Uchaguzi 2020 Eti ‘tunataka Tume huru’ wakati chaguzi za vyama vyenu hazina huo uhuru, wanafiki wakubwa!

Hero

JF-Expert Member
Aug 20, 2010
3,932
2,832
Katika kutafakari juu ya agenda ya vyama pinzani hapa Tanzania tunapoelekea Uchaguzi, nimewaza na kawazua bila kupata majibu juu ya yale yanayojiri kwenye vyama vyenyewe na kile wanachojaribu kushinikiza kifanyike!

Katika yote vifanyavyo hivi vyama vinajaribu kuhadaa watz kama mtakavyoona kwenye clips hapo chini!

Dai la tume huru ya uchaguzi: hiki kiini macho kimekuwa agenda kwa vyama hivi hasa baada ya kukosa agenda mbadala itakayoweza pambanishwa na Ccm iliyojizatiti kwa kujibu vijiagenda vyote vilivyokuwa vikiwapa kiki ktk awamu zilizopita!

Hivyo kwa sasa hawana agenda yenye mashiko ya kuipinga CCM! Uhalisia kwenye vyama vyao ni kinyume kabisa, huko hakuna utaratibu uliowazi na huru katika kuendesha chaguzi zao wenywe, na ndio maana kila kukiwa na uchaguzi ktk vyama hivi lazima malalamiko yatokee ya namna viongozi wao wa juu wasivyoruhusu huo uhuru wa vijitume vyao vya uchaguzi, lakini viongozi hao hao ndio wanahadaa watz kutaka kushinikiza tume huru.

Ingekuwa ni jambo la hekima kama wangeanza kuonyesha uwepo wa tume huru kwenye chaguzi zao za vyama kabla ya kunyooshea kidole tume yetu ya taifa ya uchaguzi ambayo inao uhuru kwa kiasi kikubwa hata kuliko kwenye vitume vya vyama vyao ambavyo havina uhuru hata kidogo! Anachosema na kutaka Zito au Mbowe ndio kinachotekelezwa na vijitume vyao vya uchaguzi!

Kwa maana hiyo, hawa watu hawana hadhi ya kuomba tume huru ya taifa ya uchaguzi zaidi ya hii iliyopo yenye uhuru wa kutosha usio holela!

Jambo jingine ni uhuru wa kujieleza: hiki kiini macho cha akina Mbowe na Zito ni cha kitoto sana. Hawa jamaa kila kukicha wanaitisha news conference bila kubugudhiwa na mtu, wanamwaga poroja zao, mwisho wa siku wanasema hawana uhuru wa kujieleza! Huu nao ni ujuha!

Ukirudi kwenye vyama vyao, wajumbe na wanachama wao hawaruhusiwi kuhoji mienendo ya viongozi wao hasa wa juu, na wakifanya hivyo ki ndakindaki wanashughurikiwa!


Sasa hawa kina Mbowe na Zitto wanapata wapi ujasiri wa kudai vitu ambavyo wao wenyewe hawawezi kuwapatia wanachama wao? Huu nao ni unafiki kupindukia!

Ngoja niishie hapa, tazameni wenyewe ticktak na faulo zinazochezwa huko kwenye vikundi vya kihuni vinavyojipanga kusaka ruzuku!





 
Nadhani anaetaka tume huru zaidi ni wananchi mkuu sio kina Mbowe.
Mkuu naomba ufafanue zaidi, maana sijasikia wala kuona huku mtaani Wananchi wakijitokeza mtaani kudai tume huru zaidi ya wanasiada kuwarubuni wanachama wao kudai tume huru ambayo kwao wananchi sidhani kama hii iliyopo wanatatizo nayo!
 
ngekuwa ni jambo la hekima kama wangeanza kuonyesha uwepo wa tume huru kwenye chaguzi zao za vyama kabla ya kunyooshea kidole tume yetu ya taifa ya uchaguzi ambayo inao uhuru kwa kiasi kikubwa hata kuliko kwenye vitume vya vyama vyao ambavyo havina uhuru hata kidogo!

Umejenga hoja ifuatayo:

  1. Ndani ya vyama hakuna uhuru
  2. kwenye Tume ya Uchaguzi hakuna uhuru.
  3. Kwa hiyo, kukosekana kwa uhuru katika Tume ni jambo halali.

HAPANA! Makosa mawili hayazalishi haki.

Huwezi kusema kuwa kwa vile ndani ya vyama hakuna uhuru basi kukosekana kwa uhuru katika tume ya Taifa ni jambo halali.

That is primitive naive and nonsensical reasoning....
 
Hili ndio jawabu Mtoa Mada wala usiangaike
Wananchi hawanampango na hiyo tume, msiwasemee! Maaskofu siyo wasemaji wa wananchi...tusichanganyane hapa!
Tume tume ni
Ushahidi huu hapa kutoka mitaani: Utumwa wa Tume Huru ya Uchaguzi

Kuna mifano lukuki!
Maaskofu sio wasemaji wa wananchi! Hatujui ni makubaliano gani waliingia na Mbowe et al, mpaka wakafikia kunajisi kazi ya Mungu! Na wala hawawakirishi maoni ya waumini wao waliowengi!

Hivyo huo sijui walaka au salamu za pasaka haina hadhi ya kutumika kama ushahidi wa wananchi kudai tume! Jaribu kingine mama!
 
