Everton vs Saigon 1967

Wa...
Mimi elimu ya mwanzo aliyonifunza mama yangu ni adabu yaani kuheshimu watu.

Nilipokuwa sasa nasoma nilifunzwa ilm ya mjadala katika madras na somo hili lina kipengele cha "Adabu ya Elimu."

Mwalimu wangu alikuwa Sheikh Haruna.
Alikuwa akinambia, "Mohamed ukitukana watu umenitukana mimi mwalimu wako na umemtukana mama yako."

Siku moja nikamuuliza, "Sheikh naelewa kukutukanisha wewe mwalimu wangu, mama yangu anaingia vipi hapa?"

Jibu lake lilinishtua sana.

"Mtoto aliyezaliwa na wazazi wenye staha na yeye atakuwa kavaa vazi la staha la wazazi wake."

Na atakua amevaa hilo vazi huku akinywa alikasusu.
 
Wa...
Ndugu yangu nachokiona kwako ni tatizo la uungwana na labda niongeze kuwa hunifahamu mimi wala wazee wangu.

Babu yako unasema hakuwa mla kashata.
Sawa.

Unasema hakuwa mkaa barazani kuanzia alfajir hadi maghrib.

Sawa.

Lakini nimekueleza babu yangu alikuwa nani.

Babu yangu Salum Abdallah alikuwa mwanachama wa AA, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, TAA na pia muasisi wa TANU.

Babu yangu alikuwa muasisi wa TRAU kiongozi wa watu na mfadhili wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nyumbani kwake kulikuwa na barza kubwa sana ya wana TANU na kahawa na kashata ikinyweka sana hapo.

Nimekufahamisha pia kuwa babu yangu juu ya kuwa mpigania uhuru alikuwa mfanyabiashara na mkulima.

Kipi kinachokushinda wewe kumweleza babu yako?

Umemtaja Dossa Aziz.

Babu yangu alikuwa na nyumba yake Mtaa wa Congo na Mbaruku katika miaja ya 1930 jirani na nyumba ya Aziz Ali baba yake Dossa.

Dossa na baba yangu wamecheza pamoja udogoni.

Unapomkejeli Dossa umemkejeli baba yangu.

Hapa kwenye huu mjadala baina yangu na wewe haya maneno ya "makafiri," ya kutukana imani na dini za watu yanaingia vipi?

Mimi sikuenda Library of Congress "kupiga picha," nilikuwa hapo na Capitol Hill katika utafiti na katika miaka yangu ya uanafunzi nilikuwa member wa maktaba hiyo.

Ndugu yangu si ungefanya hata juhudi kidogo unijue ujiondolee fedheha ya kuropoka?

Hii picha hapo chini niko Northwestern University, Evanston Chicago, Illinois nilialikwa kufanya mhadhara.

View attachment 1875046

View attachment 1875049
Capitol Hill Washington DC

No wonder kipindi kile wale jamaa wa pale airport ilibidi wakutengee choo chako ili waangalie kama umebeba ngada.
 
Ndugu zanguni note mnaofuatilia huu mjadala kama London alivyoshauri ni kweli hapana tija ya mimi kumjibu huyu ndugu yetu.

In Shaa Allah nitakuleteeni mkasa wa uchaguzi wa 1995 Dodoma kupata jina la mgombea wa CCM.
Itakua vzr mno Muft
 
Itakua vzr mno Muft
Muuza...
Mimi si Muft wala si Ustaadh.

Nimerudia mara kadhaa hapa kutahadharisha kuhusu hili.

Hizo ni fani za wengine mimi sikujaaliwa na kwa kuwa ni vyeo katika Uislam si vitu vya kufanyiwa maskhara kwa kunitumia mimi.

Haipendezi.

Ikiwa unapendezewa kunivika joho basi nifunge kilemba kwa sifa nilizonazo si kwa elimu ambayo sina.

Mimi ni huyo hapo chini:

PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002
The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York
Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam
Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam
In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London)
Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London)
Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam)

The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003)

Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003)

Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004)

Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004)

Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006)

Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi

Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg

Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi

Awards: Several Awards

Visiting Scholar: (2011)
University of Iowa, Iowa City, USA
Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin, Germany.

OTHER COUNTRIES VISITED
Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi
 
Muuza...
Mimi si Muft wala si Ustaadh.
NImerudia mara kadhaa hapa kutahadharisha kuhusu hili.

Hizo ni fani za wengine mimi sikujaaliwa na kwa kuwa ni vyeo katika Uislam si vitu va kufanyiwa maskhara kwa kunitumia mimi.

Haipendezi.

Ikiwa unapendezewa kunivika joho basi nifunge kilemba kwa sifa nilizonazo si kwa elimu ambayo sina.

Mimi ni huyo hapo chini:

PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002
The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York
Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam
Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam
Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam
The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam
Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam
In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London)
Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London)
Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam)

The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003)

Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003)

Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004)

Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004)

Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006)

Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi

Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg

Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi

Awards: Several Awards

Visiting Scholar: (2011)
University of Iowa, Iowa City, USA
Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.

OTHER COUNTRIES VISITED
Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi
Sawa Ndugu Mwandishi
 
Sawa Ndugu Mwandishi
Muuza Viatu,
Kwa kuwa hukupata kuniona nilivyokuwa kijana ili kukuonyesha haiba yangu nakuwekea hiyo picha.

Naamini itasaidia kufahamiana na tutaondokana na haya mambo ya Ustadhi na Muft:

1627756201769.png

London 1991
 
EVERTON VS SAIGON 1967

Rafiki yangu Mohamed Abdulrahman kutoka Ujerumani leo asubuhi kaniandikia kitu kilichonirudisha nyuma sana udogoni.

Soma stori:

"Baada ya kuundwa Saigon Everton ilibaki na tulicheza mechi mbili.

Ya kwanza nilicheza inside right pembeni yangu alikuwa Mkwanda Ingemar Johansson.

Kitu cha ajabu kilitokea.

Mwanzo wa game tu tunaanza nimepokea pasi nikamgongea Mkwanda na yeye akapiga shuti golini kutoka centre na akafunga goli.

Mnazi Mmoja hapo mbele ya Kibarua Bar.

Mechi hii nilikatika jino la chini mbele.

Alama ninayo hadi leo.

Lile goli liliwakasirisha sana Saigon.

Jumanne Masimenti ambae alikuwa akicheza Centre Half Saigon akawa ana overlap kuja mbele kusaidia mashambulizi.

Na hii ilikuwa style ya Everton tulipokuwa hatujagawanyika na lazima goli litapatikana.

Sisi kumuona Jumanne anakuja mbele ikabidi tujazane nyuma kulinda goli.

Hapo ndipo nilipovunjika jino.

Masimenti "Guu la Ngamia," marehemu Harudiki Kabunju akipenda kumwita hivyo, akakutana na loose ball ndani ya box akapiga shuti kali golini.

Nikaweka kichwa nimesimama katikati ya "goal line."

Taya ya juu na ya chini zikaumana jino likakatika.

Jumanne alikuwa na tambo kapanda juu vizuri sana kamchukua baba yake.

Lakini juu ya mwili huu Jumanne alikuwa mpole sana na wababe wakimuogopa hawathubutu kumchokoza.

Ukigongana na Jumanne hewani wewe utaanguka chini yeye atatua na miguu yake miwili kisha akupe lile kono lake kubwa kukunyanyua.

Jumanne alikuwa na mdogo wake Twaha mguu wake wa kushoto mfupi kidogo hivyo akichechemea lakini alikuwa left winger hatari kwa mashuti na mbio.

Akicheza Young Kenya club kali katika club za mitaani.

Wenzake katika timu hii walikuwa Kirk Douglas (Kitwana Douglas), Kesi Kibuda, King Kodo, Denis Law (Jamil Hizam) kwa kuwataja wachache.

Hupita Mnazi Mmoja na wanangu nikawaambia udogoni tumecheza sana mpira kwenye viwanja hivi.

Jumanne alipokwenda Cosmopolitan Coach Mansur Magram ndiyo akambadilisha position na kumchezesha Centre Forward.

Mechi ya pili sikucheza.

Nimerudi shule St. Joseph's Convent School haraka nikafika nyumbani kubadili nguo nawahi kutazama mechi hapo Mnazi Mmoja.

Tukiishi Libya Street jumba la Posta karibu na Mnazi Mmoja.

Nimekuta vurugu kumetokea ugomvi Mkwanda kampiga kichwa Mrisho Wanted kampasua.

Mrisho kuniona mimi naingia kanifata damu zinamvuja usoni.

Mimi maisha yangu yote sikuwa mtu wa ubabe na hata hao wababe wakimuogopa Mrisho sembuse mie kitoto kidogo.

Basi akafika hadi mbele yangu nami "I cooly held my ground."

Nadhani kwa ile heshima niliyokuwanayo na kule kutulia kwangu nikimwangalia aliona aibu hakunigusa.

Wanted siku ile alikuwa ameadhirika kupigwa na Mkwanda mtoto mdogo juu ya ubabe wake wote.

Akamfuata Mkwanda nyumbani kwao.

Mkwanda akatoka ndani kwao kumkabili barabarani.

Mrisho akampiga Mkwanda ngumi ya tumbo.

Mkwanda hakumrudishia alirudi nyuma kashika tumbo lake.

Ugomvi ukaisha Mrisho akaondoka.

Mrisho akajakuwa mtu aliyekuwa na mapenzi makubwa sana na mimi kila akiniona atanipigia kelele, "Eusobio njoo nipe hela niingie kwa Gersan."

Pale Mchikichi na Sikukuu Amani Gersan alifungua mgahawa wake akiuza pilau mchana.

Gersan mwenyewe mbabe unaogopa hata kumwambia kachumbari haikukolea ndimu.

Hii ilikuwa hoteli ya wababe.

Mandava ndiyo wanakutana hapo mchana kula.

Mimi nikiingizwa hapo na Ali Ugaga (Uri Gagarin) mbabe mwenzao tukitokea bandarini.

Siku nyingine tunakwenda kula kwa Matataiwa kisha tukahamia Msimbazi na Kiungani kwa Amiri Ali Mchawi.

Hoteli zote hizi walikuwa na wapishi hodari sana.

Matataiwa akipika hadi mseto na papa.

Allah awarehemu ndugu zetu wote waliotangulia mbele ya haki.

Utoto una raha zake."

PICHA: Kulia ni Mwandishi na Victor John.

View attachment 1870155
Heshima kwako mkuu, hakika simulizi na uandishi wako hauna mfano, kwa sisi Wakristu tunasema Mungu akubariki sana na akupe maisha marefu ,huu uandishi wako ni mtamu sana, ni kama nasoma vitabu vya Shaaban Robert. Pia leo ndio najua Masimenti kuwa alikuwa anacheza beki kabla ya kwenda Cosmopolitan ya Mansour Magram, mzee wa kukalia mpira! Mungu awarehemu hawa miamba.
 
Nataka kujiunga na klabu yenu, nasikia nyie ndio mnapanga Nani awe Rais wa nchi
Saigon ya sasa sio ile ya akina Kitwana Kondo . Iddi Simba na wageni kama akina Ndolanga, Rage na wengineo ninaowasikia.
 
Heshima kwako mkuu, hakika simulizi na uandishi wako hauna mfano, kwa sisi Wakristu tunasema Mungu akubariki sana na akupe maisha marefu ,huu uandishi wako ni mtamu sana, ni kama nasoma vitabu vya Shaaban Robert. Pia leo ndio najua Masimenti kuwa alikuwa anacheza beki kabla ya kwenda Cosmopolitan ya Mansour Magram, mzee wa kukalia mpira! Mungu awarehemu hawa miamba.
Mfia...
Amin kwa sote ndugu yangu.

Jumanne tumekuwa pamoja udogoni na kipaji chake cha kucheza mpira kilijitokeza toka utotoni.

Kwa kweli tukimtegemea sana katika kupata ushindi.

Kuna kocha Mjerumani alikuja kufundisha Tanzania alimpa jina la utani Jumanne akamwita, "Tarzan," kwa ajili ya lile umbo lake.
 
Mfia...
Amin kwa sote ndugu yangu.

Jumanne tumekuwa pamoja udogoni na kipaji chake cha kucheza mpira kilijitokeza toka utotoni.

Kwa kweli tukimtegemea sana katika kupata ushindi.

Kuna kocha Mjerumani alikuja kufundisha Tanzania alimpa jina la utani Jumanne akamwita, "Tarzan," kwa ajili ya lile umbo lake.
Asante kwa hakika unatupa historia iliyotukuka, hicho kizazi cha akina Jumanne ndio kilikuwa cha mpira hasa, walicheza mpira kwa mapenzi na sio kama ilivyo sasa ambapo mpira imekuwa ni ajira , wachezaji wetu wa sasa hawawafikii hata robo wachezaji wa zamani kwa uchezaji wao, sidhani kama kuna wachezaji wa aina ya akina Mohamed Bakari Tall, Mohamed Kajole , Sunday manara na kaka yake pamoja na mdogo wao, Khalid Abeid, Mambosasa.Ahamed Amasha. Boy Wickens, Adamu Sabu na wengineo wengio ambao ndio wamemalizia kizazi cha mpira uliotukuka.
 
Usisahau kuhusu tukio LA mwaka 1995 aliyepindua meza ndani ya chimwaga na kumuwezesha mwela wa lupaso kuongoza nchi uliahidi utalihadithia
Muuza Viatu,
Mkutano Maalum wa NEC uliitishwa kuchagua mgombea urais kwa tiketi ya CCM na Jakaya Mrisho Kikwete akashinda akifuatiwa na Benjamin William Mkapa, Cleopa Msuya akiwa wa mwisho.

Kwa kuwa Kikwete hakuweza kupata ‘’absolute majority,’’ ikabidi uchaguzi urudiwe.

Ukumbi ulikuwa umegubikwa na ‘’tension,’’ nzito wajumbe wa CCM walipokuwa wanapiga kura kuchagua kati ya Kikwete na Mkapa.

Jiulize msomaji wangu hii ‘’tension,’’ wasiwasi ulisababishwa na nini ilhali wagombea wote ni wa chama kimoja?

Iweje wajumbe wapate shinikizo la damu ghafla?

Walikuwa wanatishwa na jinamizi lipi?

Kuna tofauti gani katika ya hawa wagombea wawili wa chama kimoja?

Mpashaji wangu alinifahamisha kuwa baadhi ya wajumbe walikuwa wakinong’onezana ndani ya ukumbi wakati wa kupiga kura.

Alipofika hapa nikamsimamisha mpashaji wangu nikamuuliza, ‘’Wewe ulitegemea Kikwete ashinde dhidi ya Mkapa?’’

Mpashaji wangu alicheka akasema, ‘’Alipoingia Mkapa katika kinyang'anyiro kile nilijua yeye atakuwa rais wala sikuwa na wasiwasi kwa kuwa naijua nguvu iliyokuwa nyuma yake kwanza na pili nazijua siasa za Tanzania. Mimi nilikuwa natazama ile senema na kuangalia itaishia wapi hasa pale Kikwete alipoingia dakika za mwisho baada ya Prof. Malima. Nilijua sasa kocha anamwingiza mfungaji magoli timu ichukue kikombe.’’

Nikamuuliza mpashaji wangu, ‘’Huyu kocha nanI?’’

''Tulizana tumia ubongo wako utamjua,'' Mpashaji alinijibu.

Duru ya pili Kikwete akabwagwa na hivi ndivyo Mkapa alivyokuja kuwa Rais.

Katika ukumbi ule ule wa Chimwaga mwaka wa 1992 hali inayofanana na hii ya 1995 kati ya Kikwete na Mkapa, Prof Malima alibwagwa alipokuwa anagombea kuingia NEC iliyokuwa na viti 20.

Prof. Malima hakuanguka hivi hivi tu mpango makhsusi ulikuwa umepangwa ndani ya CCM dhidi yake na alipoangushwa wabaya wake walikesha wakisheherekea ushindi wao.

Kikwete kama Prof. Malima halikadhalika hakuanguka hivi hivi.

Kama walivyosheherekea kuangushwa kwa Malima miaka mitatu iliyopita halikadhalika ulifanyika mkesha Dodoma kwa kuanguka kwa Kikwete.

Msomaji wangu huoni kuna ‘’variable,’’ zinazofanana katika yale yaliyotokea kwa Prof. Malima 1992 na haya yaliyomfika Kikwete 1995?

Swali la kujiuliza nani anavuruga hizi kete kwenye dama?

Mwalimu Gurumo wa Msondo Ngoma, Juwata Jazz alikuwa akisema,’’Msondo ngoma akili kichwani mwako.’’
 
Muuza Viatu,
Mkutano Maalum wa NEC uliitishwa kuchagua mgombea urais kwa tiketi ya CCM na Jakaya Mrisho Kikwete akashinda akifuatiwa na Benjamin William Mkapa, Cleopa Msuya akiwa wa mwisho.

Kwa kuwa Kikwete hakuweza kupata ‘’absolute majority,’’ ikabidi uchaguzi urudiwe.

Ukumbi ulikuwa umegubigwa na ‘’tension,’’ nzito wajumbe wa CCM walipokuwa wanapiga kura kuchagua kati ya Kikwete na Mkapa.

Jiulize msomaji wangu hii ‘’tension,’’ wasiwasi ulisababishwa na nini ilhali wagombea wote ni wa chama kimoja?

Iweje wajumbe wapate shinikizo la damu ghafla?
Walikuwa wanatishwa na jinamizi lipi?

Kuna tofauti gani katika ya hawa wagombea wawili wa chama kimoja?

Mpashaji wangu alinifahamisha kuwa baadhi ya wajumbe walikuwa wakinong’onezana ndani ya ukumbi wakati wa kupiga kura.

Alipofika hapa nikamsimamisha mpashaji wangu nikamuuliza, ‘’Wewe ulitegemea Kikwete ashinde dhidi ya Mkapa?’’

Mpashaji wangu alicheka akasema, ‘’Alipoingia Mkapa katika kinyang'anyiro kile nilijua yeye atakuwa rais wala sikuwa na wasiwasi kwa kuwa naijua nguvu iliyokuwa nyuma yake kwanza na pili nazijua siasa za Tanzania. Mimi nilikuwa natazama ile senema na kuangalia itaishia wapi hasa pale Kikwete alipoingia dakika za mwisho baada ya Prof. Malima. Nilijua sasa kocha anamwingiza mfungaji magoli timu ichukue kikombe.’’

Nikamuuliza mpashaji wangu, ‘’Huyu kocha nanI?’’

''Tulizana tumia ubongo wako utamjua,'' Mpashaji alinijibu.
Duru ya pili Kikwete akabwagwa na hivi ndivyo Mkapa alivyokuja kuwa Rais.

Katika ukumbi ule ule wa Chimwaga katika 1992 hali inayofanana na hii ya 1995 katika ya Kikwete na Mkapa, Prof Malima alibwagwa alipokuwa anagombea kuingia NEC iliyokuwa na viti 20.

Prof. Malima hakuanguka hivi hivi tu mpango makhsusi ulikuwa umepangwa ndani ya CCM dhidi yake na alipoangushwa wabaya wake walikesha wakisheherekea ushindi wao.

Kikwete kama Prof. Malima halikadhalika hakuanguka hivi hivi.

Kama walivyosheherekea kuangushwa kwa Malima miaka mitatu iliyopita halikadhalika ulifanyika mkesha Dodoma kwa kuanguka kwa Kikwete.

Msomaji wangu huoni kuna ‘’variable,’’ zinazofanana katika yale yaliyotokea kwa Prof. Malima 1992 na haya yaliyomfika Kikwete 1995?

Swali la kujiuliza nani anavuruga hizi kete kwenye dama?

Mwalimu Gurumo wa Msondo Ngoma, Juwata Jazz alikuwa akisema,’’Msondo ngoma akili kichwani mwako.’’
Nimekuelewa Mo,Said
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom