Eti ni lini serikari itapiga marufuku Uvaaji wa hovyo hovyo

funza

JF-Expert Member
Sep 5, 2013
7,460
3,137
Kwa siku za karibuni kumeibuka wimbi la vijana mabinti na hata baadhi ya watu wazima kuvaa mavazi ambayo hayaendani na mila na desturi ya mtanzania Vijana wanazidi kuiga kila wanachokiona kwenye Tv lakini kwa Kuwa Serikari haijawakemea wao wanaona ni ujanja kwenda na wakati hata Kama huo wakati hauzingatii maadili ya mtanzania tusipokuwa makini vijana watatembae bila nguo
 
Pigeni marufuku kwanza mitoto yenu inayowavalieni ovyo toka majumbani kwenu. We unaliangalia litoto lako limepiga kimini linaenda kukata mitaa halafu unataka serikali ndo ikamvalishe nguo yenye heshima? Kwa hilo tutakuwa tunaionea serikali bure.
 
Acheni kujifanya mnachangia hoja kwenye mada hii ilihali hamna kitu cha maana mnachosaidia. kusema kweli mleta mada kaniwahi kidogo tu kuitoa hii. tuwe wakweli Tanzania inakoelekea ni kubaya sana nadhani inawezaa kuwa miongoni mwa nchi tatu mbaya barani afrika kwa nchi zinazovaa mavasi yasiyo na heshima. A. KUSINI pia. Hapa kwetu wanawake wanatia kinyaa sawa na mtu aambiwe ale matapishi ya mbwa, yaani wanavaa nguo zinafanana na kondom kila kitu kinaonekana mpaka ukubwa wa kinena chake. sasa hii ni adabu? Ningefurahi kama jukumu hili wangekabidhiwa siasa kali wiki moja tu lingefutika .
 
Mavazi si kigezo cha tabia ya mtu kama wewe ni malaya ni malaya tu.Serikali isidhubutu kuingilia uhuru wa mtu binafsi ilhali inawafuga majangili,mafisadi na wabakaji.Mababu zenu walikuwa wanaficha sehemu za siri tu tena kwa ngozi za wanyama na ------ wazi mbona walikuwa wastaarabu tu?
 
Kwa siku za karibuni kumeibuka wimbi la vijana mabinti na hata baadhi ya watu wazima kuvaa mavazi ambayo hayaendani na mila na desturi ya mtanzania Vijana wanazidi kuiga kila wanachokiona kwenye Tv lakini kwa Kuwa Serikari haijawakemea wao wanaona ni ujanja kwenda na wakati hata Kama huo wakati hauzingatii maadili ya mtanzania tusipokuwa makini vijana watatembae bila nguo

mila na desturi zetu zipi??babu/bibi zetu walikuwa wanavaa vibwaya vifupi matiti nje....nguo tumeletewa na wazungu na waarabu ndio mila zetu hizo.....acheni unafiki mtu avae anavyojisikiia....btw sheria ya nchi hairuhusu mtu kutembea uchi kwanini wasiwachukulie hatua kama wanarembea uchi???unafiki tu unawasumbua..........
 
Funza kuna msemo unasema"MTOTO MLEAVYO NDIVYO AKUAVYO" hivyo jukumu la mavazi linaanzia kwetu sisi wenyewe na wazazi, na familia kwa ujumla.
 
mila na desturi zetu zipi??babu/bibi zetu walikuwa wanavaa vibwaya vifupi matiti nje....nguo tumeletewa na wazungu na waarabu ndio mila zetu hizo.....acheni unafiki mtu avae anavyojisikiia....btw sheria ya nchi hairuhusu mtu kutembea uchi kwanini wasiwachukulie hatua kama wanarembea uchi???unafiki tu unawasumbua..........

wanataka kuleta sharia hao hawana lolote!
 
Uarabuni na znz wanajifunika na mabaibui ila ushenzi uliopo wanajua wenyewe.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Kwa siku za karibuni kumeibuka wimbi la vijana mabinti na hata baadhi ya watu wazima kuvaa mavazi ambayo hayaendani na mila na desturi ya mtanzania Vijana wanazidi kuiga kila wanachokiona kwenye Tv lakini kwa Kuwa Serikari haijawakemea wao wanaona ni ujanja kwenda na wakati hata Kama huo wakati hauzingatii maadili ya mtanzania tusipokuwa makini vijana watatembae bila nguo

ili iweje,itawanunulia watu nguo wazitakazo?we mtu akitembea uch unaumia au inakuhusu nini?maisha ya kupangiana cha kuvaa na jins ya kuvaa yamepitwa na wakati.
 
Kuvaa hovyo ni nini? Binadamu ana utashi, wanyama wengine wanatumia silika.
Mtoa mada usitake kunambia utashi wa binadamu umekwisha sasa tunatumia silika.
 
Hakika mwafrika ni mtumwa wa akili tangu kuumbwa kwa dunia na mapaka mwisho wake!!
Ni mtu huyu anayefikiri kwenda na wakati ni kuiga yote ya mtu mweupe.hivi ni kitu gani tunachoweza kujivunia?uchumi tegemezi,tamaduni tegemezi,siasa tegemezi,akili tegemezi.
Leo hii hata kuvaa kwa heshima na hadhi ni mpaka serikali iingilie kati?iko siku watu wataoa mama zao au kuolewa na baba zao eti ni kwenda na wakati!
Ebu pata picha inakuweje pale unaalikwa kwenda ktk kichen party,sendoff au harusi na bi harusi ni babako mdogo kapata mume-nao wana uhuru wao binafsi waachwe na maisha yao.

KILA KITU KINA MIPAKA YAKE.ULAJI ,UVAAJI,ULALAJI,UFANYAJI KAZI,USOMAJI,IMANI,N.K. VIKIZIDI NI SHIDA KTK JAMII YOYOTE ILE
 
hebu muiache serekali ipumue
kila kitu serikali serikaliiiii kaaaa

maadili na malezi bora yanajengwa na jamii nzima. Hili ni swala mtambuko (cross cutting), wazazi, mashule, nyumba za ibada, vyombo vya habari n.k.. kila mtu kwa nafasi yake akemee yasiyofaa.
 
Pigeni marufuku kwanza mitoto yenu inayowavalieni ovyo toka majumbani kwenu. We unaliangalia litoto lako limepiga kimini linaenda kukata mitaa halafu unataka serikali ndo ikamvalishe nguo yenye heshima? Kwa hilo tutakuwa tunaionea serikali bure.

na wale wasio na wazazi atawarekebisha nani? serikali haichomoki kama katiba inavyoruhusu umri wa kuoa na kuolewa hivohivo kwenye our culture bwana
 
Back
Top Bottom