Everton vs Saigon 1967

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,772
30,046
EVERTON VS SAIGON 1967

Rafiki yangu Mohamed Abdulrahman kutoka Ujerumani leo asubuhi kaniandikia kitu kilichonirudisha nyuma sana udogoni.

Soma stori:

"Baada ya kuundwa Saigon Everton ilibaki na tulicheza mechi mbili.
Ya kwanza nilicheza inside right pembeni yangu alikuwa Mkwanda Ingemar Johansson.

Kitu cha ajabu kilitokea.

Mwanzo wa game tu tunaanza nimepokea pasi nikamgongea Mkwanda na yeye akapiga shuti golini kutoka centre na akafunga goli.

Mnazi Mmoja hapo mbele ya Kibarua Bar.
Mechi hii nilikatika jino la chini mbele.

Alama ninayo hadi leo.
Lile goli liliwakasirisha sana Saigon.

Jumanne Masimenti ambae alikuwa akicheza Centre Half Saigon akawa ana overlap kuja mbele kusaidia mashambulizi.

Na hii ilikuwa style ya Everton tulipokuwa hatujagawanyika na lazima goli litapatikana.
Sisi kumuona Jumanne anakuja mbele ikabidi tujazane nyuma kulinda goli.

Hapo ndipo nilipovunjika jino.

Masimenti "Guu la Ngamia," marehemu Harudiki Kabunju akipenda kumwita hivyo, akakutana na loose ball ndani ya box akapiga shuti kali golini.

Nikaweka kichwa nimesimama katikati ya "goal line."
Taya ya juu na ya chini zikaumana jino likakatika.

Jumanne alikuwa na tambo kapanda juu vizuri sana kamchukua baba yake.

Lakini juu ya mwili huu Jumanne alikuwa mpole sana na wababe wakimuogopa hawathubutu kumchokoza.

Ukigongana na Jumanne hewani wewe utaanguka chini yeye atatua na miguu yake miwili kisha akupe lile kono lake kubwa kukunyanyua.

Jumanne alikuwa na mdogo wake Twaha mguu wake wa kushoto mfupi kidogo hivyo akichechemea lakini alikuwa left winger hatari kwa mashuti na mbio.

Akicheza Young Kenya club kali katika club za mitaani.

Wenzake katika timu hii walikuwa Kirk Douglas (Kitwana Douglas), Kesi Kibuda, King Kodo, Denis Law (Jamil Hizam) kwa kuwataja wachache.

Hupita Mnazi Mmoja na wanangu nikawaambia udogoni tumecheza sana mpira kwenye viwanja hivi.

Jumanne alipokwenda Cosmopolitan Coach Mansur Magram ndiyo akambadilisha position na kumchezesha Centre Forward.

Mechi ya pili sikucheza.

Nimerudi shule St. Joseph's Convent School haraka nikafika nyumbani kubadili nguo nawahi kutazama mechi hapo Mnazi Mmoja.

Tukiishi Libya Street jumba la Posta karibu na Mnazi Mmoja.

Nimekuta vurugu kumetokea ugomvi Mkwanda kampiga kichwa Mrisho Wanted kampasua.

Mrisho kuniona mimi naingia kanifata damu zinamvuja usoni.

Mimi maisha yangu yote sikuwa mtu wa ubabe na hata hao wababe wakimuogopa Mrisho sembuse mie kitoto kidogo.

Basi akafika hadi mbele yangu nami "I cooly held my ground."

Nadhani kwa ile heshima niliyokuwanayo na kule kutulia kwangu nikimwangalia aliona aibu hakunigusa.

Wanted siku ile alikuwa ameadhirika kupigwa na Mkwanda mtoto mdogo juu ya ubabe wake wote.

Akamfuata Mkwanda nyumbani kwao.
Mkwanda akatoka ndani kwao kumkabili barabarani.

Mrisho akampiga Mkwanda ngumi ya tumbo.
Mkwanda hakumrudishia alirudi nyuma kashika tumbo lake.

Ugomvi ukaisha Mrisho akaondoka.

Mrisho akajakuwa mtu aliyekuwa na mapenzi makubwa sana na mimi kila akiniona atanipigia kelele, "Eusobio njoo nipe hela niingie kwa Gersan."

