EWURA wamekaa kimya bei ya mafuta ikizidi kupaa, mpango wa bei elekezi umeishia wapi?

Utotole

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,604
4,259
Kwa kuwa mimi si mtaalam wa uchumi nitaanza kwa kuomba radhi pale nitakapoandika mambo yatokayo kwa mtu wa kawaida (lay person). Ni kuhusu bei ya mafuta inayozidi kupaa kila siku. Sasa hivi bei mahali fulani inakaribia kufika shiling 2000 kwa lita moja.

Kipindi fulani hapo awali kulikuwa na hali kama hii na EWURA walikuja juu na kupanga bei elekezi za mafuta na bidhaa zinazotokana na mafuta hayo. na kuna vituo tulishuhudia vikifungwa kutokana na kukaidi agizo la kutumia bei hizo, pamoja na uchakachuaji ulioibuka ili kufidia mapungufu yatokanayo na bei kushushwa.

Hali iliendelea taratibu lakini kidogo kidogo bei ilianza kupanda si ghafla ila kwa viji-shilingi kidogo kidogo (labda ndiyo maana EWURA haikushtuka), mara 1,250/-...1,265/-...1,300/-...1,305/-...1,575/-...1,800/-...etc.

Swali langu ni hili, bei zimekuwa zikipanda sasa kwa muda na zimerudi kule kule ambako EWURA walikuwa wamekataa. Wafuatiliaji wa mambo, na EWURA napenda wanisaidie, wanijuze kama bei za sasa zinaendana na bei kwenye soko la kimataifa au ni yale yale ya mwanzo?

Nahitaji msaada maana naona hatuwasikii tena EWURA wakilizungumzia japo twaendelea kulipia gharama za uendeshaji wao katika kila huduma tunayopata yenye kuhusiana na nishati!!
 
Kwa kuwa mimi si mtaalam wa uchumi nitaanza kwa kuomba radhi pale nitakapoandika mambo yatokayo kwa mtu wa kawaida (lay person). Ni kuhusu bei ya mafuta inayozidi kupaa kila siku. Sasa hivi bei mahali fulani inakaribia kufika shiling 2000 kwa lita moja.

Kipindi fulani hapo awali kulikuwa na hali kama hii na EWURA walikuja juu na kupanga bei elekezi za mafuta na bidhaa zinazotokana na mafuta hayo. na kuna vituo tulishuhudia vikifungwa kutokana na kukaidi agizo la kutumia bei hizo, pamoja na uchakachuaji ulioibuka ili kufidia mapungufu yatokanayo na bei kushushwa.

Hali iliendelea taratibu lakini kidogo kidogo bei ilianza kupanda si ghafla ila kwa viji-shilingi kidogo kidogo (labda ndiyo maana EWURA haikushtuka), mara 1,250/-...1,265/-...1,300/-...1,305/-...1,575/-...1,800/-...etc.

Swali langu ni hili, bei zimekuwa zikipanda sasa kwa muda na zimerudi kule kule ambako EWURA walikuwa wamekataa. Wafuatiliaji wa mambo, na EWURA napenda wanisaidie, wanijuze kama bei za sasa zinaendana na bei kwenye soko la kimataifa au ni yale yale ya mwanzo?

Nahitaji msaada maana naona hatuwasikii tena EWURA wakilizungumzia japo twaendelea kulipia gharama za uendeshaji wao katika kila huduma tunayopata yenye kuhusiana na nishati!!


Asanteni kwa kuleta hii habari. Hawa Jamaa Ndio wanazo zile dosier za mara yakwanza na kwa sababu gani ziliwafanya wakafanikiwa kudhibiti bei wakati ule. yani wasije wakawa ni mafisadi hawa?. Kwani hata biashara inayonyonya damu ni fisadi. huu sio wakati wakuanza kupandishwa bei. hamna vipa wazee. mbona mnatamaa hivo? ebu tuambieni kwanini bei juu? au mnasherehekea ushindi wa ccm and cafu?
 
Majibu marahisi na mafupi ni kuwa wafanya biashara walichangia sana CCM kipindi cha uchaguzi sasa hvi ndiyo muda wa kurudisha fedha zao. Siyo bei ya mafuta tu hata sabuni na bati.

Endelea kufuatilia utagundua vitu vingi vimepanda bei
 
Iyo imetoka, c uchaguzi umekwisha. Ni mpaka mwaka 2013 ndio EWURA wataibuka tena.
 
Kwa kuwa mimi si mtaalam wa uchumi nitaanza kwa kuomba radhi pale nitakapoandika mambo yatokayo kwa mtu wa kawaida (lay person). Ni kuhusu bei ya mafuta inayozidi kupaa kila siku. Sasa hivi bei mahali fulani inakaribia kufika shiling 2000 kwa lita moja.

Kipindi fulani hapo awali kulikuwa na hali kama hii na EWURA walikuja juu na kupanga bei elekezi za mafuta na bidhaa zinazotokana na mafuta hayo. na kuna vituo tulishuhudia vikifungwa kutokana na kukaidi agizo la kutumia bei hizo, pamoja na uchakachuaji ulioibuka ili kufidia mapungufu yatokanayo na bei kushushwa.

Hali iliendelea taratibu lakini kidogo kidogo bei ilianza kupanda si ghafla ila kwa viji-shilingi kidogo kidogo (labda ndiyo maana EWURA haikushtuka), mara 1,250/-...1,265/-...1,300/-...1,305/-...1,575/-...1,800/-...etc.

Swali langu ni hili, bei zimekuwa zikipanda sasa kwa muda na zimerudi kule kule ambako EWURA walikuwa wamekataa. Wafuatiliaji wa mambo, na EWURA napenda wanisaidie, wanijuze kama bei za sasa zinaendana na bei kwenye soko la kimataifa au ni yale yale ya mwanzo?

Nahitaji msaada maana naona hatuwasikii tena EWURA wakilizungumzia japo twaendelea kulipia gharama za uendeshaji wao katika kila huduma tunayopata yenye kuhusiana na nishati!!

Kura zetu zingeondoa kero hizi..... its too late watu wanalipia gharama za kampeni!!! hakuna sababu yoyote ya kupandisha bei ya mafuta kwa sasa zaidi ya kiu ya Kleptomaniacs!!!

:A S angry:
 
Back
Top Bottom