Everton vs Saigon 1967

Saigon ya sasa sio ile ya akina Kitwana Kondo . Iddi Simba na wageni kama akina Ndolanga, Rage na wengineo ninaowasikia.
Saigon choka mbovu ya kina Ditopile ndio ipange rais atakua nani?labda rais wa kucheza rede
 
Muuza Viatu,
Mkutano Maalum wa NEC uliitishwa kuchagua mgombea urais kwa tiketi ya CCM na Jakaya Mrisho Kikwete akashinda akifuatiwa na Benjamin William Mkapa, Cleopa Msuya akiwa wa mwisho.

Kwa kuwa Kikwete hakuweza kupata ‘’absolute majority,’’ ikabidi uchaguzi urudiwe.

Ukumbi ulikuwa umegubigwa na ‘’tension,’’ nzito wajumbe wa CCM walipokuwa wanapiga kura kuchagua kati ya Kikwete na Mkapa.

Jiulize msomaji wangu hii ‘’tension,’’ wasiwasi ulisababishwa na nini ilhali wagombea wote ni wa chama kimoja?

Iweje wajumbe wapate shinikizo la damu ghafla?
Walikuwa wanatishwa na jinamizi lipi?

Kuna tofauti gani katika ya hawa wagombea wawili wa chama kimoja?

Mpashaji wangu alinifahamisha kuwa baadhi ya wajumbe walikuwa wakinong’onezana ndani ya ukumbi wakati wa kupiga kura.

Alipofika hapa nikamsimamisha mpashaji wangu nikamuuliza, ‘’Wewe ulitegemea Kikwete ashinde dhidi ya Mkapa?’’

Mpashaji wangu alicheka akasema, ‘’Alipoingia Mkapa katika kinyang'anyiro kile nilijua yeye atakuwa rais wala sikuwa na wasiwasi kwa kuwa naijua nguvu iliyokuwa nyuma yake kwanza na pili nazijua siasa za Tanzania. Mimi nilikuwa natazama ile senema na kuangalia itaishia wapi hasa pale Kikwete alipoingia dakika za mwisho baada ya Prof. Malima. Nilijua sasa kocha anamwingiza mfungaji magoli timu ichukue kikombe.’’

Nikamuuliza mpashaji wangu, ‘’Huyu kocha nanI?’’

''Tulizana tumia ubongo wako utamjua,'' Mpashaji alinijibu.
Duru ya pili Kikwete akabwagwa na hivi ndivyo Mkapa alivyokuja kuwa Rais.

Katika ukumbi ule ule wa Chimwaga katika 1992 hali inayofanana na hii ya 1995 katika ya Kikwete na Mkapa, Prof Malima alibwagwa alipokuwa anagombea kuingia NEC iliyokuwa na viti 20.

Prof. Malima hakuanguka hivi hivi tu mpango makhsusi ulikuwa umepangwa ndani ya CCM dhidi yake na alipoangushwa wabaya wake walikesha wakisheherekea ushindi wao.

Kikwete kama Prof. Malima halikadhalika hakuanguka hivi hivi.

Kama walivyosheherekea kuangushwa kwa Malima miaka mitatu iliyopita halikadhalika ulifanyika mkesha Dodoma kwa kuanguka kwa Kikwete.

Msomaji wangu huoni kuna ‘’variable,’’ zinazofanana katika yale yaliyotokea kwa Prof. Malima 1992 na haya yaliyomfika Kikwete 1995?

Swali la kujiuliza nani anavuruga hizi kete kwenye dama?

Mwalimu Gurumo wa Msondo Ngoma, Juwata Jazz alikuwa akisema,’’Msondo ngoma akili kichwani mwako.’’
Alisikika mchanja gomba kwa fasi akijifariji huku akila miraa.
 
Wa...
Ndugu yangu nachokiona kwako ni tatizo la uungwana na labda niongeze kuwa hunifahamu mimi wala wazee wangu.

Babu yako unasema hakuwa mla kashata.
Sawa.

Unasema hakuwa mkaa barazani kuanzia alfajir hadi maghrib.

Sawa.

Lakini nimekueleza babu yangu alikuwa nani.

Babu yangu Salum Abdallah alikuwa mwanachama wa AA, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, TAA na pia muasisi wa TANU.

Babu yangu alikuwa muasisi wa TRAU kiongozi wa watu na mfadhili wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nyumbani kwake kulikuwa na barza kubwa sana ya wana TANU na kahawa na kashata ikinyweka sana hapo.

Nimekufahamisha pia kuwa babu yangu juu ya kuwa mpigania uhuru alikuwa mfanyabiashara na mkulima.

Kipi kinachokushinda wewe kumweleza babu yako?

Umemtaja Dossa Aziz.

Babu yangu alikuwa na nyumba yake Mtaa wa Congo na Mbaruku katika miaja ya 1930 jirani na nyumba ya Aziz Ali baba yake Dossa.

Dossa na baba yangu wamecheza pamoja udogoni.

Unapomkejeli Dossa umemkejeli baba yangu.

Hapa kwenye huu mjadala baina yangu na wewe haya maneno ya "makafiri," ya kutukana imani na dini za watu yanaingia vipi?

Mimi sikuenda Library of Congress "kupiga picha," nilikuwa hapo na Capitol Hill katika utafiti na katika miaka yangu ya uanafunzi nilikuwa member wa maktaba hiyo.

Ndugu yangu si ungefanya hata juhudi kidogo unijue ujiondolee fedheha ya kuropoka?

Hii picha hapo chini niko Northwestern University, Evanston Chicago, Illinois nilialikwa kufanya mhadhara.

View attachment 1875046

View attachment 1875049
Capitol Hill Washington DC
Kwa hio tukusaidiaje ndg?
 
Nimekuelewa Mo,Said
Muuza Viatu,
Nilijua wasomaji wangu hawatashindwa kukitegua kitendawili hiki.

Lakini yako mengi yaliyopitika ukipenda unaweza kuita, "usaliti," la unaona hilo neno zito sana unaweza kujiridhisha kwa kusema ule ulikuwa mchezo wa siàsa.

Ilikuwaje "vijana wa mtandao," wakapoteza mechi katika kupiga zile penalti tano tano?"

Hivi karibuni Kikwete alisikika akisema kuwa iko siku ataeleza kwa nini aligombea urais.

Ningekuwa sikijui kisa ningeshangazwa na kauli hii.

Ningejiuliza kwani vipi kipi kinamfanya leo atake kumtoa paka ndani ya kapu?

Jambo si lishapita na watu tumesahau?

Ila namsifu Kikwete na Mtandao kwa kitu kimoja kuwa mwisho wa siku walichukua kikombe.

Salim Ahmed Salim alijaribu lakini aliposhindwa hakurejea tena ulingoni.

Kuna gazeti lilisema kuwa alishiriki katika kumuua Karume na pia siku nyingi ilikwishasemwa kuwa ni Muarabu.

Mara ya kwanza kukutana na Salim nyumbani kwake nilimuuliza kuhusu kuandika kumbukumbu zake.

Napitia kumbukumbu za Mzee Mwinyi labda nitaliona hili la Salim.

Halipo.

Katika kitabu chake Mzee Mwinyi kampamba sana Baba wa Taifa.

Sasa hapa nikajiuliza kwa nini kafanya vile?

Mzee Mwinyi alikuwa na tui mkononi asipolienga linaweza likakatika na yeye anazijua sheria za mchezo.

Kikwete katika hotuba yake ya kwanza Kibaha anagombea urais alilipamba Kanisa Katoliki kwa kusema kama si wao kumpa elimu angekuwa anakimbiza mabasi Chalinze huku ana kikapu cha karanga kichwani anawauzia abiria kwenye mabasi.

Kikwete na yeye pia alikuwa na tui mkononi.

Hizi ndizo sheria za mchezo huu.
Hautaki ujifanye mjuaji sana.