Umejenga hoja ifuatayo:

  1. Ndani ya vyama hakuna uhuru
  2. kwenye Tume ya Uchaguzi hakuna uhuru.
  3. Kwa hiyo, kukosekana kwa uhuru katika Tume ni jambo halali.

HAPANA! Makosa mawili hayazalishi haki.

Huwezi kusema kuwa kwa vile ndani ya vyama hakuna uhuru basi kukosekana kwa uhuru katika tume ya Taifa ni jambo halali.

That is primitive naive and nonsensical reasoning....
Mbona unaonekana umesoma ukiwajuu juu umesimama! Kaa chini mama utulie kabla ya kukurupuka na ufupisho wa kizembe hivyo!
Chukulia mfano; wewe mama Amon unamsaliti mmumeo baba Amon na baadae unamkuta mumeo baba Amon na mwanamke mwingine unaanza kuleta songombingo wakati kila mmoja anajua wewe pia huwa unafanya mchezo huo na jamaa flani, sasa utapata wapi ujasiri wa kudai kukosewa na mumeo mama Amon?

Mbowe et al, acheni unafiki, safisheni ndani kwenu kwanza kabla ya kutoka nje!
 
Mkuu naomba ufafanue zaidi, maana sijasikia wala kuona huku mtaani wananchi wakijitokeza mtaani kudai tume huru zaidi ya wanasiada kuwarubuni wanachama wao kudai tume huru ambayo kwao wananchi sidhani kama hii iliyopo wanatatizo nayo!
Kama kupiga picha ni uhujumu uchumi kuidai tume huru si itakua uhaini!!? Aliyekutuma kuandika huu upupu ndiye anasababisha wapiga kura waone hakuna uhuru wa chaguo lao.
 
Kama kupiga picha ni uhujumu uchumi kuidai tume huru si itakua uhaini!!?
Aliyekutuma kuandika huu upupu ndiye anasababisha wapiga kura waone hakuna uhuru wa chaguo lao.
Tume kama ilivyo ni huru kwa std zetu za Kitanzania! Kwa hivyo tume kwenye frequency za Kitanzania utaelewa barabara kuwa hii tume inao uhuru wa kupindukia!
 
Mbona unaonekana umesoma ukiwajujuu umesimama! Kaa chini mama utulie kabla ya kukurupuka na ufupisho wa kizembe hivyo!
Chukulia mfano; wewe mama Amon unamsaliti mmumeo baba Amon na baadae unamkuta mumeo baba Amon na mwanamke mwingine unaanza kuleta songombingo wakati kila mmoja anajua wewe pia huwa unafanya mchezo huo na jamaa flani, sasa utapata wapi ujasiri wa kudai kukosewa na mumeo mama Amon?
Mbowe et al, acheni unafiki, safisheni ndani kwenu kwanza kabla ya kutoka nje!


Mfano batili. Vikwazo vya uhuru wa tume ni tofauti na vikwazo vya uhuru wa chama. Unachanganya maembe na machungwa
 
Tume kama ilivyo ni huru kwa std zetu za kitz! Kwa hivyo tune kwenye frequency za kitz utaelewa barabara kuwa hii tume inao uhuru wa kupindukia!
Iko huru kutangaza mshindi, haiko huru kuonyesha mshindi amepatikanaje.
Rejea majibu ya Damian Lubuva alipobanwa kuhusu matokeo akajibu "mimi natangaza matokeo ninayoletewa"
 
Iko huru kutangaza mshindi, haiko huru kuonyesha mshindi amepatikanaje.
Rejea majibu ya Damian Lubuva alipobanwa kuhusu matokeo akajibu "mimi natangaza matokeo ninayoletewa"
Sasa ulitakaje, kama mawakala wenu wapo kila sehemu wakihakiki kura! Mshindi si anapatikana kwa kupata kura nyingi baada ya kuhesabu kura zote!?
Ulitaka apatikanaje mkuu?
 
Sasa ulitakaje, kama mawakala wenu wapo kila sehemu wakihakiki kura! Mshindi si anapatikana kwa kupata kura nyingi baada ya kuhesabu kura zote!?
Ulitaka apatikanaje mkuu?
Rip Aquilina
 
We mama sikuwezi, ngoja nilale, wewe naona una asili ya kigoma😂😂😂😂!

Huko Kigoma wanasema kuwa ukweli hauwezi kuungua hata kama ukipitishwa kwenye tanuru la moto. Tafuta kina zito wakupe exact quotation, mie najua kifipa. Karibu sumbawanga!
 
Tunataka tume huru ya uchaguzi.
It looks like Common sense is not common to you.
Wewe andika kiswahili tu nitakuelewa! Tume huru kwa muktadha upi!? Mie hii iliyopo ni huru tayari! Unataka waje mabeberu ndio wahesabu kura ndio uamini kuwa tume yetu ya uchaguzi ni huru?

Hivi kwa mawazo yako, mahakama zetu ni huru au haziko huru?
 
Huko Kigoma wanasema kuwa ukweli hauwezi kuungua hata kama ukipitishwa kwenye tanuru la moto. Tafuta kina zito wakupe exact quotation, mie najua kifipa. Karibu sumbawanga!
Muda mwingine siyo ukweli, ni ujinga tu mtu anaung'ang'ania bila kuuacha kwa ubishi uliopitiliza! Sawa, alamski!
 
Back
Top Bottom