kuti kavu
Member
- Feb 25, 2009
- 68
- 21
Baada ya kuchomwa na jua mpaka jasho kukauka katika harakati zangu za kujenga taifa letu 'changa' pia ikiwa kama niia ya kupata mkate wa kila siku,hatimae nabahatika kupata msamaria mwema anaekubali kuniazima walau ukurasa wa gazeti la leo la Nipashe,ni kaukurasa ka 5, nakapembua na kukutana na kichwa cha habari kimoja kisemacho "waekezaji wengi huja kuchuma na kuondoka".
Katika kupitia nakuja ona ni kauli iliyotolewa na mtaalamu wa masuala ya uchumi kutoka chuo kikuu cha cha Dar es salaam Dk. Haji Semboja wakatiwa kongamano la biashara kati ya China na Bara la Afrika. Semboja anendelea kulalamika kuwa wawekezeji hao wanakuja Tanzania wakiwa na lengo moja tu la kuchuma na sio kuendeleza Nchi yetu.
Kauli ya Semboja imenipa maswali mengi ambayo labda wana JF wenzangu mnaweza kunisaidia kuyajibu...
Hivi lengo kuu la mwekezaji yeyote ni lip zaidi ya ukupata faida???.....
Kati ya mwekezaji na yule anaemkaribisha huyo mwekezaji ni nani mwenye jukumu la kuhakikisha mikataba ya ki-uwekezaji haitamnufaisha mwekezaji bali iwanuafaishe na wale wenye rasilimali zilizomvutia mwekezaji huyo???....
Ni Nchi gani hapa duniani ambayo ilipokea wawekezaji waliokuja nchini humo kwa lengo la kuto kujinufaisha ila kuleta maendeleo ya nchi hiyo husika???....
Na je si jukumu la wasomi wa fani ya uchumi kama Dk Semboka kutusaidia sisi wanyonge kutengeneza mazingira ambayo hatamnufaisha muwekezaji ila na sisi pia ambao tunanyonywa na wawekezaji hao???...
Nionavyo mimi kauli hii ya Dr Semboja ni sawa na baba mwenye nyumba kuwaambia watoto wake wadogo kuwa lengo la njaa siku zote ni kuua,ilhali ni jukumu lake kuleta chakula nyumbani!!!!
Katika kupitia nakuja ona ni kauli iliyotolewa na mtaalamu wa masuala ya uchumi kutoka chuo kikuu cha cha Dar es salaam Dk. Haji Semboja wakatiwa kongamano la biashara kati ya China na Bara la Afrika. Semboja anendelea kulalamika kuwa wawekezeji hao wanakuja Tanzania wakiwa na lengo moja tu la kuchuma na sio kuendeleza Nchi yetu.
Kauli ya Semboja imenipa maswali mengi ambayo labda wana JF wenzangu mnaweza kunisaidia kuyajibu...
Hivi lengo kuu la mwekezaji yeyote ni lip zaidi ya ukupata faida???.....
Kati ya mwekezaji na yule anaemkaribisha huyo mwekezaji ni nani mwenye jukumu la kuhakikisha mikataba ya ki-uwekezaji haitamnufaisha mwekezaji bali iwanuafaishe na wale wenye rasilimali zilizomvutia mwekezaji huyo???....
Ni Nchi gani hapa duniani ambayo ilipokea wawekezaji waliokuja nchini humo kwa lengo la kuto kujinufaisha ila kuleta maendeleo ya nchi hiyo husika???....
Na je si jukumu la wasomi wa fani ya uchumi kama Dk Semboka kutusaidia sisi wanyonge kutengeneza mazingira ambayo hatamnufaisha muwekezaji ila na sisi pia ambao tunanyonywa na wawekezaji hao???...
Nionavyo mimi kauli hii ya Dr Semboja ni sawa na baba mwenye nyumba kuwaambia watoto wake wadogo kuwa lengo la njaa siku zote ni kuua,ilhali ni jukumu lake kuleta chakula nyumbani!!!!