Labda mimi sijaelewa lakini nimesikia eti serikali inafikiria kupiga marufuku uuzwaji nje malighafi? nashindwa kuelewa kama kweli serikali inafikiria hili.
Hii itakuwa ni "mistake" kubwa sana na ni maamuzi yasiyo na tija bali kuwaongezea watanzania umasikini. sio swala la mtu kukaa chini na kusema malighafi zikiuzwa nje watanzania wanakosa ajira hivyo jawabu ni kupiga marufuku malighafi kuuzwa nje. nashindwa kusema hii ni fikra ya aina gani maana inaweza kutafsirika nimetukana.
ki msingi serikali inatakiwa kufikiri kibiashara. bidhaa zinazokwenda nje zinafuata soko lililopo nje. kama kuna mnunuzi ananunua kahawa ghafi huwezi kupakia kwenye makopo ukampelekea akanunua. na kama soko tunaloweza kulipata la nje kwa sasa ni la kahawa ghafi basi ukipiga marufuku uuzwaji wa kahawa ghafi nje unaua kilimo cha kahawa kwa wakati huo maana waliokuwa wakinunua kahawa ghafi yenu hawaji kuanzisha kiwanda kwenu bali watahamia kwingine wanakoweza kupata kahawa ghafi.
watanzania tuna matatizo makubwa sana katika kupanga. wataalamu wanaopanga mipango ya maendeleo wanatakiwa kutoa "detailled development plans". tunatumia wahumi wanatoa skeleton za mipango ya maendeleo nadhani ndio chanzo cha haya.
tuzuie sukari kutoka nje basi serikali inakimbilia kupiga marufuku bila kuandaa programu ya uzalishaji wa ndani kutosheleza mahitaji na matokeo yake ni kuleta tatizo la sukari.
sasa bado tuko kwenye mambo yaleyale eti kupiga marufuku uuzwaji malighafi nje? ni kweli ili tupige hatua za maendeleo tunatakiwa kuuza nje bidhaa si malighafi lakini haya ni mabadailiko yanayotakiwa kufanyika kibiashara. tafuta masoko ya kuuza finished goods nje na kuweka mazingira ya watu kuzalishia hapa na kupeleka nje.
lakini itakuwa ni makosa makubwa serikali kupiga marufuku uuzwaji wa malighafi nje ikidhani hiyo ndio njia ya kuhamasisha ujenzi wa viwanda hapa kwa maana biashara haiendi hivyo. ukiwazuia waliokuwa wakinunua kwako watanunua kutoka nchi nyingine na waliokuwa wakiuza huko inawezekana hawana soko la finished goods.
mambo yote yanatakiwa yaendelee sambamba, kujenga viwanda ndani na kuendelea kuuza mazao ghafi nje kwani itatoa soko pana zaidi kwa kilimo. pale tu itakapobainika kuwa ndani kuna kiwanda kinakosa malighafi kutokana na malighafi hizo kupelekwa nje ndio serikali wala isipige marufuku bali icheze na viwango vya kodi kutoa profit margin kwa wanaouza ndani kupata faida zaidi.
Hii itakuwa ni "mistake" kubwa sana na ni maamuzi yasiyo na tija bali kuwaongezea watanzania umasikini. sio swala la mtu kukaa chini na kusema malighafi zikiuzwa nje watanzania wanakosa ajira hivyo jawabu ni kupiga marufuku malighafi kuuzwa nje. nashindwa kusema hii ni fikra ya aina gani maana inaweza kutafsirika nimetukana.
ki msingi serikali inatakiwa kufikiri kibiashara. bidhaa zinazokwenda nje zinafuata soko lililopo nje. kama kuna mnunuzi ananunua kahawa ghafi huwezi kupakia kwenye makopo ukampelekea akanunua. na kama soko tunaloweza kulipata la nje kwa sasa ni la kahawa ghafi basi ukipiga marufuku uuzwaji wa kahawa ghafi nje unaua kilimo cha kahawa kwa wakati huo maana waliokuwa wakinunua kahawa ghafi yenu hawaji kuanzisha kiwanda kwenu bali watahamia kwingine wanakoweza kupata kahawa ghafi.
watanzania tuna matatizo makubwa sana katika kupanga. wataalamu wanaopanga mipango ya maendeleo wanatakiwa kutoa "detailled development plans". tunatumia wahumi wanatoa skeleton za mipango ya maendeleo nadhani ndio chanzo cha haya.
tuzuie sukari kutoka nje basi serikali inakimbilia kupiga marufuku bila kuandaa programu ya uzalishaji wa ndani kutosheleza mahitaji na matokeo yake ni kuleta tatizo la sukari.
sasa bado tuko kwenye mambo yaleyale eti kupiga marufuku uuzwaji malighafi nje? ni kweli ili tupige hatua za maendeleo tunatakiwa kuuza nje bidhaa si malighafi lakini haya ni mabadailiko yanayotakiwa kufanyika kibiashara. tafuta masoko ya kuuza finished goods nje na kuweka mazingira ya watu kuzalishia hapa na kupeleka nje.
lakini itakuwa ni makosa makubwa serikali kupiga marufuku uuzwaji wa malighafi nje ikidhani hiyo ndio njia ya kuhamasisha ujenzi wa viwanda hapa kwa maana biashara haiendi hivyo. ukiwazuia waliokuwa wakinunua kwako watanunua kutoka nchi nyingine na waliokuwa wakiuza huko inawezekana hawana soko la finished goods.
mambo yote yanatakiwa yaendelee sambamba, kujenga viwanda ndani na kuendelea kuuza mazao ghafi nje kwani itatoa soko pana zaidi kwa kilimo. pale tu itakapobainika kuwa ndani kuna kiwanda kinakosa malighafi kutokana na malighafi hizo kupelekwa nje ndio serikali wala isipige marufuku bali icheze na viwango vya kodi kutoa profit margin kwa wanaouza ndani kupata faida zaidi.