Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Sijui ana professiona gani!
Actually he is for presidential post in TZ, zile issue za akina Lowasa, Karamagi n.k kwenye RICHMOND, angezishughulikia mwenyewe achilia mbali kama asingewapiga shaba wezi wa EPA!
Chadema,
Nafikiri kuna haja ya kumchukua huyu jamaa na kuwa mgombea ubunge wilaya za Mbeya au hata huko Bukoba au kwao (sijui anatoka wapi). Na kama ikiwezekana basi apelekwe shule na kumuandaa kwa mwaka 2015 kuwa mgombea Urais. Maana watu wakorofi kama hawa wanaweza kuishia kuwa akina Idd Amin kama hawatakuwa na shule. Ila kwa kuanzia angelifaa sana kuwa walau Waziri Mkuu.
Nina imani kokote atakapogombea na kushinda ubunge, basi uzembe mdogomdogo utaisha. Huyu jamaa utamlaani weee, ila mwisho wa siku unakuwa unakubali kuwa "walau huyu kaamua kufanya kitu positive". Kawa na uchungu na nchi yake. Wengine si tu kuwa hawana uchungu na nchi yao ila wao "wananyonya damu za Watz hadi matone ya mwisho".
Yes, MNALI FOR PRESIDENT!!!!!!!!!!!!!!