Diana-DaboDiff
JF-Expert Member
- Jul 13, 2009
- 376
- 19
Hili tatizo lipo na sio ma-secretary peke bali kina dada wote wa ngazi za chini maofisini wanapata taabu sana kutoka kwa mabosi wao na kwakua kazi ni za shida wengine huangukia mitego hii.Kuna upande mwingine pia ambao haujaongelewa hapa,kuna ofisi ya jirani imepata bosi mpya sasa ma-secretary pale walizoea kujigonga kwa mabosi basi wakawa wanafanya kila jinsi mavazi,vituko siku moja bosi akawaita wote wawili akawaambia sikilizeni mimi nina mke na watoto na sijui hapa ilikuwaje kabla lakini mimi hata mkija uchi sitaki,nahitaji ufanisi na kujituma.Pia nawahakikishia mwenye shida ya kweli natamsaidia kama wafanyakazi wote,wadada wakawa wanaangalia chini.Kwahiyo msiwalaumu mabosi tu.