICC ili prosecutor wake aje afanye uchunguzi? coz hii si mara ya kwanza sababu nafkiri Nyamongo ni kama mauaji ya tatu kama niko wrong naweza sahihishwa halafu haya mashtaka yakawa joined na matukio mengine ya unyama na mauaji yanayofanywa na wawekezaji ktk migodi ikibidi hata issue ya Bulyanhulu iwe raised. Kwa upande wangu katika haya kuna Crime against humanity, kuna vitendo vya uzalilishaji, na pia kuna mass killings. Na uchunguzi huru ufanyike na Barrick Gold na wao wajumuishwe kama chachu ya mauaji coz nafkiri kuna influence yao pia. Kwa hili siziamini kabisa mahakama za Tanzania kama zitatenda haki simply because they are not independent they have been bound with this corrupt political system. Kama la ICC linawezekana now its time to take a step foward.

Pukudu @Ilkiding'a Arusha
 
Nikifa nikumbukwe kwa kusema ukweli, nitasimama mahakamani kwa ujasiri wangu na kwa nguvu ya Mungu, nitaunena ukweli hadharani, bila hofu na kwa kuheshimu kiapo changu cha maadili na uaminifu akatika fani yangu,
Naingoja hatima ya haki za wana ndugu za marehemu niione.
 
Nikifa nikumbukwe kwa kusema ukweli, nitasimama mahakamani kwa ujasiri wangu na kwa nguvu ya Mungu, nitaunena ukweli hadharani, bila hofu na kwa kuheshimu kiapo changu cha maadili na uaminifu akatika fani yangu,
Naingoja hatima ya haki za wana ndugu za marehemu niione.

Nyakarungu Mungu akubariki sana, ubarikiwe kila njia upitayo and God will never leave you alone
Amani iwe nawe siku zote:
 
Nimeelewa ni kwa nini polisi walitaka hawa watu wazikwe mapema....na laiti hilo wangefanikiwa uovu huu usingefahamika
 
Ardhi ya nyamongo na Tarime inakunywa damu ya wasio na hatia ipo siku haki itapatikana
 
HABARI ZENU WANAJAMII!!!!!!!!!?

Nafahamu nyote mwajua tukio la Tarime, la wananchi kuuwawa na jeshi la polisi huko migodini Nyamongo Wilayani Tarime,tarehe juma lililopita.

Wafiwa wallitaka kujua undani wa mauaji ya ndugu zao, ili waweze kufuata njia za kisheria za kudai haki yao ya kisheria.

Ililazimika uchunguzi wa kitaalam ufanyike ili ukweli ujulikane...
Uchunguzi huu ulifanywa jana na mtaalam wa uchunguzi wa aina hii (Post Motum) ya kitaalam, Dr Makata kutoka wizara ya afya kitengo cha dharura matukio tata.
Kwa upande wa wafiwa waliwakilishwa na Grayson Nyakarungu, aliyepewa imani na chama pia kuhakikisha ukweli ndio unaletwa hadharani.
Pia jeshi la polisi na Hospitali ya wilaya ya Tarime walikuwa na wawakilishi wao.
Tuliifanyia miili mnne kati ya mitano, ya watu walio uwawa, kwani mwili mmoja ulishazikwa kwa kuibiwa na polisi.

IFUATAYO NI TAARIFA HALISI TULIYOTOKA NAYO BAADA YA UCHUNGUZI WA WETU, KWA KULINDA NA KUHESHIMU UADILIFU WA TAALUMA YETU YA KIAFYA.

KIAPO NILICHOAPA HUKO CHUONI (MEDICAL ETHICS)
1. Kile kinachoonekana katika vipimo/uchunguzi, ndicho kinachotakiwa kuwekwa wazi kwa muhusika.
2. Sitakeuka wala kughiribu utu wa mtu kwa sababu zozote zile.

Hizo ni chache tu kati ya Medical Ethics nyingi, ambazo niliapa kuzilinda na kuzisimamia.

POST MOTUM ROOM
Tulianza kazi hii saa 10:25 A.M hadi saa 16:57 P.M baada ya wafiwa kuitambua miili ya ndugu zao.

1. Mwili wa Emmanueli Magige
P.M No 1-5-11
T.G.H
Entrance site: Left illiac cleft (upande wa kushoto wa juu ya nyonga)
Wound size: 0.5 cm diameter the wound was round.
Exit site: Lumber region back (juu ya kiuno kidogo karibu na uti wa mgongo)
Wound size: 2.5 cm diameter

Positive findings;-
-Blood vessels/Nerves and surrounding muscles were destroyed.
-The clavicle bone was destroyed and blood clots was seen, ( mfupa mkuu wa kiuno na nyonga uliharibiwa na damu nyingi ilivuja na imeonekana imeganda humo)

But beneath the exit site, there was a cut wound, 2.5 cm diameter.

Lakini kulikuwa na alama ya jeraha kubwa linaloonyesha alama ya kuwa kitu chenye ncha kali kilichoma, na hii ilileta hisia tofauti, polisi walihisi kuwa aliangukia jiwe au kijiti kilichomchoma, kwa hili tulibishana na tukaamua hakuna jibu la nini kilichoma, ila mimi nilihisi na kusimamia kuwa alichomwa na singe ya bunduki, na ndipo niliomba nguo zake zitafutwe ili tuzichunguze na tubaini ukweli, hata hivyo hazikupatikana.

2. Mwili wa Chacha Ngoka
P.M No. 2-5-11
T.G.H

Entrance site: Right side of the body back 16 cm from illiac (usawa wa bega chini na juu ya kiuno, nyuma ya mwili.
Wound size: 0.3 cm diameter
Exit site: In 5th intercoastal muscle right side, 2cm from the nipple.
Wound size: 5cm diameter

Positive findings
Major blood vessels were destroyed
Midle and right lobe of liver were destroyed led to laceration
In the Trachea, blood clot was seen.

3. Mwili wa Chawali Boke.
P.M No. 3-5-11.
T.G. H

Entrance site: Occipital bone 8cm from the Pinna, (Kisogoni sm 8 kutoka sikio la kushoto)
Wound size: 0.2 cm diameter
Exit site: In parietal bone ( kwenye paji la uso pembeni kidogo)
Wound size: 5cm diameter

Positive findings;-
The brain and inner part of the head was destucted, blood clots was seen, this was due to blood aspiration.

4. Mwili wa Mwikwabe Marwa Mwita
P.M No. 4-5-11
T.G.H
Entrance site: Left illiac cleft (upande wa kushoto juu ya nyonga)
Wound size: 3.5 cm diameter
Exit site: It was not pass through, it remained intact.
Wound size: None

Positive findings;-
There was worse destruction of;-
-Femoral artery
-Femoral vein
-Sorrounding muscles
- Fructure of illiac bone ( mfupa wa nyonga na uzazi)
- Piece of lead was seen lying deeply inpsoas muscle, surrounded by bone fragments

Msimamo wangu kimaadili na na kibinadamu;-

1. Polisi walikusudia kuua na sio kudhibiti watu waliowaita wavamizi, kwani kwa mjibu wa force law, hawakutakiwa kupiga risasi sehemu yoyote tofauti na miguuni.
2. Polisi waliwapiga risasi watu waliokuwa wakikimbia kutoka eneo hilo, kwani risasi zote zimepenya kwa upande wa nyuma wa mwili na zikatokea upande wa mbele wa mwili.

HIVYO wananchi hawa hawakupambana na polisi, bali walipigwa risasi wakiwa wanakimbia, ndio sababu ya risasi zote kuingia sehemu za nyuma za miili yao.
Mungu watazame waja wako na uwalinde na yote aliyoyaandaa SHETANI.

MUNGU AWALAZE PEMA PEPONI AMINA, NITAKUWA SHAHIDI MWEMA NA MSEMA UKWEI KWA KUUENZI UTU.


Jamani Watanzania wenzangu hii hali itaendelea hivi mpaka lini? kwanini tusiseme sasa huu ndiyo mwisho wa kunyanyasika, inatia uchungu na inauma sana kuona Mambo kama aya na Polisi wa kulinda raia wakiwa uwa Wenzetu kama wanyama.
Tuseme Mwisho wa hii Serekali ndiyo huu, we can't take it any more !!!
Nipo tayari kupoteza maisha kwa kutetea haki yangu.
RIP wote mlio poteza Maish.
 
Nyakarungu ahsante mzee naomba un PM tujadili upenuni maana maiti ya huyo kijana Boke imeachwa barabani na Polisi
 
Kikwete hajatuma hata salam za rambirambi! Hana uchungu na hawa eeeeh! Mungu yupo na mapambano ya kudai haki hayawezi kuzimwa kwa mtutu. Eeee Mwenyezi Mungu, sikia kilio cha waja wako na ukawalipie coz hii vita ni yako.
 
Tarime nightmare Wednesday, 25 May 2011 00:09

By Beldina Nyakeke
The Citizen Correspondent


Police yesterday failed in their bid to force relatives of four of the five people shot dead at the North Mara gold mine last week to bury them.The victims were shot dead by police after they allegedly invaded the mine on May 16.There was heightened tension when police collected the bodies from the Tarime District Hospital mortuary against the wishes of the deceased’s relatives.But the Tarime/Rorya Special Police Zone Commander, Mr Constantine Massawe, said they had decided to collect the bodies from the mortuary and take them to their homes after their families agreed to bury them.However, some of the coffins bearing the bodies were dumped by the roadsides.

The one bearing the remains of 27-year-old Emmanuel Magige was left by the roadside in Nyakarungu Village.On Monday, it had been agreed that Chadema hold a farewell rally for the victims in the afternoon at the local stadium, but police later cancelled the event on security grounds.At around 10pm, armed police officers arrived at the Tarime District Hospital in about 10 vehicles, and took the bodies away.

Eyewitnesses said two bodies were ferried to Bonchugu Village in Serengeti District. Police dumped the coffin containing the remains of Chawali Bhoke after firing tear gar at his relatives following their refusal to accept it.


Tensions mounted when police arrested several Chadema officials, including Shadow Constitutional Affairs and Justice minister Tundu Lissu, who was in Tarime to assist the victims’ relatives.

Mr Lissu, a lawyer, was charged at the Tarime District Court along with Mr Mwita Waitara, Mr Stanslaus Nyembela, Mr Anderson Chacha and Mr Andrea Andalu with unlawful entry into the Tarime District Hospital mortuary.
The prosecution told the presiding magistrate, Mr Yusto Ruboroga, that the accused also conducted an illegal meeting and obstructed a medical officer from carrying out his duties.They denied the charges, but were still in custody awaiting the court to rule on their bail applications by the time we went to press.

Chadema Special Seats MP Esther Matiku and a number of journalists, including this reporter, were also arrested for allegedly instigating violence.They were seized on their way to Kewanja Village, where police delivered one of the bodies, and recorded statements at Nyamwaga Police Post before they were taken to Tarime Police Station. They were released in the afternoon, and told they could be summoned soon.

In Dar es Salaam, Chadema pledged to assist the victims’ families to sue the government.Party official Mabere Marando, a lawyer, said in the presence of Chadema founder Edwin Mtei and former chairman Bob Makani that the families had been advised to collect evidence that would enable Chadema lawyers to help them initiate legal proceedings against the government.

“We are collecting evidence against the government following the killing of innocent people at Nyamongo. They did not deserve to die like that irrespective of whether or not they were criminals,” he said.Mr Marando said they had directed Chadema MP John Mnyika to inform the Clerk to the National Assembly, Dr Thomas Kashillila, of the “illegal” arrest of Mr Lissu and Ms Matiku.“Two of our MPs have been arrested while observing the police taking the bodies from the mortuary against the wishes of family members,” he said.

Mr Mtei, a former Finance minister, attributed the killings to the government’s ignoring of Mwalimu Julius Nyerere’s vision on mining the sector. He said Mwalimu was against privatisation of mines for fear of such deadly conflicts.
In Tarime, Mr Massawe said police were holding eight people on suspicion of holding an illegal meeting and incitement, and confirmed that Mr Lissu, the Singida East MP, was among those arrested. He said the suspects had gathered at the hospital at around 8pm on Monday, posing as the victims’ relatives.

Mr Massawe defended the police against the allegations of sparking chaos when they stormed the mortuary, saying it was people who had gathered at the hospital who were looking for trouble.Meanwhile, Zanzibar First Vice-President Seif Shariff Hamad yesterday urged the Union government to find a lasting solution to the recurring conflicts around the North Mara gold mine.

“We can’t continue pretending that something is not wrong...the government and Tarime residents need to sit down and find a peaceful way of solving the existing problems,” said Mr Hamad, who is also secretary-general of the Civic United Front (CUF).
 
Hapa kama haya ni kweli, wafiwa ni kumuomba mungu awasaidie na kuwafariji kwa njia yoyote maana hawa wauaji wana bunduki tulizowapa wenyewe kwa kura zetu kupambana sasa na polisi wenye silaha ni suicide. tutumie busara na subira na kusubiri wakati mwafaka wa kudai haki. kwa sasa taratibu za amani zitumike mwenye akili ameelewa. pia tusubiri upande wa serikali una nini la kweli kutueleza hapa? Waeleze ukweli kati ya haya tunayosikia mimi naamini quick response ndiyo inatoa ukweli. hapa ni facts tu hakuna cha kujificha katika pazia la udini au siasa.
 
(1)Mahakamani ni nani ataendesha mashtaka? Ni Jeshi la hao hao Polisi?

(2) Tangu lini Polisi wakiua raia Tanzania wanafanywa lolote? Wale waliouwa watu Arusha bila sababu wamefanywa nini?

(3)When will enough be enough?
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom