Ex wangu anaondoka... msaada

Meridah Tough

Senior Member
Nov 27, 2017
136
363
Habari zenu?
Kwanza napenda kuwashukuru wale wote wanaojitahidi kutoa ushauri kwa watu wenye matatizo mbalimbali. Kuna muda mtu unahitaji kuongea tu ili upate ushauri ila unapokosa mtu wa kukusikiliza ndipo hupelekea hata kujiua na kufanya mambo ambayo hukuwahi kufikiria kuyafanya.

BACK TO TOPIC

Mimi ni mwanamke mtu mzima mwenye miaka 28. Katika safari yangu ya mahusiano nimewahi kudate na wanaume wawili. Huyo wa kwanza sikuwahi kumpenda na yeye hakuwahi kunipenda. Tatizo lipo kwa huyu mtu wa pili.
yeye tumefahamiana naye miaka kumi sasa ingawa safari ya mapenzi ilidumu kwa miaka mitatu tu mpaka 2017.

Kutokana na mimi kufahamika kwao na yeye kufahamika kwetu, kuna undugu ambao ulianza kujitokeza hata kabla ya sisi kuunganishwa na Mungu. Kushirikiana kwenye mambo ya kijamii, kusaidia na kwenye magonjwa, kushirikiana kwenye sherehe nk. Vitu hivi vilitufanya tuwe karibu sana na ex wangu.

Tulikaa chini tukayaongea na yeye akaweka wazi kuwa katika watu asiowafikiria kuwa nao tena ni mimi hivyo tunaweza kuwa best friend kama kawaida. Na kweli tuilishirikiana sana sana sana kwa muda wa miezi kama mitatu au minne. Yeye akinishirikisha vitu vyake vya ndani hata vinavyomuhusu girlfriend wake nami nikimuhusisha katika baadhi ya mambo.

Ugumu ulianza pale ambapo kila jamaa anapolewa, ananiambia ananipenda anaitaka nk. Na msema kweli mpenzi wa Mungu, mimi nampenda sana huyu kaka ila naenjoy hata kuwa rafiki nae inatosha.
Mara mbili tatu tulifanikiwa kuvunja amri ya sita pasipo kupanga.

Yalipotokea hayo, ex akaniomba kuwa inabidi tuanze kudate lakini tutakua pamoja na yule girlfriend wake yaani tuwe wawili ingawa huyo girlfriend wake hajui uwepo wangu ila ananifahamu kwa kunisikia kua nilikua na huyo jamaa kwa muda tena in serious relationship.

Mara ya kwanza aliponiambia swala la kuwa nae, nilimuomba aniache kwanza nifikirie. Baada ya siku ya pili nilimuambia wazi kuwa mapenzi ya nmana hiyo yasiyo na dira mimi siyawezi. Kama ananitaka kweli achague moja, either tubaki kwenye serious relationship au tuendelee kuwa marafiki tena tunaoheshimiana.
Cha ajabu mwenzangu amekasirika na nikimtumia ujumbe hajibu wala kupokea simu yangu.

Asubuhi ya leo amenipigia na kuniambia hawezi kuwa rafiki nami kwa kua kila anapokua nami anapata hisia za kimapenzi hivyo kujiepusha ni bora tukatengana.

Guys i feel bad kumpoteza mtu ambaye tumesaidiana naye kwenye kila hali na bado anaendelea kunisaidia hata baada ya kuniambia hivyo.

Naombeni mnishauri kwa vyovyote vile jamani.
 
Ulikosea sana kuamua kua best wa ex wako na wakati ulijua kua bado unahisia nae..mtafute muongee kama hayuko tayari kumuacha mwanamke wake nawewe kua na msimamo huohuo kua haiwezekani ninyi kua wapenzi
Msikilize atasemaje ila kikubwa uwe na msimamo tu


Kwa akili zangu ningeacha tu aende kwa kweli furaha yangu haitegemei mtu mwingine
 
Habari zenu?
Kwanza napenda kuwashukuru wale wote wanaojitahidi kutoa ushauri kwa watu wenye matatizo mbalimbali. Kuna muda mtu unahitaji kuongea tu ili upate ushauri ila unapokosa mtu wa kukusikiliza ndipo hupelekea hata kujiua na kufanya mambo ambayo hukuwahi kufikiria kuyafanya.
BACK TO TOPIC
Mimi ni mwanamke mtu mzima mwenye miaka 28. Katika safari yangu ya mahusiano nimewahi kudate na wanaume wawili. Huyo wa kwanza sikuwahi kumpenda na yeye hakuwahi kunipenda. Tatizo lipo kwa huyu mtu wa pili.
yeye tumefahamiana naye miaka kumi sasa ingawa safari ya mapenzi ilidumu kwa miaka mitatu tu mapak 2017. Kutokana na mimi kufahamika kwao na yeye kufahamika kwetu, kuna undugu ambao ulianza kujitokeza hata kabla ya sisi kuunganishwa na Mungu. Kushirikiana kwenye mambo ya kijamii, kusaidia na kwenye magonjwa, kushirikiana kwenye sherehe nk. Vitu hivi vilitufanya tuwe karibu sana na ex wangu.
Tulikaa chini tukayaongea na yeye akaweka wazi kuwa katika watu asiowafikiria kua nao tena ni mimi hivyo tunaweza kuwa best friend kama kawaida. Na kweli tuilishirikiana sana sana sana kwa muda wa miezi kama mitatu au minne. Yeye akinishirikisha vitu vyake vya ndani hata vinavyomuhusu girlfriend wake nami nikimuhusisha katika baadhi ya mambo.
Ugumu ulianza pale ambapo kila jamaa anapolewa, ananiambia ananipenda anaitaka nk. Na msema kweli mpenzi wa Mungu, mimi nampenda sana huyu kaka ila naenjoy hata kuwa rafiki nae inatosha.
Mara mbili tatu tulifanikiwa kuvunja amri ya sita pasipo kupanga. Yalipotokea hayo, ex akaniomba kuwa inabidi tuanze kudate lakini tutakua pamoja na yule girlfriend wake yaani tuwe wawili ingawa huyo girlfriend wake hajui uwepo wangu ila ananifahamu kwa kunisikia kua nilikua na huyo jamaa kwa muda tena in serious relationship.
Mara ya kwanza aliponiambia swala la kuwa nae, nilimuomba aniache kwanza nifikirie. Baada ya siku ya pili nilimuambia wazi kuwa mapenzi ya nmana hiyo yasiyo na dira mimi siyawezi. Kama ananitaka kweli achague moja, either tubaki kwenye serious relationship au tuendelee kuwa marafiki tena tunaoheshimiana.
Cha ajabu mwenzangu amekasirika na nikimtumia ujumbe hajibu wala kupokea simu yangu.
Asubuhi ya leo amenipigia na kuniambia hawezi kuwa rafiki nami kwa kua kila anapokua nami anapata hisia za kimapenzi hivyo kujiepusha ni bora tukatengana.
Guys i feel bad kumpoteza mtu ambaye tumesaidiana naye kwenye kila hali na bado anaendelea kunisaidia hata baada ya kuniambia hivyo.
Naombeni mnishauri kwa vyovyote vile jamani.
Unamwita Ex na wakati bado anakukula we ni mchepuko wake kwa sasa siyo EX tena.
 
Huyo bwana muongo wala hakupendi, umeshindwa kumuacha kwasababu mlifanya kaurafiki mjinga kanuni kuu ya kumsahau mtu ni kuwa mbali nae.Angalia umri wako unapaswa kuwa na maamuzi acha utoto umekua.
 
Uyo inaonekana mnapendana sema hamkuweza kua pamoa kwasababu pamoja na hisia zenu kupatana ila mnatenganishwa na aina au mfumo nje ya hisia zenu.Inawezekana uyo jamaa anaona huna vigezo vya aina ya mwanamke anayemtaka na wewe ulikua naye katika ile dhana ya lets love lead the way bila kujua mapenzi ni sanaa.Nje ya hisia kuwaongoza mlitakiwa kila mmoja ajue namna yakumuwin mwenzake kitu ambacho hakikufanyika.Sasa kwavile toka awali mmeharibu njia yakufanya ni kumwacha aende then if I will be back basi jua uyo ni wako kumpoteza tena utakua uzembe wako plus plus.
 
Kila mtu ana juha lake, wewe ni juha la huyo jamaa na ataendelea kikutumia huku akiendelea maisha na familia yake wakati wewe unahangaika tu.
 
Misaada ndo inakufanya ubaki kwakwe?
Hebu kua na maamuz magumu mwache aende asikuzingue
 
Huyo wa kwanza hamkupendana lkn mlipasuana?!...dunia ina mambo jamani


Kama hutaki kumpoteza si uendelee kumpa papa kwani utapata hasara gani?!
Umeona eeeh, hasara hamna kabisa. Kumnyima mwenzio ulichopewa bure sio vizuri.
 
Ukikubali moyo wako ukuongoze badala ya kukubali kuongozwa na akili. Lazima mwili wako upate taabu.
 
Back
Top Bottom