BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
kwa kipi hasa alichokifanya!?
Hawa wanafiki wa CCM kwa kujibaraguza!! Mbona hawajaandamana kumpongeza Slaa aliyeibua uozo mkubwa ndani ya BOT uliosababisha wizi wa mabilioni ya shilingi!? Mbona hawajaandamana kumpongeza Zitto kwa kuibua uozo mkubwa kuhusiana na mkataba wa Buzwagi ambapo yote aliyosema yalikuwa kweli tupu na mkataba ambao hauna manufaa yoyote kwa Watanzania?
JK azima maandamano CCM
na Waandishi Wetu
Tanzania Daima
RAIS Jakaya Kikwete amezima maandamano ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yaliyokuwa yafanyike kwa ajili ya kumpongeza kwa hatua yake ya kutengua uteuzi wa Gavana wa Benki Kuu, (BoT), Daudi Balali.
Maandamano hayo ya CCM yalipangwa yafanyike nchi nzima kwa siku tofauti ambapo Mkoa wa Dar es Salaam na Lindi, ilipanga kufanya maandamano hayo juzi.
Habari kutoka ndani ya CCM, zinasema kuwa Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho taifa, awali hakuwa na taarifa ya kuwapo kwa maandamano.
Vyanzo vyetu vya habari vya kuaminika vimesema CCM iliamua kufanya maandalizi hayo kimya kimya bila kumjulisha rais kutokana na hulka yake ya kukataa kuandaliwa maandamano, hafla au mapokezi ya kishindo na tayari alishazima maandamno ya aina hiyo siku za nyuma.
"Safari hii pia chama kimejiandaa, lakini dakika za mwisho akapata taarifa hizo, akapiga 'stop', akaamuru yasifanyike na hataki kusikia kitu kama hicho, basi tumeshindwa na hatutafanya tena maandamano, maana bwana mkubwa hayataki..," chanzo chetu cha habari kilisema.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mkoa wa Dar es Salaam tayari ulishakamilisha maandalizi ya maandamano hayo ambayo yangeishia katika ofisi ndogo za CCM, Lumumba na kufuatiwa na hotuba za pongezi na hatimaye Rais mwenyewe angezungumza na wanachama wa CCM.
Maandamano hayo mbali ya kuwa na hotuba, yangesindikizwa na burudani mbalimbali kutoka kundi la burudani la CCM, Tanzania One Theater (TOT) na makundi mengine.
Mkoani Lindi nako, taarifa zinasema kuwa, baadhi ya maofisa waandamizi wa chama hicho walisafiri hadi Lindi kushiriki maandamno hayo, lakini hayakufanyika kutokana na Rais Kikwete kuyapiga marufuku.
Akizungumzia hali hiyo, Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Barongo alikiri kuahirishwa kwa maandamano yaliyoandaliwa na mkoa wake.
Alisema maandamano hayo yaliahirishwa baada ya mgeni rasmi aliyetarajiwa kuwapo siku ya maandamano (juzi), kuwa Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho ya miaka 44 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
"Kweli tulikuwa na maandamano, lakini tumeyaahirisha hadi hapo tutakapokaa na kupanga tena, kwa kuwa mgeni rasmi ambaye tulikuwa tumemwandaa alikuwa kwenye sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar," alisema Barongo.
Hata hivyo, Barongo alipobanwa kutaka ataje jina la mgeni rasmi ambaye kukosekana kwake kumesababisha kuahirisha maandamano hayo, alikataa katakata kumtaja.
"Mgeni rasmi unataka kumjua wa nini? Haina haja, kwani maandamano si yameahirishwa? Hayo mengine yatakuwa na mgeni rasmi mwingine…." alisema Barongo.
Aidha, Barongo alikana kuwa Rais Kikwete ndiye aliyezima maandamano hayo kwa madai kuwa Kikwete hakuwa na taarifa ya kuwapo maandamano hayo.
Vyanzo zaidi vya habari vilisema kuwa hii ni kawaida kwa Rais Kikwete kuzima maandamano, kwani alishazuia kufanyika maandamano ya kumpongeza pale alipotunukiwa tuzo ya Leon Sullivan na wafanyabiashara wa asili ya Kiafrika waishio nchini Marekani, kwa kukubali mkutano wao ufanyike Arusha Juni mwaka huu.
Pia Rais Kikwete alikataa kufanyiwa hafla ya kupongezwa hivi karibuni baada ya mkutano mkuu wa CCM Dodoma, ambapo alichaguliwa kwa kura nyingi za ndiyo kwa ajili ya kuendelea kuwa mwenyekiti wa chama hicho.
Wiki iliyopita, Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Ballali na kumteua Profesa Beno Ndulu kuwa gavana mpya.
Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Ballali kwa madai ya kukiuka kwa makusudi sheria, kanuni na taratibu za uuzaji wa madeni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa ikisimamiwa na Benki Kuu.
Hasira hizo za Rais Kikwete zimetokana na kubainika kuwa kampuni 22 zikitumia hati na nyaraka bandia au zikiwa hazina usajili halali, zililipwa zaidi ya sh bilioni 133 na BoT kupitia akaunti ya EPA.
Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete alitoa agizo la miezi sita kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema, Mkurungenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kuhakikisha wanachunguza na kuwachukulia hatua wahusika wa ubadhirifu huo wa kihistoria.
Wengi walimpongeza Kikwete kwa hatua hiyo, lakini wachache wakihoji uhalali wa rais kutengua uteuzi wa Ballali badala ya kumfukuza kazi.
Hawa wanafiki wa CCM kwa kujibaraguza!! Mbona hawajaandamana kumpongeza Slaa aliyeibua uozo mkubwa ndani ya BOT uliosababisha wizi wa mabilioni ya shilingi!? Mbona hawajaandamana kumpongeza Zitto kwa kuibua uozo mkubwa kuhusiana na mkataba wa Buzwagi ambapo yote aliyosema yalikuwa kweli tupu na mkataba ambao hauna manufaa yoyote kwa Watanzania?
JK azima maandamano CCM
na Waandishi Wetu
Tanzania Daima
RAIS Jakaya Kikwete amezima maandamano ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yaliyokuwa yafanyike kwa ajili ya kumpongeza kwa hatua yake ya kutengua uteuzi wa Gavana wa Benki Kuu, (BoT), Daudi Balali.
Maandamano hayo ya CCM yalipangwa yafanyike nchi nzima kwa siku tofauti ambapo Mkoa wa Dar es Salaam na Lindi, ilipanga kufanya maandamano hayo juzi.
Habari kutoka ndani ya CCM, zinasema kuwa Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho taifa, awali hakuwa na taarifa ya kuwapo kwa maandamano.
Vyanzo vyetu vya habari vya kuaminika vimesema CCM iliamua kufanya maandalizi hayo kimya kimya bila kumjulisha rais kutokana na hulka yake ya kukataa kuandaliwa maandamano, hafla au mapokezi ya kishindo na tayari alishazima maandamno ya aina hiyo siku za nyuma.
"Safari hii pia chama kimejiandaa, lakini dakika za mwisho akapata taarifa hizo, akapiga 'stop', akaamuru yasifanyike na hataki kusikia kitu kama hicho, basi tumeshindwa na hatutafanya tena maandamano, maana bwana mkubwa hayataki..," chanzo chetu cha habari kilisema.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mkoa wa Dar es Salaam tayari ulishakamilisha maandalizi ya maandamano hayo ambayo yangeishia katika ofisi ndogo za CCM, Lumumba na kufuatiwa na hotuba za pongezi na hatimaye Rais mwenyewe angezungumza na wanachama wa CCM.
Maandamano hayo mbali ya kuwa na hotuba, yangesindikizwa na burudani mbalimbali kutoka kundi la burudani la CCM, Tanzania One Theater (TOT) na makundi mengine.
Mkoani Lindi nako, taarifa zinasema kuwa, baadhi ya maofisa waandamizi wa chama hicho walisafiri hadi Lindi kushiriki maandamno hayo, lakini hayakufanyika kutokana na Rais Kikwete kuyapiga marufuku.
Akizungumzia hali hiyo, Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Barongo alikiri kuahirishwa kwa maandamano yaliyoandaliwa na mkoa wake.
Alisema maandamano hayo yaliahirishwa baada ya mgeni rasmi aliyetarajiwa kuwapo siku ya maandamano (juzi), kuwa Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho ya miaka 44 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
"Kweli tulikuwa na maandamano, lakini tumeyaahirisha hadi hapo tutakapokaa na kupanga tena, kwa kuwa mgeni rasmi ambaye tulikuwa tumemwandaa alikuwa kwenye sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar," alisema Barongo.
Hata hivyo, Barongo alipobanwa kutaka ataje jina la mgeni rasmi ambaye kukosekana kwake kumesababisha kuahirisha maandamano hayo, alikataa katakata kumtaja.
"Mgeni rasmi unataka kumjua wa nini? Haina haja, kwani maandamano si yameahirishwa? Hayo mengine yatakuwa na mgeni rasmi mwingine…." alisema Barongo.
Aidha, Barongo alikana kuwa Rais Kikwete ndiye aliyezima maandamano hayo kwa madai kuwa Kikwete hakuwa na taarifa ya kuwapo maandamano hayo.
Vyanzo zaidi vya habari vilisema kuwa hii ni kawaida kwa Rais Kikwete kuzima maandamano, kwani alishazuia kufanyika maandamano ya kumpongeza pale alipotunukiwa tuzo ya Leon Sullivan na wafanyabiashara wa asili ya Kiafrika waishio nchini Marekani, kwa kukubali mkutano wao ufanyike Arusha Juni mwaka huu.
Pia Rais Kikwete alikataa kufanyiwa hafla ya kupongezwa hivi karibuni baada ya mkutano mkuu wa CCM Dodoma, ambapo alichaguliwa kwa kura nyingi za ndiyo kwa ajili ya kuendelea kuwa mwenyekiti wa chama hicho.
Wiki iliyopita, Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Ballali na kumteua Profesa Beno Ndulu kuwa gavana mpya.
Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Ballali kwa madai ya kukiuka kwa makusudi sheria, kanuni na taratibu za uuzaji wa madeni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa ikisimamiwa na Benki Kuu.
Hasira hizo za Rais Kikwete zimetokana na kubainika kuwa kampuni 22 zikitumia hati na nyaraka bandia au zikiwa hazina usajili halali, zililipwa zaidi ya sh bilioni 133 na BoT kupitia akaunti ya EPA.
Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete alitoa agizo la miezi sita kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema, Mkurungenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kuhakikisha wanachunguza na kuwachukulia hatua wahusika wa ubadhirifu huo wa kihistoria.
Wengi walimpongeza Kikwete kwa hatua hiyo, lakini wachache wakihoji uhalali wa rais kutengua uteuzi wa Ballali badala ya kumfukuza kazi.