Pale Mchikichi na Sikukuu Amani Gersan alifungua mgahawa wake akiuza pilau mchana.
Gersan mwenyewe mbabe unaogopa hata kumwambia kachumbari haikukolea ndimu.

Hii ilikuwa hoteli ya wababe.
Mandava ndiyo wanakutana hapo mchana kula.

Mimi nikiingizwa hapo na Ali Ugaga (Uri Gagarin) mbabe mwenzao tukitokea bandarini.

Siku nyingine tunakwenda kula kwa Matataiwa kisha tukahamia Msimbazi na Kiungani kwa Amiri Ali Mchawi.

Hoteli zote hizi walikuwa na wapishi hodari sana.
Matataiwa akipika hadi mseto na papa.

Allah awarehemu ndugu zetu wote waliotangulia mbele ya haki.
Utoto una raha zake."

PICHA: Kulia ni Mwandishi na Victor John.

Screenshot_20210727-122923_Photos.jpg
 
Stori nzuri za maisha yenu ya utotoni. Nimevutiwa kuona karibu kila mtu enzi zenu ktk stori hii alikuwa amekatiwa jina la mtaani.

Mzee Mohammed Said nicknames zenu Uri Gagarin, Kirk, Wanted n.k zilimaanisha nini kwa kila mtu na kwa sababu gani.
 
Stori nzuri za maisha yenu ya utotoni. Nimevutiwa kuona karibu kila mtu enzi zenu ktk stori hii alikuwa amekatiwa jina la mtaani.

Mzee Mohammed Said nicknames zenu Uri Gagarin, Kirk, Wanted n.k zilimaanisha nini kwa kila mtu na kwa sababu gani.
Bagamoyo,
Hizi ni athari za ukoloni wakati ule muziki, senema, mpira na kila kitu tunaangalia kaskazini.

Empire Cinema wakionyesha senema zile Westerns maisha yalivyokuwa Wild West ubaya, ubaya tu.

Kulikuwa na zile za Hollywood kisha Wataliani wakaja na kama hizo na zilipendwa sana mfano wa movie za Hollywood ni "Shane," actor Allan Ladd.

Mfano wa Italian Spaghetti kama walvyozibeza Hollywood ni, "The Good The Bad And The Ugly," na zilitia fora sana actor Clint Eastwood tena Mmarekani.

Sasa tukawa tunajipa majina ya wale actors.
Katika mpira ni hivyo hivyo unachagua jina la mchezaji unaempenda.

Ndiyo unakuta Kitwana Douglas anacheza mpira lakini kajipa jina la Kirk Douglas ambae ni actor.

Suleiman Jongo anacheza mpira lakini jina lake Rory Calhoun actor.
Haya majina yakavuma na yakatushika na kuchukua nafasi ya majina yetu.

Leo baada ya miaka zaidi ya 50 ukimuuliza Jamil humpati.
Lakini ukitaja Denis Law kila mtu anamfahamu.

Haya hayajaondoka angalia leo majina ya wanamuziki wa Bongo Flavour.
 
Nafanyeje ili niwe mwanachama?
Bujibuji,
Nilibahatika kuingia Muthaiga Club Nairobi mwaka wa 1989 na aliyeniiingiza ni Ally Sykes.

Mimi nilikuwa nakaa 680 Hotel nakaa hapo na vilevile ndipo ilipokuwa mahali nahudhuria mkutano.

Bwana Ally akawa anakuja Nairobi akanambia nikamuone Muthaiga Club kwani hapo ndiyo mafikizio yake kila akija Nairobi.

Mimi nilikuwa siijui Muthaiga Club wala sijapata kuisikia hata siku moja.

Baada ya kumaliza mkutano na kiza kilikuwa kinaanza kuingia nikashuka chini nikachukua taxi ya Mkikuyu mmoja nikamwambia anipeleke Muthaiaga Club.

Jamaa akaniuliza, ''Unakwenda Muthaiga Club?''

Nikamjibu ndiyo.
''Unafata nini Muthaiga Club?''

Hapa nikapigwa na mshangao kidogo kwa swali lile kwani taxi driver ukimfahamisha unapokwenda sana sana atakuuliza sehemu unayokwenda kama yeye haujui vyema lakini hakuulizi unakwenda Gymkhana Club kufanya nini.

''Baba yangu anakaa Muthaiga Club,'' nilimjibu.

''Baba yako anakaa Muthaiga Club?''

Mkikuyu akaniuliza kwa mshangao.

Nikamjibu kuwa hapo ndipo anapofikia kila akija Nairobi.

''Hii mutu ya Tanzania bwana kubwa!''

Mkikuyu sasa anajaza ''dots'' mwenyewe.

Nilipofika Muthaiga ndipo nilipojua kwa nini Mkikuyu yule alishangaa kuona kitoto kidogo kama mimi kinakwenda Muthaiga Club.

Muthaiga Club wanachama Waafrika huwaoni wote Wazungu tena wazee wamepinda migongo na wote mamilionea.

Ukimuona Mwafrika mle ndani jua mtumishi.

Malipo yote hapo unaweka sahihi hakuna kulipa fedha taslimu.

Ukiomba unachama unafanyiwa mahojiano na wanataka kukujua nje ndani, ndani nje.

Unafuata nini katika club.
Unasoma vitabu?

Unapenda kuangalia filamu na zipi?
Lukuki ya maswali wanataka ujibu.

Wenyewe wanasema wanachukia mtu awe mwanachama na aje club kunywa pombe kisha anaondoka.
Wanataka mwanachama akifika club anaingia maktaba kuangalia vitabu vipya na kuazima kwenda kusoma.

Lakini hii yote babaisha ubaguzi umewaelemea hawataki watu katika club yao.

Yapo mengi na haya mengi alikujanieleza Peter Colmore nilipomhoji kuhusu Muthaiga Club.
Peter Colmore ndiye aliyemdhamini Ally Sykes kuwa mwanachama mwaka wa 1967.

Nishamweleza sana huyu mtu Colmore hapa.

Mtafuteni.
Huwezi kuamini.

Gavana wa Kenya wakati wa ukoloni anaomba uanachama na anaweza kukataliwa kuwa mwanachama wa Muthaiga Club.

Gavana hana hela.

Ukitaka kuijua nguvu ya "Capitalism," fika Muthaiga Club Nairobi.

Lakini kubwa ni kuwa ukishafanikiwa kuwa mwanachama wa Muthaiga Club basi ni kuwa tayari ushaunganishwa na club nyingine kama hizo kwingi ulimwenguni.

Fursa ikitokea nitakupa kisa cha Ally Sykes na genge la Roy Wellensky wa Rhodesia pale Wellensky na wenzake walipomuona Ally Sykes Harare Club wakamtolea ufedhuli kwani hawakupatapo wao kumuona mwanachama Mwafrika ndani ya club ile ila waiter, mhudumu wamemvisha unifomu inayowapendeza wao wakimtuma kwa dharau.

Rhodesia ilikuwa Zimbabwe na Salsibury ni Harare na nchi iko huru na Robert Mugabe ndiye rais lakini Wazungu hawataki kuamini.

Tuje kwenye Saigon Club.
Ally Sykes alikuwa mwanachama.

Wewe ndugu yangu Bujibuji unataka kuwa mwanachama lakini hata kabla hujawa mwanachama unatukebehi ati Saigon ndiyo tunaamua nani awe rais wa Tanzania.

Leo unauliza ufanye nini uwe mwanachama wa chama chenye nguvu ya kuunda serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwani ukitaka kuwa mwanachama wa CCM, Yanga au Simba mtu anafanya nini?

PICHA:
Picha ya kwanza Ally Sykes na M-wandishi Muthaiga Club 1989 na ya pili Ally Sykes wa kwanza kulia, Sheikk Issa Ausi, na wa mwisho Juma Abeid (Spencer) wakiwa kwenye Khitma ya Saigon 2010,

1627471862750.png

1627472032799.png
 
Bujibuji,
Nilibahatika kuingia Muthaiga Club Nairobi mwaka wa 1989 na aliyeniiingiza ni Ally Sykes.

