Evariste Ndayishimiye aapishwa kuwa Rais mpya wa Burundi

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
1592482259277.png


Burundi imemuapisha rais mpya wa taifa hilo , Evariste Ndayishimiye, katika hafla iliofanyika mbele ya raia wa taifa hilo na baadhi ya viongozi kutoka mataifa tofauti.

Katika kiapo chake rais huyo ameapa kulinda katiba ya Burundi, kuheshimu umoja wa raia wa taifa hilo, kutoa haki kwa wote mbali na kutetea mipaka ya taifa hilo.

Kiapo hicho kinatokana na kifungu cha 107 cha katiba ya nchi hiyo

Sherehe hiyo iliofanyika katika uwanja wa kandanda wa Ingoma katika mkoa wa Gitega imefanyika wakati ambapo taifa hilo limeathirika na mlipuko wa vurusi vya corona.

Rais Evariste baada ya kumaliza kula kiapo alkagua gwaride la kijeshi na baadaye kutoa hotuba.

Muda mchache kabla ya kula kiapo rais Evariste aliombewa na baadhi ya maaskofu ambao walimtaka kufungua milango ya uhusiano mwema na mataifa mengine.

Mbali na kwamba baadhi ya wageni hawakuvalia barakoa, raia wengi waliohudhuria hafla hiyo hawakuvaa kifaa hicho cha kuwalinda dhidi ya corona.

Hatahivyo shirika la msalaba mwekundu liliandaa maji na sabuni kwa raia wote waliokuwa wakiingia katika uwanja huo kuosha mikono yao.

Maelfu ya raia wa Burundi wamefurika katika uwanja huo wakisubiri kuapishwa kwa rais huyo kufuatia kifo cha aliyekuwa rais wa taifa hilo Pierre Nkurunziza.

Makamu wa rais wa Tanzania bi Samia Suluhu na aliyekuwa rais wa taifa hilo jakaya Mrisho Kikwete wamewasili nchi humo.

BBC Swahili
 
Hivyo viapo havina maana kwani wakishakwaa utawala wanaojiingiza kwenye vitengo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Na huyo muonekano wake inavyoonyesha anaweza kuja kuwa mbaya kuliko Nkurunziza na labda ndio kigezo alichokitumia kumteua awe mrithi wake.

Hamna mabadiliko yoyote hapo ni sawa tu na kubadilisha gongo kwa kuiondoa kwenye chupa ya soda na kuimimina kwenye chupa ya bia. Very hopeless indeed.
 
U
Hivyo viapo havina maana kwani wakishakwaa utawala wanaojiingiza kwenye vitengo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Na huyo muonekano wake inavyoonyesha anaweza kuja kuwa mbaya kuliko Nkurunziza na labda ndio kigezo alichokitumia kumteua awe mrithi wake.

Hamna mabadiliko yoyote hapo ni sawa tu na kubadilisha gongo kwa kuiondoa kwenye chupa ya soda na kuimimina kwenye chupa ya bia. Very hopeless indeed.
Mada mpya, kitabu kilekile!!
Ndaishimiye: Katibu Mkuu wa chama tawala (CNDD/FDD), mshauri wa Nkuruzinza, waziri wa Ulinzi zama za Nkuruzinza, meja generali mstaafu, ......
Naamini nimeeleweka
 
U
Mada mpya, kitabu kilekile!!
Ndaishimiye: Katibu Mkuu wa chama tawala (CNDD/FDD), mshauri wa Nkuruzinza, waziri wa Ulinzi zama za Nkuruzinza, meja generali mstaafu, ......
Naamini nimeeleweka
Heeeeeh kumbeeee? Lol mbna ni sheeeda sasa hiii.
 
Hivyo viapo havina maana kwani wakishakwaa utawala wanaojiingiza kwenye vitengo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Na huyo muonekano wake inavyoonyesha anaweza kuja kuwa mbaya kuliko Nkurunziza na labda ndio kigezo alichokitumia kumteua awe mrithi wake.

Hamna mabadiliko yoyote hapo ni sawa tu na kubadilisha gongo kwa kuiondoa kwenye chupa ya soda na kuimimina kwenye chupa ya bia. Very hopeless indeed.

U
Mada mpya, kitabu kilekile!!
Ndaishimiye: Katibu Mkuu wa chama tawala (CNDD/FDD), mshauri wa Nkuruzinza, waziri wa Ulinzi zama za Nkuruzinza, meja generali mstaafu, ......
Naamini nimeeleweka

Leo kwenye hotuba yake amesema hataki kabisa kusikia mambo ya Upinzani na hamna nafasi hio,kwanza kwanini watu waipinge serikali?Ameuliza

Nkurunziza yawezekana alikua na afadhali kulinganisha na huyu.
 
U
Mada mpya, kitabu kilekile!!
Ndaishimiye: Katibu Mkuu wa chama tawala (CNDD/FDD), mshauri wa Nkuruzinza, waziri wa Ulinzi zama za Nkuruzinza, meja generali mstaafu, ......
Naamini nimeeleweka
Lakini ana hofu ya mungu,,ni muumini mzuri
 
Hongera na kila jema kwako Evariste Ndayishimiye, Rais wa Burundi.
 
Leo kwenye hotuba yake amesema hataki kabisa kusikia mambo ya Upinzani na hamna nafasi hio,kwanza kwanini watu waipinge serikali?Ameuliza

Nkurunziza yawezekana alikua na afadhali kulinganisha na huyu.
😃😃duhh kasema hivyo? ndio maana waliona wamuapishe tu kabla ya wakati ili waepushe vita ya wenyewe kwa wenyewe
 
Kama ilivyo kawaida ya Nyota kung'aa popote pale, JK ndio Mgeni pekee ambae Rais mpya wa Burundi aliona ampe fursa ahutubie Umati wa wahudhuriaji, nae kama kawaida yake hakutuangusha Muungwana yule ambae alimaliza hotuba yake kwa deremo ukumbi Mzima
 
duhh kasema hivyo? ndio maana waliona wamuapishe tu kabla ya wakati ili waepushe vita ya wenyewe kwa wenyewe

Hahah amesema hivyo mkuu na amemelizia kwa kusema Wapinzani na vyombo vya habari nchini humo wanatumiwa na mabeberu na yeye ataendeleza wembe ule ule wa Nkurunziza.
 
Back
Top Bottom