Kuna mwaka tutapishana na watu barabarani hawajavaa nguo kabisa na wala hawana matatizo ya akili! Kweli nguo inafika imekuacha wazi mpaka mfereji wa makalio uko nje kweli mtu anaona ni sawa tu! Hata kama ni uhuru wa mavazi kwa mvaaji, na wavaaji wajue stara ni nini khaa...
Na REDDS nao kama ndio wako behind the idea of such tiny costumes to those ladies, wanastahili fungu lao la lawama pia!
... Ule muda wa sheria ya mavazi Tanzania umewadia..!! Si Hijabu Ninja Type.., [Pweza Paolo anajua]., Ni mavazi ya heshima yenye kumsitiri mtu. Wanaharakati tunakuna vichwa hapa...:confused2:
Huo unaitwa utumwa na umaskini wa fikra. Kila wanachofanya wenzetu "weupe"sisi tunaiga kwa kufikiri ndio bora na sahihi. Wameendelea kutuita maskini, nasi tunakubali kuwa ni maskini. Inawezekana ni kweli maskini, maskini wa fikra.
Napata tabu kujua kwa dhahiri kama promotion hii inahusu redds au hawa ladies wenye business isiyosemwa bayana;maana kwa kuangalia picha hizi naona kuna promotion inayoweza kuvuta mawazo ya watu zaidi ya ile iliyokusudiwa.
Nilishawahi kusema ipo siku badala ya kuacha sehemu ya matiti kina dada wataacha sehemu ya ****** naona kauli yangu inatimia sasa.. hizi ni fasheni tu na hii itapita!
sometimes huwa najiaminisha kuwa tunaoishi hapa duniani wote si lazima tuwe wanadamu wa kawaida...nadhani pia kuna idadi ya kutosha ya majini na maajenti wa shetani kati yetu! tunaishi nayo....yanashiriki katika matamasha mbalimbali na hujiingiza pia kwenye vinyang'anyiro...... mix with yours
Hivi Tanzania kuna "Reed Dance"? Hayo mambo nilikuwa nayaona kwa King Mswati kumbe na TZ tumenogewa na tunaaza taratibu kupenyeza huo mfumo kwa gharama ya Bia?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.