Mimi nilikuwa nakaa 680 Hotel nakaa hapo na vilevile ndipo ilipokuwa mahali nahudhuria mkutano.

Bwana Ally akawa anakuja Nairobi akanambia nikamuone Muthaiga Club kwani hapo ndiyo mafikizio yake kila akija Nairobi.

Mimi nilikuwa siijui Muthaiga Club wala sijapata kuisikia hata siku moja.

Baada ya kumaliza mkutano na kiza kilikuwa kinaanza kuingia nikashuka chini nikachukua taxi ya Mkikuyu mmoja nikamwambia anipeleke Muthaiaga Club.

Jamaa akaniuliza, ''Unakwenda Muthaiga Club?''

Nikamjibu ndiyo.
''Unafata nini Muthaiga Club?''

Hapa nikapigwa na mshangao kidogo kwa swali lile kwani taxi driver ukimfahamisha unapokwenda sana sana atakuuliza sehemu unayokwenda kama yeye haujui vyema lakini hakuulizi unakwenda Gymkhana Club kufanya nini.

''Baba yangu anakaa Muthaiga Club,'' nilimjibu.

''Baba yako anakaa Muthaiga Club?''

Mkikuyu akaniuliza kwa mshangao.

Nikamjibu kuwa hapo ndipo anapofikia kila akija Nairobi.
''Hii mutu ya Tanzania bwana kubwa!''

Mkikuyu sasa anajaza ''dots'' mwenyewe.

Nilipofika Muthaiga ndipo nilipojua kwa nini Mkikuyu yule alishangaa kuona kitoto kidogo kama mimi kinakwenda Muthaiga Club.

Muthaiga Club wanachama Waafrika huwaoni wote Wazungu tena wazee wamepinda migongo na wote mamilionea.

Ukimuona Mwafrika mle ndani jua mtumishi.

Malipo yote hapo unaweka sahihi hakuna kulipa fedha taslimu.

Ukiomba unachama unafanyiwa mahojiano na wanataka kukujua nje ndani, ndani nje.

Unafuata nini katika club.
Unasoma vitabu?

Unapenda kuangalia filamu na zipi?
Lukuki ya maswali wanataka ujibu.

Wenyewe wanasema wanachukia mtu awe mwanachama na aje club kunywa pombe kisha anaondoka.
Wanataka mwanachama akifika club anaingia maktaba kuangalia vitabu vipya na kuazima kwenda kusoma.

Lakini hii yote babaisha ubaguzi umewaelemea hawataki watu katika club yao.

Yapo mengi na haya mengi alikujanieleza Peter Colmore nilipomhoji kuhusu Muthaiga Club.
Peter Colmore ndiye aliyemdhamini Ally Sykes kuwa mwanachama mwaka wa 1967.

Nishamweleza sana huyu mtu Colmore hapa.

Mtafuteni.
Huwezi kuamini.

Gavana wa Kenya wakati wa ukoloni anaomba uanachama na anaweza kukataliwa kuwa mwanachama wa Muthaiga Club.

Gavana hana hela.

Ukitaka kuijua nguvu ya "Capitalism," fika Muthaiga Club Nairobi.

Lakini kubwa ni kuwa ukishafanikiwa kuwa mwanachama wa Muthaiga Club basi ni kuwa tayari ushaunganishwa na club nyingine kama hizo kwingi ulimwenguni.

Fursa ikitokea nitakupa kisa cha Ally Sykes na genge la Roy Wellensky wa Rhodesia pale Wellensky na wenzake walipomuona Ally Sykes Harare Club wakamtolea ufedhuli kwani hawakupatapo wao kumuona mwanachama Mwafrika ndani ya club ile ila waiter, mhudumu wamemvisha unifomu inayowapendeza wao wakimtuma kwa dharau.

Rhodesia ilikuwa Zimbabwe na Salsibury ni Harare na nchi iko huru na Robert Mugabe ndiye rais lakini Wazungu hawataki kuamini.

Tuje kwenye Saigon Club.
Ally Sykes alikuwa mwanachama.

Wewe ndugu yangu Bujibuji unataka kuwa mwanachama lakini hata kabla hujawa mwanachama unatukebehi ati Saigon ndiyo tunaamua nani awe rais wa Tanzania.

Leo unauliza ufanye nini uwe mwanachama wa chama chenye nguvu ya kuunda serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwani ukitaka kuwa mwanachama wa CCM, Yanga au Simba mtu anafanya nini?

PICHA:
Picha ya kwanza Ally Sykes na M-wandishi Muthaiga Club 1989 na ya pili Ally Sykes wa kwanza kulia, Sheikk Issa Ausi, na wa mwisho Juma Abeid (Spencer) wakiwa kwenye Khitma ya Saigon 2010,

View attachment 1871567
View attachment 1871573
Swali langu halikuwa la kebehi, kipindi Mkapa anakaribia kuondoka, tulijulishwa Saigon wamemtaka Kimwete ndio awe rais wa nchi hii, akawa.
Pia nimewahi kusikia kuwa pakiwa na kisomo nasikia mitaa kadhaa hufungwa.
Nitafurahi sana nikiwa mmoja wenu
 
Swali langu halikuwa la kebehi, kipindi Mkapa anakaribia kuondoka, tulijulishwa Saigon wamemtaka Kimwete ndio awe rais wa nchi hii, akawa.
Pia nimewahi kusikia kuwa pakiwa na kisomo nasikia mitaa kadhaa hufungwa.
Nitafurahi sana nikiwa mmoja wenu
Bujibuji,
Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimtaka Julius Nyerere awe Waziri Mkuu wa Tanganyika na akawa kweli.

Hii ilikuwa 1953.

Unanifanya nianze kuangalia nyuma.

Unamjua nani alimtaka Kikwete agombee urais 1995 na kwa sababu gani?

Haikua Saigon.

Saigon ichague rais halafu serikali nzima iwe 20:80?

Mawaziri 20:3.
Inaingia akilini?

Ndiyo nikasema hii ni kejeli.

Unamjua aliemkingia kifua Mkapa apite Dodoma duru ya pili baada ya kushindwa ile ya kwanza?
 
Bujibuji,
Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimtaka Julius Nyerere awe Waziri Mkuu wa Tanganyika na akawa kweli.

Hii ilikuwa 1953.

Unanifanya nianze kuangalia nyuma.

Unamjua nani alimtaka Kikwete agombee urais 1995 na kwa sababu gani?

Haikua Saigon.

Saigon ichague rais halafu serikali nzima iwe 20:80?

Mawaziri 20:3.
Inaingia akilini?

Ndiyo nikasema hii ni kejeli.

Unamjua aliemkingia kifua Mkapa apite Dodoma duru ya pili baada ya kushindwa ile ya kwanza?

Kumbe Saigoni jumuiya ya kiislam?nilikua sijui.
 
Bujibuji,
Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimtaka Julius Nyerere awe Waziri Mkuu wa Tanganyika na akawa kweli.

Hii ilikuwa 1953.

Unanifanya nianze kuangalia nyuma.

Unamjua nani alimtaka Kikwete agombee urais 1995 na kwa sababu gani?

Haikua Saigon.

Saigon ichague rais halafu serikali nzima iwe 20:80?

Mawaziri 20:3.
Inaingia akilini?

Ndiyo nikasema hii ni kejeli.

Unamjua aliemkingia kifua Mkapa apite Dodoma duru ya pili baada ya kushindwa ile ya kwanza?
Naomba ufunge makablasha yako, una madini adhimu sana. Nakukubali sana mzee wangu.
 
Bujibuji,
Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimtaka Julius Nyerere awe Waziri Mkuu wa Tanganyika na akawa kweli.

Hii ilikuwa 1953.

Unanifanya nianze kuangalia nyuma.

Unamjua nani alimtaka Kikwete agombee urais 1995 na kwa sababu gani?

Haikua Saigon.

Saigon ichague rais halafu serikali nzima iwe 20:80?

Mawaziri 20:3.
Inaingia akilini?

Ndiyo nikasema hii ni kejeli.

Unamjua aliemkingia kifua Mkapa apite Dodoma duru ya pili baada ya kushindwa ile ya kwanza?
Fungua makabati yako mwalimu
 
Kumbe Saigoni jumuiya ya kiislam?nilikua sijui.
Wa...
Unadhani utamtisha mtu kwa maneno hayo?

Ati nilikuwa sijui.
Kwani wewe ulikuwa unajua nini?

1627497667658.png

Khitma Saigon kushoto Sunday Kayuni, Harudiki Kabunju na Atika Kombo.

1627497819177.png

Khitma Saigon: Kulia Sheikh Yahya Hussein, Stephen John Rupia, Hamza Kassongo na Kitwana Manara.
 
Missile...
Taratibu tutajadili kwa pamoja.
Ilm bila khiyana.
Mzee Mohamed Said, tunamuomba Mwenyezi Mungu akutie nguvu na kukupa afya njema ili uweze kuandika vitabu vingi zaidi vitakavyo tuelimisha mambo ya kale! Barikiwa sana.
 
Asante sana Mwl. Nyerere uliwaweza ssna wadini hawa.
Wa...
Umeghadhibika.

Unawakebehi Waislam unasema,"Ahsante sana Mwl. Nyerere uliwaweza sana wadini hawa."

Ninì kimekukasirisha?

Kuwa Saigon wanasoma Khitma na kufuturisha kila mwaka?

Tuje kwenye tuhuma yako ya udini.
Nini ambacho wewe unaona katuweza?

Wazee wetu hawakuwa wabaguzi wa kumbagua mtu kwa dini yake.

Bahati mbaya Mwalimu yeye mwenyewe hakupenda kueleza historia yake ni vipi na ni nani waliompokea Dar es Salaam.

Bahati mbaya Mwalimu hakupata kueleza ni vipi alichaguliwa katika nafasi ya juu kabisa katika TAA katika uchaguzi wa mwaka wa 1953.

Mwalimu hakueleza kuwa ilikuwa shida kubwa kwake kushinda uchaguzi ule ambao alishinda kwa kura chache sana.

Ipo sababu yake ukitaka kujua niambie.

Mwalimu hakueleza hata kama alipata kugombea nafasi ya Rais wa TAA katika Ukumbi wa Arnautoglo dhidi ya Abdulwahid Sykes aliyekuwa Kaimu Rais wa TAA na Katibu; Katibu kwa miaka minne mfululizo kuanzia 1950 na Kaimu Rais kuanzia 1951.

Uchaguzi huu ulifanyika tarehe 17 April 1953.

Judith Listowel kaueleza vizuri uchaguzi huu katika kitabu chake, "The Making of Tanganyika," (1965).

Mimi nayajua mengi kupita Listowel kwa kuwa historia hii ni ya watu wangu ni historia ya wazee wangu na katika kuieleza si kuwa nataka kumueleza Nyerere la hasha Mwalimu anaingia kama sehemu ya historia ya wazee wangu.

Ushajiuliza kwa nini Nyerere hakupenda kueleza historia yake?

Ukitaka kujua nifahamishe.

Hawa wazee wangu ndiyo waliomuweka Nyerere madarakani na kumfikisha pale alipofika.

Kuwa wewe unathubutu kuwatusi wazee wangu na kuwaita, "wadini hawa," mimi sina la kukujibu ila neno moja tu kuwa "hutujui."

1627588308842.png


1627588545877.png

1627590098265.png

Ndugu yangu,
Mtafute Julius Kambarage Nyerere katika makundi haya ya Waislam.

Picha ya juu mwaka ni 1956 watu wamerudi Hija wako shambani kwa Sheikh Abdallah Chaurembo Mtoni wamekusanyika kuomba dua kwa mengi na kubwa Tanganyika ipate uhuru.

Picha inayofuatia ina maelezo ni mwaka wa 1957.

Wako wapi hao Wengine?

(Wengine nimeweka herufi kubwa usidhani nimekosea ipo maana hapo).

Ikiwa hujui niulize.

Unajua sababu gani Wengine walikuwa wanamnyanyapaa Nyerere?

Ukitaka kujua sababu nifahamishe.

1627589987361.png
 
Mo Said,wewe ni kisima cha historia, document hiyo elimu yako ili vizazi vya sasa na vijavyo vinufaike
 

Similar Discussions

13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom