Ex-wako anapokusifia sana inaashiria nini jamani?

malang0

JF-Expert Member
Apr 7, 2021
440
518
Jumamosi nilipata mgeni binamu yangu kutoka Dodoma, ikabidi nimtoe out kubadilishana mawazo, tukiwa out nikakutana na ex-wangu.

Duu akanishangaa sana, mara ya mwisho kukutana naye miaka miwili, duu kumwona tuu akaanza kunimwagia masifa ooh umenawiri sana mambo yako safi.

Tutafutane aah ikabidi nimpange nitamtafuta, je inaashiria nini?
 
Anakubipu aone kama bado wewe ni boya utarudia makosa Yako ya zamani ambayo ndo huenda yalisababisha mkaachana.

Sasa hapo utachagua kusuka ama kunyoa.
 
Usiwe na wasiwasi nitafute tuu nataka kuuliza huwa unakula nini na unajipaka mafuta gani
 
To be honest, kuna wakati baadhi ya nyuzi huwa napata shaka kama waandishi huwa wapo serious au ndio uwezo wao wa akili umeishia hapo!!!
 
To be honest, kuna wakati baadhi ya nyuzi huwa napata shaka kama wandishi huwa wapo serious au ndio uwezo wao wa akili umeishia hapo!!!
Ndugu.....usishangae siku hizi vijana vinywa na mikono yao umepoteza ushirikiano na ubongo.......matokeo vinatangulia vitendo kabla ya fikra.......na haya ndio madhara yake.......wala hawafanyi makusudi hapo ndio mwisho wa akili zao......
 
Ni vizuri hilo Swali Ungemuuliza x Wako ili upate Jibu la Uhakika.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom