EWURA: Kuna ubambikiziwaji mkubwa wa bili za maji kwenye Mamlaka za Maji Nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968
Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji hapa nchini EWURA imesema imebaini baadhi ya mamlaka za maji kukiuka sheria zinazosimamia mamlaka hizo katika kutoa huduma kwa wananchi ikiwamo kutoza bei ambazo hazijapitishwa na EWURA na ubambikiziwaji wa bili za maji.

Hayo yamebainishwa leo Mei 8,2021 jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Godfrey Chibulunje wakati akizungumza na wanahabari amesema baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wateja waliamua kufanya ukaguzi katika mamlaka 24 kati ya 94 zilizopo.
 

Attachments

  • support@ewura.go.tz_20020209_071643.pdf
    1.4 MB · Views: 7
Hivi shida nin haswaa?mm niliongezewa zaidi ya unit 50 na IRUWASA iringa.
 
Ni wizi mkubwa sana unafanywa na staff wa mamlaka mfano Dawasco.

Majuzi hapa wamenibambikizia bili kutoka shs 6800 hadi shs 120,000 kisa bomba linavuja.
 
Unit 7 elfu 12 si uhuni huo. Hapo maji yanakatika ovyo kwa wiki Mara 2 au 3 yanatoka.
 
Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji hapa nchini EWURA imesema imebaini baadhi ya mamlaka za maji kukiuka sheria zinazosimamia mamlaka hizo katika kutoa huduma kwa wananchi ikiwamo kutoza bei ambazo hazijapitishwa na EWURA na ubambikiziwaji wa bili za maji.

Hayo yamebainishwa leo Mei 8,2021 jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Godfrey Chibulunje wakati akizungumza na wanahabari amesema baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wateja waliamua kufanya ukaguzi katika mamlaka 24 kati ya 94 zilizopo.
Hilo la kubambikiza bill ni moja lipo la kuwalazimisha wateja kununua vifaa vya maji kutoka kwenye hizo Mamlaka kwa bei mara mbili ya zile za maduka ya kawaida wakati manufacturer ni yuleyule na vifaa ni vilevile
 
Jaman Mimi kila Siku Nalia na Muwasa, Mamlaka ya Maji Safi Musoma Ni ya kumulikwa kwa Tochi Kali Sana, Yaan Bili haziendani na Uhalisia kabisa.. Huduma za Maji Ni mbovu, Mkoa Ni mdogo lakini zoezi la usambazaji Maji limekaa kihunihuni na Ziwa lipo jirani, Huyu Mkurugenzi wa Idara ya Hapa Ni wa kutumbua kabisa!!
 
Haya mambo yapo. Nimewahi kuletewa bill ya TSh. 68,000/= kwa mwezi wakati average ya bill kwa mwezi ni 15,000/=. Kuna tatizo mahali. Mamlaka inayonihudumia ni S*****sa
 
Hilo bomba linavuja kabla au baada ya mita?
Linavuja baada ya meter.

But hipo hivi, lilikuwa linavuja kitambo na bill haikuwahi kuja hata 40kl sababu nina tank kubwa huwa najaza kwa mwezi mara moja.

So kuna wakati sikuwepo home kwa miezi miwili ndiposa nilipoletewa bill hiyo but hapo nyuma mbona hawakuwahi kuleta matumizi ya 68units?
 
Hii issue juzi nimemsikia mbunge mmoja akilalamikia hii issue na akawa anapendekeza watumie mfumo wa Luku kwenye mita za maji.
 
Tena DAWASA ndio majambazi kabisa, sijui kwa nini EWURA kwenye huu uchunguzi wao wamewaweka kando.
 
Mwezi 1 bili zinakuja Mara 2...
Tena zote units ambazo wala hujawahi kuzitumia.
 
Back
Top Bottom