Excel kupanga matokeo, divisions na points

castongo

Member
Mar 16, 2008
56
67
Watu wengi wamekua wakiuliza swali hili, hasa wale wanaofanya kazi kama waalimu, ambao wanatakiwa kuwa-grade wanafunzi kulingana na matokeo ya mitihani kwa kutumia Microsoft excel.
Nimeona watu wengi wametoa maelekezo kwa kutumia function ya "If" na ndiyo niliyokua naijaribu katika kutatua tatizo hilo lakini baadae nimeona ni ndefu sana, na mahali fulani unaweza kujivuruga wakati wa kupanga mambo. Kwa mfano nilikua naangalia maelekezo ya Kyatsvapi akiwa anajibu swali hilo. Ni njia nzuri na ndiyo niliyokua natumia kwa muda mrefu.

Lakini nilikua nafikiria Kutumia function ya "Vlookup" kupanga points na baadae kutumia function ya "sum" pamoja na ya "small" Kupata divisions.
SASA TWENDE HATUA KWA HATUA.
Kwanza, nina wanafunzi wangu
upload_2016-12-30_21-12-44.png

Na hizo ndo marks zao.
Pili
Mahali fulani kwenye excel yangu natengeneza refference table yangu
upload_2016-12-30_21-19-4.png

Column ya kwanza ni Marks ya pili kama unavoona ni kwamba mark inaangukia kwenye A au B,C nk ya tatu ni points husika.
Tatu
Naenda kwenye cell ambayo nitacopy table ya matokeo na badala ya marks table itaniletea sasa Points kwa kila somo lililo kwenye table ya matokeo.
Namna rahisi ni kwa kutumia alama "=" Naiweka mahali ninapo taka table yangu itokekee,
kisha naclick cell ya juu kushoto ya table yangu
upload_2016-12-30_21-27-57.png


kisha enter
cell niliyochagua itajirudia kwenye point niliyo chagua
Kisha na-drag kwenda kulia kwa kushika dot ya chini ya cell
upload_2016-12-30_21-32-19.png

Mpaka row yote itokee namna hii
upload_2016-12-30_21-33-50.png

halafu naselect tena cell mbili za kushoto kabisa, maana column ya sex itajirudia
Nashika dot kwenye kona ya cells hizo na kudrag chini
upload_2016-12-30_21-41-34.png

Hadi cell za kwenda chini zitokee
upload_2016-12-30_21-42-45.png

Table yangu ipo tayari kwa kujaza points
upload_2016-12-30_21-43-40.png

Hapa ndio tunaanza kuweka mambo ya "Vlookup" na tunaanza na cell yenye marks za Biology za mwanafunzi Chungwa Tamu. pale andika alama ya sawasawa, kisha vlookup kisha fungua mabano =vlookup(

upload_2016-12-30_21-55-34.png


Kisha click Marks za biology za Chungwa Tamu kwenye ile table yenye marks
upload_2016-12-30_21-58-4.png


bonyeza mkato , Kisha select ile table ya refference yote
upload_2016-12-30_22-0-41.png

Bonyeza F4 ili alama za dolar zitokee kwenye hiyo refference, au table array

upload_2016-12-30_22-3-21.png

Bonyeza mkato tena tayari kwa kuweka return value ya table ya refference, ambayo ni column ya value unayotaka irudi. Ka case yetu ni column ya tatu

upload_2016-12-30_22-6-14.png


Kwa hiyo baada ya mkato tunaweka 3
Mkato tena, sasa hapo kuna true na false. True kama ni approximate match, au False kama ni exact match. Lakini kwasababu kenye refference table yetu kutoka 0 hadi 30 kuna namba katikati na zinatakiwa zikadiriwe kuwa ni poit 5 au 4 kwahiyo jibu letu ni True approximate.
Sasa kitu chetu kitaonekana hivi
upload_2016-12-30_22-11-54.png


Hapo gonga enter. Na utaona 1 inatokea ikimaanisha 89 ambayo ni marks ya Chungwa tamu katika Biology, ikipimwa na table yetu inakua ni point 1.
Sasa shika tena kona ya cell hiyo na uivute hadi mwisho
upload_2016-12-30_22-15-17.png


Kisha ushike tena kona hiyo uivute hadi chini
upload_2016-12-30_22-17-1.png


Na kila kitu kitakua kimejaa kwa mwendo wa point.

Wamenikataza nisiongeze picha. Naomba niishie hapa kwanza. Halafu nitaendeleza kwa mwendo sasa wa division na kumalizia kila kitu. Kimsingi maelezo ni mengi sana, lakini unapokuja kwenye uhalisia na kuelewa itakua ni kitu cha dakika chache tu. Pia kuna mambo ya kurahisisha, kwa mfano baada ya kudrag kwa kukatisha, unapotaka kujaza kwa kwenda chini select viboksi vitupu vya chini kisha bonyeza control na D.
Nitaendelea. Baadae nitaleta sample na utaona ni rahisi sana.
 

Attachments

  • upload_2016-12-30_20-32-49.png
    upload_2016-12-30_20-32-49.png
    15 KB · Views: 509
  • upload_2016-12-30_21-25-39.png
    upload_2016-12-30_21-25-39.png
    634 bytes · Views: 422
  • upload_2016-12-30_21-36-10.png
    upload_2016-12-30_21-36-10.png
    4.4 KB · Views: 418
  • upload_2016-12-30_21-37-23.png
    upload_2016-12-30_21-37-23.png
    4 KB · Views: 425
Asanteni sana wadau. Nashukuru.
Sasa table yetu ikijaa itafanana namna hii

upload_2016-12-31_12-16-2.png


Kwa maelezo kifupi, tuangalie function ya Vlookup, na utaratibu tulio tumia.
Katika utaratibu wetu tumekua na table A, B na C kama ifuatavyo.
(A)Table original, ambayo ina majina ya wanafunzi na Marks zao
(B) Table ya refferences, ambayo ina mgawanyiko wa scores na points kulingana na Marks. Kwa mfano 45 ni alama C na pia ni 3 points.
(C) Table mpya inayotengenezwa, inayoonyesha sasa points kwa kila somo katika table A, kulingana na utaratibu ulio katika table B.

Function ya vlookup yenyewe imegawanyika katika sehemu 4. Sehemu hizo zinaonekana baada ya kuandika "=vlookup(" na sehehemu hizo hutenganishwa kwa alama ya mkato","
Kwa mfano wetu function yetu ilionekana kama hivi "=vlookup(E3,$A$19:$C$24,3,True)
hapa ukitazama kila baada ya mkato utagudua kuwa sehemu hizo ni nne:-

(1)="E3"
ambayo ni cell (kiboksi) katika table A (original) yenye Maksi unayo taka kubadili kuwa Point. Kawaida hii italinganishwa na column ya kwanza kabisa / ya kushoto kabisa, katika selection ya Table B

(2)="$A$19:$C$24
ambayo ni range (mipaka) ya table B (refferences). Kawaida range hiyo ingekuka hivi A19:C24, Lakini alama za dola "$" zinaongezwa ili range ya Table B isisogee wakati unapo drag kujaza cells "vyumba/viboksi" kwenye table ya matokeo (Table C).
Alama hii ya dola huongezwa kirahisi kwa kubonyeza key "F4" unapokua umechagua mipaka ya Table B.

(3)="3"
Kama nilivyo sema awali, ni namba ya column ikihesabiwa kutoka kushoto katika Table B. Kwamba ni katika column ipi (yangapi toka kushoto) ya Table B, utataka kitu kipelekwe kama jibu kwenye Table C, endapo namba uliyochagua kwenye Table A itafanana na yoyote iliyo katika column ya kushoto katika table B. (sijui nimechanganya maneno au imeeleweka?)

4)="True"
Hapa tunatakiwa tujaze "True" au "False". Kwamba namba iliyochaguliwa kwenye Table A inafananaje na namba iliyo katika column ya kushoto ya Table B. Hapa tuna True ambayo ni approximate match na False ambayo ni Exact match",
Kwa kilugha chetu tungesema "ni (TRUE), inayohusiana nayo kiaina au NI (FALSE) kwamba ni yenyewe moja kwa moja". Kama ni inayohisianahusiana nayo tunasema "True", kama ni yenyewe moja kwa moja tunasema "False". Kwa hiyo Maksi 0hadi 29.999, inahusiana na 0, na maksi 31 hadi 44.999 inahusiana na 30. Kama kwa mfano wetu, tungekua tumeweka False, manake namba ambazo zingerudisha majibu toka table A ni zile zenye 0, 30, 45, 65 na 75 tu. Nyingine tofauti na hizo zingeleta error (kosa).

Sasa kwa uelewa huu, Tukirudi kwenye matokeo yetu katika Table C, ambayo tulikua na points. Tukizifuta na kubaki na kiboksi kimoja, cha kwanza juu kushoto,

upload_2016-12-31_12-18-26.png


"ilitusipoteze formula yetu" Kwenye formula ya Vlookup tukirekebisha kipengele namba tatu. Badala ya "3"
Tuweke "2"

upload_2016-12-31_12-20-9.png

Kisha Enter.
Tukidrag,(kuvuta) kushoto kisha chini.
Matokeo yatakua sasa kwa alama badala ya Points.

upload_2016-12-31_12-22-5.png


Naomba tena niishie hapa kwa sasa. Baada ya muda nitarudi na suala la Division.
Mchana mwema.
 
Kupanga division huwa yanachukuliwa masomo 7 ambayo mwanafunzi anakua amefualul vizuri zaidi. Somo ambalo mwanafunzi amefaulu zaidi linapoints chache zaidi, kuliko lile alilofeli. Hapa tunatumia Table C. Tunacho hitaji ni masomo 7 yenye points chache zaidi. Hivyo katika masomo 9 tutatafuta 7 yenye points chache zaidi kuliko mengine.
Njia ya kufikia hiyo ni kwa kutumia function ya "Sum" pamoja na function ya "Small"

SUM (kutafuta jumla)
Mara nyingi tumezoea kuandika function ya sum ikiwa na range (mipaka) ya cells (viboksi) tunavyotaka. Kwa mfano "=SUM(E28:M28)" ambavyo cells zilizo kati ya E28 na M28. Lakini vipengele vya sum pia vinaweza kuandikwa kimoja kimoja vikitenganishwa kwa mikato. Kwa mfano "=SUM(E28,F28,G28,H28,I28,K28,J28,L28,M28,)"

upload_2017-1-1_12-14-55.png

Nimefanya hivi ili tuelewe kwamba vipengele vya sum vinavyotenganishwa kwa mikato, vinaweza kuwa function nyingine. Na hii function nyingine kwa case yetu ni "SMALL"

SMALL (Ndogo)
Function hii ina vipengele viwili, ambavyo vinatenganishwa kwa mkato vikiwa ndani ya mabano. Vipengele hivi ni Array (Mipaka), ni katika eneo gani unatafuta ndogo. Kipengele cha pili ni " Ndogo ya ngapi" Ndogo ya kwanza (1), ni ndogo kuliko zote, Ndogo ya pili (2) ni kubwa kuliko ndogo ya kwanza nk. Kwahiyo kwa mfano function "=SMALL(E28:M28,3)" itanipa jibu 3. Kwamba ni thamani iliyo ndogo ya tatu kwenye table yetu.

upload_2017-1-1_12-10-47.png


SUM na SMALL
Function ya "Small" inaweza kubebwa ndani ya function ya "Sum"
Angalia kwa makini

upload_2017-1-1_11-52-35.png


Ni ndefu sana. Lakini inaweza kuandikwa kwa kufupisha kama namna hii
=SUM(SMALL(E28:M28,({1,2,3,4,5,6,7}))).

upload_2017-1-1_12-7-21.png

Utapata kitu kile kile. Ni mambo mengine ya Excel. Kwamba kwa namna flan ({1,2,3,4,5,6,7}) kipande hicho kinachezesha function zote mbili.
Drag chini kupata nyingine zote.

upload_2017-1-1_12-18-48.png


Utakua umepata jumla ya points.
Tengeneza table ya refferences za division (Tuiite table D) na utumie utaratibu wa "Vlookup" tulivyojifunza awali, kutengeneza divisions.

upload_2017-1-1_12-0-47.png

Kumbuka kwamba jumla ya points ndio inakua kipengele cha kwanza cha function ya vlookup, na range hapo ni ya table yetu mpya table D.

upload_2017-1-1_12-32-18.png


Kwa bahati mbaya inaonekana wanafunzi wangu watakua wanalingana sana.

Kuna changamoto kwamba table inapokua na points ndio unaweza kukokotoa jumla ya points (kwa sum&small) na dividions (kwa vlookup), lakini mwishoni unataka uwe na Alama, kama vile A, B nk badala ya points kwenye table yako.

upload_2017-1-1_12-36-17.png


Tumia utaratibu wa ku-copy columns za Points na divisions na kuzi-paste-values palepale ili kuondoa formulas ili columns hizo zibaki bila kubadilika. Kisha pale ilipokua 3 na kuifanya kuwa 2 kwenye function ya vlookup kama nilivyoonyesha juu. Badili cell ya kwanza juu kushoto kisha drag kulia na chini kusudi sasa ziwe alama A, B nk.
Wadau naomba kama mna chochote cha kurekebisha, kurahisisha, tusaidiane tutajirishane.
 
Kupanga division huwa yanachukuliwa masomo 7 ambayo mwanafunzi anakua amefualul vizuri zaidi. Somo ambalo mwanafunzi amefaulu zaidi linapoints chache zaidi, kuliko lile alilofeli. Hapa tunatumia Table C. Tunacho hitaji ni masomo 7 yenye points chache zaidi. Hivyo katika masomo 9 tutatafuta 7 yenye points chache zaidi kuliko mengine.
Njia ya kufikia hiyo ni kwa kutumia function ya "Sum" pamoja na function ya "Small"

SUM (kutafuta jumla)
Mara nyingi tumezoea kuandika function ya sum ikiwa na range (mipaka) ya cells (viboksi) tunavyotaka. Kwa mfano "=SUM(E28:M28)" ambavyo cells zilizo kati ya E28 na M28. Lakini vipengele vya sum pia vinaweza kuandikwa kimoja kimoja vikitenganishwa kwa mikato. Kwa mfano "=SUM(E28,F28,G28,H28,I28,K28,J28,L28,M28,)"

View attachment 452874
Nimefanya hivi ili tuelewe kwamba vipengele vya sum vinavyotenganishwa kwa mikato, vinaweza kuwa function nyingine. Na hii function nyingine kwa case yetu ni "SMALL"

SMALL (Ndogo)
Function hii ina vipengele viwili, ambavyo vinatenganishwa kwa mkato vikiwa ndani ya mabano. Vipengele hivi ni Array (Mipaka), ni katika eneo gani unatafuta ndogo. Kipengele cha pili ni " Ndogo ya ngapi" Ndogo ya kwanza (1), ni ndogo kuliko zote, Ndogo ya pili (2) ni kubwa kuliko ndogo ya kwanza nk. Kwahiyo kwa mfano function "=SMALL(E28:M28,3)" itanipa jibu 3. Kwamba ni thamani iliyo ndogo ya tatu kwenye table yetu.

View attachment 452872

SUM na SMALL
Function ya "Small" inaweza kubebwa ndani ya function ya "Sum"
Angalia kwa makini

View attachment 452864

Ni ndefu sana. Lakini inaweza kuandikwa kwa kufupisha kama namna hii
=SUM(SMALL(E28:M28,({1,2,3,4,5,6,7}))).

View attachment 452871
Utapata kitu kile kile. Ni mambo mengine ya Excel. Kwamba kwa namna flan ({1,2,3,4,5,6,7}) kipande hicho kinachezesha function zote mbili.
Drag chini kupata nyingine zote.

View attachment 452876

Utakua umepata jumla ya points.
Tengeneza table ya refferences za division (Tuiite table D) na utumie utaratibu wa "Vlookup" tulivyojifunza awali, kutengeneza divisions.

View attachment 452868
Kumbuka kwamba jumla ya points ndio inakua kipengele cha kwanza cha function ya vlookup, na range hapo ni ya table yetu mpya table D.

View attachment 452883

Kwa bahati mbaya inaonekana wanafunzi wangu watakua wanalingana sana.

Kuna changamoto kwamba table inapokua na points ndio unaweza kukokotoa jumla ya points (kwa sum&small) na dividions (kwa vlookup), lakini mwishoni unataka uwe na Alama, kama vile A, B nk badala ya points kwenye table yako.

View attachment 452888

Tumia utaratibu wa ku-copy columns za Points na divisions na kuzi-paste-values palepale ili kuondoa formulas ili columns hizo zibaki bila kubadilika. Kisha pale ilipokua 3 na kuifanya kuwa 2 kwenye function ya vlookup kama nilivyoonyesha juu. Badili cell ya kwanza juu kushoto kisha drag kulia na chini kusudi sasa ziwe alama A, B nk.
Wadau naomba kama mna chochote cha kurekebisha, kurahisisha, tusaidiane tutajirishane.
Ahsanteh sana mkuu nimepata kitu ila hapa sijaelewa kitu =SUM(SMALL(E28:M28,({1,2,3,4,5,6,7}))). haya mabano matatu ))) ya mwisho yamezingatia nini kwanini tusingeweka moja? na haya mabano ya hivi {} yana maana katika hii kanuni mkuu? Ahsanteh sana mkuu kama nitafanya ufumbuzi juu ya hili mkuu
 
Ahsanteh sana mkuu nimepata kitu ila hapa sijaelewa kitu =SUM(SMALL(E28:M28,({1,2,3,4,5,6,7}))). haya mabano matatu ))) ya mwisho yamezingatia nini kwanini tusingeweka moja? na haya mabano ya hivi {} yana maana katika hii kanuni mkuu? Ahsanteh sana mkuu kama nitafanya ufumbuzi juu ya hili mkuu

Samahani, kuna mahali nimeona nimeongeza mabano hapo.
Hivi =SUM(SMALL(E28:M28,{1,2,3,4,5,6,7})) ingetosha. Haya mabano ya mwisho yanafunga yote yaliyokua yamefunguliwa mwanzoni.
Nimesikia kuwa kwenye version nyingine za excell, pengine chini ya office 2007 "{ } haikubali, sijajaribu maana sina 2003 na chini yake.
Lakini kwa urahisi kabisa inaweza pia kuandikwa kama hivi. =SMALL(E28:M28,1)+SMALL(E28:M28,2)+SMALL(E28:M28,3)+SMALL(E28:M28,4)+SMALL(E28:M28,5)+SMALL(E28:M28,6)+SMALL(E28:M28,7) inakuja pia

upload_2017-1-2_17-8-55.png


Manake ni namba ndogo kabisa iliyo kati ya E28 na M28, jumlisha namba ya pili kwa udogo katika mstari huo huo wa E28:M28, jumlisha namba ya tatu kwa udogo etc hadi 7
upload_2017-1-2_17-14-36.png

Hii formula nyingine ni ya kufupisha tu lakini kama inazingua afadhali kupitia parefu.
 
Back
Top Bottom