Ujue wapi kwa kuponda na wapi na wapi kwa kusifia.

Kikwete alikuwa na Prof. Malima katika kundi la wagombea wa CCM.

Kulikuwa na kichekesho au unaweza kuita, "tragic comedy," kilichoanzishwa na gazeti moja lililoandika kuwa, "Waislam Waiogopa Ikulu."

Sababu ya maneno haya ni kuwa hadi wakati ule hapakuwa na Muislam yeyote aliyejitokeza kuomba nafasi ya Urais.

Wahariri hao hao wakaja na lingine jipya ikasemwa kuwa wananchi Waislam wamekamia kuchagua rais Muislam.

Bunge likawaka moto.
Huko ni kuchanganya dini na siasa.

Mwiko mkubwa.

Ikabidi Waislam ndani ya Bunge kwa Spika waorodheshe majina yao kukataa kuwa wao wana nia ya kugombea urais.

Kikwete jina lake lilikuweko kwenye orodha ile.

Karatasi ilipofika kwa Prof. Malima msomi wa Princeton University, New Jersey yeye alikataa hata kuigusa ile karatasi.

Mzee Mwinyi kamtaja Prof. Malima katika hili sakata la uchaguzi wa mwaka 1995.

Lakini kwa ajili ya utu uzima mengi muhimu nadhani kasahau kuhusu Prof. Malima hivyo hakuyaandika.

Kasahau na haya ninayoeleza hapa hayamo katika kumbukumbu zake.

Laiti angeyakumbuka kitabu chake kingenoga sana.

Screenshot_20210802-072057_Facebook.jpg


Screenshot_20210802-072902_Photos.jpg


Screenshot_20210802-075118_Photos.jpg
 
Muuza Viatu,
Nilijua wasomaji wangu hawatashindwa kukitegua kitendawili hiki.

Lakini yako mengi yaliyopitika ukipenda unaweza kuita, "usaliti," la unaona hilo neno zito sana unaweza kujiridhisha kwa kusema ule ulikuwa mchezo wa siàsa.

Ilikuwaje "vijana wa mtandao," wakapoteza mechi katika kupiga zile penalti tano tano?"

Hivi karibuni Kikwete alisikika akisema kuwa iko siku ataeleza kwa nini aligombea urais.

Ningekuwa sikijui kisa ningeshangazwa na kauli hii.

Ningejiuliza kwani vipi kipi kinamfanya leo atake kumtoa paka ndani ya kapu?

Jambo si lishapita na watu tumesahau?

Ila namsifu Kikwete na Mtandao kwa kitu kimoja kuwa mwisho wa siku walichukua kikombe.

Salim Ahmed Salim alijaribu lakini aliposhindwa hakurejea tena ulingoni.

Napitia kumbukumbu za Mzee Mwinyi labda nitaliona hili la Salim.

Halipo.

Katika kitabu chake Mzee Mwinyi kampamba sana Baba wa Taifa.

Sasa hapa nikajiuliza kwa nini kafanya vile?

Mzee Mwinyi alikuwa na tui mkononi asipolienga linaweza likakatika na yeye anazijua sheria za mchezo.

Kikwete katika hotuba yake ya kwanza Kibaha anagombea urais alilipamba Kanisa Katoliki kwa kusema kama si wao angekuwa anakimbiza mabasi Chalinze huku ana kikapu cha karanga anawauzia abiria kwenye mabasi.

Kikwete na yeye pia alikuwa na tui mkononi.

Hizi ndizo sheria za mchezo huu.
Hautaki kujua sana.

Ujue wapi kwa kuponda wapi kwa kusifia.

Kikwete alikuwa na Prof. Malima katika kundi la wagombea wa CCM.

Kulikuwa na kichekesho kilichoanzishwa na gazeti moja lililoandika kuwa Waislam waiogopa Ikulu.

Sababu ya maneno haya ni kuwa hadi wakati ule hapakuwa na Muislam yeyote aliyejitokeza kuomba nafasi hiyo.

Wahariri hao hao wakaja na lingine jipya ikasemwa kuwa wananchi Waislam wamekamia kuchagua rais Muislam.

Bunge likawaka moto.

Ikabidi Waislam ndani ya Bunge waorodheshe majina yao kukataa kuwa wao wana nia ya kugombea urais.

Kikwete jina lake lilikuweko kwenye orodha ile.

Karatasi ilipofika kwa Prof. Malima msomi wa Princeton University, New Jersey yeye alikataa hata kuigusa ile karatasi.

Mzee Mwinyi kamtaja Prof. Malima katika hili sakata la uchaguzi wa mwaka 1995.

Lakini kwa ajili ya utu uzima mengi muhimu nadhani kasahau kuhusu Prof. Malima hivyo hakuyaandika.

Kasahau na haya ninayoeleza hapa.

Laiti angeyakumbuka kitabu chake kingenoga sana.

View attachment 1877064
Kwa kifupi unasema Mwalimu Nyerere (Marehemu) alikuwa ni "mdini".
 
Muuza Viatu,
Nilijua wasomaji wangu hawatashindwa kukitegua kitendawili hiki.

Lakini yako mengi yaliyopitika ukipenda unaweza kuita, "usaliti," la unaona hilo neno zito sana unaweza kujiridhisha kwa kusema ule ulikuwa mchezo wa siàsa.

Ilikuwaje "vijana wa mtandao," wakapoteza mechi katika kupiga zile penalti tano tano?"

Hivi karibuni Kikwete alisikika akisema kuwa iko siku ataeleza kwa nini aligombea urais.

Ningekuwa sikijui kisa ningeshangazwa na kauli hii.

Ningejiuliza kwani vipi kipi kinamfanya leo atake kumtoa paka ndani ya kapu?

Jambo si lishapita na watu tumesahau?

Ila namsifu Kikwete na Mtandao kwa kitu kimoja kuwa mwisho wa siku walichukua kikombe.

Salim Ahmed Salim alijaribu lakini aliposhindwa hakurejea tena ulingoni.

Kuna gazeti lilisema kuwa alishiriki katika kumuua Karume na pia siku nyingi ilikwishasemwa kuwa ni Muarabu.

Mara ya kwanza kukutana na Salim nyumbani kwake nilimuuliza kuhusu kuandika kumbukumbu zake.

Napitia kumbukumbu za Mzee Mwinyi labda nitaliona hili la Salim.

Halipo.

Katika kitabu chake Mzee Mwinyi kampamba sana Baba wa Taifa.

Sasa hapa nikajiuliza kwa nini kafanya vile?

Mzee Mwinyi alikuwa na tui mkononi asipolienga linaweza likakatika na yeye anazijua sheria za mchezo.

Kikwete katika hotuba yake ya kwanza Kibaha anagombea urais alilipamba Kanisa Katoliki kwa kusema kama si wao kumpa elimu angekuwa anakimbiza mabasi Chalinze huku ana kikapu cha karanga kichwani anawauzia abiria kwenye mabasi.

Kikwete na yeye pia alikuwa na tui mkononi.

Hizi ndizo sheria za mchezo huu.
Hautaki ujifanye mjuaji sana.

Ujue wapi kwa kuponda wapi na kwa kusifia.

Kikwete alikuwa na Prof. Malima katika kundi la wagombea wa CCM.

Kulikuwa na kichekesho au unaweza kuita, "tragic comedy," kilichoanzishwa na gazeti moja lililoandika kuwa, "Waislam Waiogopa Ikulu."

Sababu ya maneno haya ni kuwa hadi wakati ule hapakuwa na Muislam yeyote aliyejitokeza kuomba nafasi ya Urais.

Wahariri hao hao wakaja na lingine jipya ikasemwa kuwa wananchi Waislam wamekamia kuchagua rais Muislam.

Bunge likawaka moto.
Huko ni kuchanganya dini na siasa.

Mwiko mkubwa.

Ikabidi Waislam ndani ya Bunge kwa Spika waorodheshe majina yao kukataa kuwa wao wana nia ya kugombea urais.

Kikwete jina lake lilikuweko kwenye orodha ile.

Karatasi ilipofika kwa Prof. Malima msomi wa Princeton University, New Jersey yeye alikataa hata kuigusa ile karatasi.

Mzee Mwinyi kamtaja Prof. Malima katika hili sakata la uchaguzi wa mwaka 1995.

Lakini kwa ajili ya utu uzima mengi muhimu nadhani kasahau kuhusu Prof. Malima hivyo hakuyaandika.

Kasahau na haya ninayoeleza hapa hayamo katika kumbukumbu zake.

Laiti angeyakumbuka kitabu chake kingenoga sana.

View attachment 1877064

View attachment 1877065

View attachment 1877066
Naamin Kikwete kwenye harakat zake za kisiasa ni mtu wa mbinu sana naamin ana mengi ya kustaajabisha na kushangaza endapo km ataamua kuelezea ushirik wa wanamtandao ktk matukio ya uchaguz wa 95,2005 na 2015 chaguzi zote hizo naamin zilimhusisha km mmoja wa wahusika wakuu.
 
Kobello,
Umekuja na jambo muhimu sana kufahamika.

Nakushauri ufungue uzi mpya.
Sijafanya utafiti kuhusu "Udini" wa Mwalimu Nyerere, kwa hiyo kuanzisha uzi wa suala hilo itakuwa siyo sahihi.
Ila tu, nilikuwa nataka nijue, kutokana na maandishi yako kuhusu primaries za CCM na jinsi Kighoma Ali Malima (Marehemu) na Kikwete walivyowahi kushindwa.
Kwa utafiti wako wa masuala haya, unastuambia kimaandishi mwalimu Nyerere alikuwa ni "Mdini"? yaani alibagua viongozi wa nchi hii kwa kutumia "dini" kama kigezo cha kuwa kiongozi wa ngazi fulani?
Au labda nifafanue zaidi swali langu, je Mwalimu Nyerere aliwapendelea zaidi wakristu na kuwaone waislamu?
Nataka nijue tu maoni yako kiufupi sana.
 
Sijafanya utafiti kuhusu "Udini" wa Mwalimu Nyerere, kwa hiyo kuanzisha uzi wa suala hilo itakuwa siyo sahihi.
Ila tu, nilikuwa nataka nijue, kutokana na maandishi yako kuhusu primaries za CCM na jinsi Kighoma Ali Malima (Marehemu) na Kikwete walivyowahi kushindwa.
Kwa utafiti wako wa masuala haya, unastuambia kimaandishi mwalimu Nyerere alikuwa ni "Mdini"? yaani alibagua viongozi wa nchi hii kwa kutumia "dini" kama kigezo cha kuwa kiongozi wa ngazi fulani?
Au labda nifafanue zaidi swali langu, je Mwalimu Nyerere aliwapendelea zaidi wakristu na kuwaone waislamu?
Nataka nijue tu maoni yako kiufupi sana.
Kobello,
Hivi unavyoandika inatosha kufungulia uzi.

Fungua uzi mpya.
Hii ni historia muhimu ya Julius Nyerere.
 
Naamin Kikwete kwenye harakat zake za kisiasa ni mtu wa mbinu sana naamin ana mengi ya kustaajabisha na kushangaza endapo km ataamua kuelezea ushirik wa wanamtandao ktk matukio ya uchaguz wa 95,2005 na 2015 chaguzi zote hizo naamin zilimhusisha km mmoja wa wahusika wakuu.
Muuza Viatu,
Mimi nasubiri kumbukumbu za Kikwete kwa hamu kubwa sana.

Anayo mengi sana.
 
Ndugu zangu,
Nimepitia hapo chini leo fajr ingawa mimi ndiye mwandishi nimeshangazwa kidogo na mjadala tuliofanya.

Ukiwa na fursa hebu nawe chungulia:

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom