Lunyungu
JF-Expert Member
- Joined
- Aug 7, 2006
- Messages
- 8,854
- Points
- 1,250
USEMI wa Rais Jakaya Kikwete, alipochukua uongozi wa
nchi, kwamba anakusudia kuendesha uongozi wake
akijenga katika yale yaliyofanywa na mtangulizi wake,
Rais mstaafu Benjamin Mkapa, unaweza kuwa na tafsiri
nyingi sana. Wakati alipotoa msemo huo, (utabakia kuwa
msemo mpaka utekelezaji wa yaliyoahidiwa utakapoanza
kuonekana), wengi waliufasiri chini ya matumaini yao
juu yake na kuuona kama sehemu ya ahadi ya maisha bora
kwa kila Mtanzania.
Wakati huo watu tayari walikuwa wameshayapima kwa
undani yale yaliyofanywa na mtangulizi wake. Hivyo
matumaini ya watu wengi yalikwenda kwenye muendelezo
wa hayo na ndiyo maana watu walimuamini sana Kikwete
alipoahidi kuwaletea kila mmoja wao maisha bora.
Na watu walifahamu nini kuhusu mtangulizi wa Kikwete?
Walikuwa wakimfahamu Mkapa kama mtu ambaye alitumia
muda wake wa uongozi kujenga uchumi wa Tanzania.
Walimfahamu hivyo kutokana na yale yaliyofanyika
ambayo yalikuwa yanaonekana dhahiri. Haikuhitajika
kuwa na darubini au hadubini kuyajua hayo.
Katika kipindi cha miaka kumi ya kuwepo kwake
madarakani, jambo kubwa na la msingi ambalo Mkapa
alilifanya ni kufanikiwa kuutengamanisha uchumi mkuu
(macro-economy) .
Huu ulikuwa ni msingi ambao ulimjengea sifa ndani na
nje ya nchi. Hapa nchini, hivi sasa, sifa hii ya
Mkapa, pamoja na nyingine nyingi, zimeanza kupata
tafsiri nyingine baada ya upande wa pili wa shilingi
ya mambo aliyoyafanya Mkapa akiwa madarakani, kuanza
kuwekwa wazi.
Tumesikia upande mmoja tu unaotoa tuhuma hizo,
hatujasikia Mkapa mwenyewe anasema nini. Na haiyumkini
kuwa tutamsikia akisema. Lakini hata kama tunapaswa
kufanya uamuzi kuhusu tulichokisikia na ushahidi wake,
na kuamua kuwa Mkapa aliyafanya yote anayotuhumiwa
kuyafanya, haitafuta sifa zake, ikiwamo hii ya
kuujenga uchumi mkuu.
Pamoja na mabaya yake yote (na kwa hakika anayo mabaya
kwa sababu yeye ni binadamu tu), sifa hiyo itaendelea
kuwepo na kudumu, hata kama baadhi ya watu
hawatakubaliana na hilo.
Nalichukulia hili la kujenga uchumi mkuu kama msingi
wa yote aliyoyafanya Mkapa, kwa sababu hilo ndilo
jambo ambalo lilikuwa na mwelekeo wa kuleta maisha
bora kwa kila Mtanzania. Na kwa watu wa kawaida, iwapo
watapata mahitaji yao muhimu, mambo mengine wala
hayatawasumbua sana.
Iwapo mtu ana uhakika wa mlo kila siku, anapata uwezo
wa kulipia ada watoto wake, anaweza kuipatia familia
mahitaji yake yote muhimu na mwisho wa siku kuweza
kuweka akiba, hata kama Mkapa aliiba mamilioni
mangapi, hayatamuathiri sana kisaikolojia.
Ila itamuuma sana iwapo maisha yake yatakuwa ya shaka.
Kila mara, anapokuwa na uhitaji wa kitu fulani alafu
akakosa uwezo wa kukipata, mawazo yake yatamfanya
aamini kuwa wizi uliofanywa na Mkapa ndio
unaomsababishia leo hii akikose kitu hicho.
Na ukiangalia alipofikia Mkapa katika kuujenga uchumi,
aliwafikisha Watanzania mahali pa kuleta matumaini. Na
ninarudia kusema kuwa ndiyo maana Kikwete alipoahidi
kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania akijenga katika
yale aliyoyakuta, watu walimuamini sana. Walimuamini
kwa sababu waliyaona hayo ambayo yamejengwa na Kikwete
kuyakuta. Waliona kuwa ilibakia kazi ndogo tu ya
kuufanya uchumi mkubwa uujenge uchumi mdogo
(micro-economy) , ambao kimsingi ndio unaomjaza mtu
mafedha mfukoni.
Na kwa jinsi ilivyokuwa, uwezo wa uchumi mkuu wakati
Mkapa anaondoka madarakani, ulionyesha dhahiri kuwa
kazi ya kuujenga uchumi mdogo ni rahisi kwa kiasi
fulani kwa sababu misingi ilikuwa imeshajengwa.
Mfumuko wa bei ulikuwa umeshuka kutoka tarakimu mbili
na ulikuwa ukizidi kushuka. Hii ilimaanisha kuwa uwezo
wa mtu kununua (purchasing power) ulikuwa ukiongezeka.
Akiba ya fedha za kigeni nchini ilikuwa ya kuridhisha,
iliyotoa uhakika wa uchumi wa nchi kuhimili misukosuko
ya muda mfupi na wa kati iwapo itabidi.
Makusanyo ya kodi yalikuwa yakiongezeka kila mwezi na
kwa hakika kila mwisho wa mwaka, Mamlaka ya Mapato
nchini (TRA) ilikuwa ikitangaza kuvuka malengo
iliyojiwekea.
Hii inamaanisha kuwa nchi ilikuwa na uwezo wa kulipia
zaidi ya sehemu ya bajeti ambayo ilijipangia kulipia
na mapato ya ndani, ndiyo maana kila mwaka asilimia ya
utegemezi katika bajeti ilikuwa ikipungua.
Thamani ya sarafu yetu ilikuwa inajizatiti. Ni kweli
kuwa ilikuwa ikishuka, lakini si kwa kasi ambacho
tunaishuhudia hivi sasa. Hii ilionyesha kuwa mambo
hayakuwa mabaya sana.
Lakini leo hii, takriban miaka miwili baada ya Kikwete
kuingia madarakani tupo wapi? Mfumko wa bei unaelekea
kwenye tarakimu mbili, kule ambako Mkapa alitutoa.
Hapa mtu unaweza kujiuliza ni jinsi gani Kikwete
anajenga uongozi wake katika yale aliyoyafanya Mkapa.
Ushahidi kwamba mfumko wa bei unapanda, unatolewa na
Benki Kuu kila mwezi. Lakini hata katika maisha ya
kawaida, hili linaonekana. Bei za bidhaa zimepaa kiasi
kwamba watu wameanza kujiuliza maswali mengi
yanayokosa majibu.
Mtafaruku kuhusu bei ya saruji wala bado haujatulia.
Bei za vyakula zinabadilika kwa kasi kuliko kinyonga
anavyoweza kubadili rangi zake. Kibaya zaidi ni kuwa
mabadiliko hayo yanahusisha si tu kupanda, bali
kupanda kwa tofauti kubwa mno. Leo si ajabu ukakuta
bidhaa ikiwa imepanda bei mara mbili ya uliyoiona
jana.
Lakini serikali imekuwa haiishiwi na visingizio na
kutoa matumaini kwa kutumia takwimu. Tulitarajia kuwa
hali ingekuwa mbaya mwaka jana baada ya msukosuko
uliotokana na kukosekana kwa umeme. Lakini wakati wa
tatizo hilo, serikali yenyewe iliwatoa Watanzania
wasiwasi na kuwaeleza kuwa kila kitu kilikuwa
kimedhibitiwa ipasavyo.
Na kama kawadia yao wakatumia takwimu, zilizoonyesha
kupanda kwa makusanyo ya kodi ya kila mwezi
kuhalalisha kauli yao kuwa kila kitu kipo sawa.
Hamkujua kuwa kutoyumba kwa uchumi wa nchi kulitokana
na misingi ya kuweka akiba ya kutosha fedha za kigeni
kulikofanywa na Mkapa.
Leo hii uchumi wa nchi upo matatizoni. Hakuna kiongozi
wa serikali au chama anayetaka kukiri hili hadharani.
Wengi wanauchukulia uchumi kama sehemu ya siasa
wanazopiga majukwaani. Na ndiyo maana tunaumia na
tutaendelea kuumia iwapo viongozi wetu wataacha kuuona
uchumi kama siasa.
Ndio wanauona uchumi kama siasa. Hii inatokana na
jinsi wanavyotukoga. Haiwezekani mtu apange safari,
akiwa ametinga magwanda ya kijani kibichi na nyeusi,
akitumia gari la serikali, alafu anasema kuwa
anaelezea uzuri wa bajeti huku hotuba yake ikianza na
salamu za kidumu chama.
Uchumi haujui chama, unajua mipangilio na mambo
kimahesabu. Ni utaalamu wa kimahesabu, si ujuzi wa
kupiga domo jukwaani. Wanaweza kuwa mabingwa wa
kuelezea uzuri wa bajeti kwa lugha tamu,
zinazonakshiwa na vikorombwezo na vichekesho, lakini
kama hesabu za kiuchumi hazijakaa sawa, kesho yake
itajionyesha wazi kwa mfumko wa bei kupanda.
Hayo maneno matamu hayawezi kuifanya thamani ya
shilingi isishuke. Thamani ya shilingi itaendelea
kushuka na tofauti kati ya riba ya kuweka na kukopa
kupanuka iwapo tutaishia kutoa maneno matamu jukwaani
bila kuchukua hatua za kuidhibiti hali hiyo.
Iwapo watafanya mambo yanayotakiwa kudhibiti viashiria
vya uchumi, wala hawatahitaji wajuzi wa kutunga
mashairi ili kuwashawishi watu. Kila kitu kitaonekana
dhahiri; hali ya mambo itabadilika, maisha yatazidi
kuwa bora na hapo hata wasipowaambia Watanzania
lolote, watafahamu kwa kweli serikali yao ipo kazini.
Miaka miwili iliyopita, asilimia 80 ya Watanzania
waliichagua serikali hii ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
iliyopo madarakani. Huu ni ushindi ambao hadi hii leo
bado umewalevya baadhi ya watu ndani ya CCM, kiasi
kwamba hawaachi kuutajataja kana kwamba shida za
Watanzania zitamalizwa na asilimia 80.
Hivi hawa viongozi wameshawahi kujiuliza kwa nini hao
asilimia 80 waliowachagua juzi tu, leo wanaanza
kuwazomea majukwaani? Yanatokea haya mara nyingi sana,
na yanapaswa kuwa somo kwa viongozi wetu.
Lakini wao inaelekea wameamua wasiyaone. Inatisha sana
kuwa wanaozomewa ni wao, lakini wakitoka hapo
wanakanusha kuwa hawakuzomewa! Hivi ni kuwa wamelewa
sana madaraka kiasi kwamba kelele za kuzomewa wao
wanaziona kama za kushangiliwa? Siamini.
Kuzomea huku ni aina fulani ya wananchi kutoa hasira
zao. Na namna yao ya kueleza manunguniko yao. Lengo
lao ni kutaka kilio chao kisikiwe na viongozi. Lakini
viongozi wasiposikia kuzomea huko, na hata kufikia
hatua ya kukanusha kuwa hawakuzomewa, wananchi watajua
kuwa salamu zao hazijafika.
Watatafuta njia na mbinu nyingine ya kufikisha kilio
chao. Na huu ndio utabiri ambao CCM siku zote imekuwa
wakiambiwa lakini hawataki kuamini. Kwamba ipo siku,
wananchi ambao wanajihisi kudharauliwa kwa kiasi cha
juu na viongozi wao, ambao wakiwafikishia ujumbe na
kilio chao hawakisikii, wataamua kutafuta njia na
mbinu nyingine ya kufikisha kilio chao. Watafanya
nini? Ni vigumu kujua sasa.
Lakini ni dhahiri kuwa chaguo la watakachokifanya
litakuwa si kuwakumbatia viongozi wasiowasikia.
nchi, kwamba anakusudia kuendesha uongozi wake
akijenga katika yale yaliyofanywa na mtangulizi wake,
Rais mstaafu Benjamin Mkapa, unaweza kuwa na tafsiri
nyingi sana. Wakati alipotoa msemo huo, (utabakia kuwa
msemo mpaka utekelezaji wa yaliyoahidiwa utakapoanza
kuonekana), wengi waliufasiri chini ya matumaini yao
juu yake na kuuona kama sehemu ya ahadi ya maisha bora
kwa kila Mtanzania.
Wakati huo watu tayari walikuwa wameshayapima kwa
undani yale yaliyofanywa na mtangulizi wake. Hivyo
matumaini ya watu wengi yalikwenda kwenye muendelezo
wa hayo na ndiyo maana watu walimuamini sana Kikwete
alipoahidi kuwaletea kila mmoja wao maisha bora.
Na watu walifahamu nini kuhusu mtangulizi wa Kikwete?
Walikuwa wakimfahamu Mkapa kama mtu ambaye alitumia
muda wake wa uongozi kujenga uchumi wa Tanzania.
Walimfahamu hivyo kutokana na yale yaliyofanyika
ambayo yalikuwa yanaonekana dhahiri. Haikuhitajika
kuwa na darubini au hadubini kuyajua hayo.
Katika kipindi cha miaka kumi ya kuwepo kwake
madarakani, jambo kubwa na la msingi ambalo Mkapa
alilifanya ni kufanikiwa kuutengamanisha uchumi mkuu
(macro-economy) .
Huu ulikuwa ni msingi ambao ulimjengea sifa ndani na
nje ya nchi. Hapa nchini, hivi sasa, sifa hii ya
Mkapa, pamoja na nyingine nyingi, zimeanza kupata
tafsiri nyingine baada ya upande wa pili wa shilingi
ya mambo aliyoyafanya Mkapa akiwa madarakani, kuanza
kuwekwa wazi.
Tumesikia upande mmoja tu unaotoa tuhuma hizo,
hatujasikia Mkapa mwenyewe anasema nini. Na haiyumkini
kuwa tutamsikia akisema. Lakini hata kama tunapaswa
kufanya uamuzi kuhusu tulichokisikia na ushahidi wake,
na kuamua kuwa Mkapa aliyafanya yote anayotuhumiwa
kuyafanya, haitafuta sifa zake, ikiwamo hii ya
kuujenga uchumi mkuu.
Pamoja na mabaya yake yote (na kwa hakika anayo mabaya
kwa sababu yeye ni binadamu tu), sifa hiyo itaendelea
kuwepo na kudumu, hata kama baadhi ya watu
hawatakubaliana na hilo.
Nalichukulia hili la kujenga uchumi mkuu kama msingi
wa yote aliyoyafanya Mkapa, kwa sababu hilo ndilo
jambo ambalo lilikuwa na mwelekeo wa kuleta maisha
bora kwa kila Mtanzania. Na kwa watu wa kawaida, iwapo
watapata mahitaji yao muhimu, mambo mengine wala
hayatawasumbua sana.
Iwapo mtu ana uhakika wa mlo kila siku, anapata uwezo
wa kulipia ada watoto wake, anaweza kuipatia familia
mahitaji yake yote muhimu na mwisho wa siku kuweza
kuweka akiba, hata kama Mkapa aliiba mamilioni
mangapi, hayatamuathiri sana kisaikolojia.
Ila itamuuma sana iwapo maisha yake yatakuwa ya shaka.
Kila mara, anapokuwa na uhitaji wa kitu fulani alafu
akakosa uwezo wa kukipata, mawazo yake yatamfanya
aamini kuwa wizi uliofanywa na Mkapa ndio
unaomsababishia leo hii akikose kitu hicho.
Na ukiangalia alipofikia Mkapa katika kuujenga uchumi,
aliwafikisha Watanzania mahali pa kuleta matumaini. Na
ninarudia kusema kuwa ndiyo maana Kikwete alipoahidi
kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania akijenga katika
yale aliyoyakuta, watu walimuamini sana. Walimuamini
kwa sababu waliyaona hayo ambayo yamejengwa na Kikwete
kuyakuta. Waliona kuwa ilibakia kazi ndogo tu ya
kuufanya uchumi mkubwa uujenge uchumi mdogo
(micro-economy) , ambao kimsingi ndio unaomjaza mtu
mafedha mfukoni.
Na kwa jinsi ilivyokuwa, uwezo wa uchumi mkuu wakati
Mkapa anaondoka madarakani, ulionyesha dhahiri kuwa
kazi ya kuujenga uchumi mdogo ni rahisi kwa kiasi
fulani kwa sababu misingi ilikuwa imeshajengwa.
Mfumuko wa bei ulikuwa umeshuka kutoka tarakimu mbili
na ulikuwa ukizidi kushuka. Hii ilimaanisha kuwa uwezo
wa mtu kununua (purchasing power) ulikuwa ukiongezeka.
Akiba ya fedha za kigeni nchini ilikuwa ya kuridhisha,
iliyotoa uhakika wa uchumi wa nchi kuhimili misukosuko
ya muda mfupi na wa kati iwapo itabidi.
Makusanyo ya kodi yalikuwa yakiongezeka kila mwezi na
kwa hakika kila mwisho wa mwaka, Mamlaka ya Mapato
nchini (TRA) ilikuwa ikitangaza kuvuka malengo
iliyojiwekea.
Hii inamaanisha kuwa nchi ilikuwa na uwezo wa kulipia
zaidi ya sehemu ya bajeti ambayo ilijipangia kulipia
na mapato ya ndani, ndiyo maana kila mwaka asilimia ya
utegemezi katika bajeti ilikuwa ikipungua.
Thamani ya sarafu yetu ilikuwa inajizatiti. Ni kweli
kuwa ilikuwa ikishuka, lakini si kwa kasi ambacho
tunaishuhudia hivi sasa. Hii ilionyesha kuwa mambo
hayakuwa mabaya sana.
Lakini leo hii, takriban miaka miwili baada ya Kikwete
kuingia madarakani tupo wapi? Mfumko wa bei unaelekea
kwenye tarakimu mbili, kule ambako Mkapa alitutoa.
Hapa mtu unaweza kujiuliza ni jinsi gani Kikwete
anajenga uongozi wake katika yale aliyoyafanya Mkapa.
Ushahidi kwamba mfumko wa bei unapanda, unatolewa na
Benki Kuu kila mwezi. Lakini hata katika maisha ya
kawaida, hili linaonekana. Bei za bidhaa zimepaa kiasi
kwamba watu wameanza kujiuliza maswali mengi
yanayokosa majibu.
Mtafaruku kuhusu bei ya saruji wala bado haujatulia.
Bei za vyakula zinabadilika kwa kasi kuliko kinyonga
anavyoweza kubadili rangi zake. Kibaya zaidi ni kuwa
mabadiliko hayo yanahusisha si tu kupanda, bali
kupanda kwa tofauti kubwa mno. Leo si ajabu ukakuta
bidhaa ikiwa imepanda bei mara mbili ya uliyoiona
jana.
Lakini serikali imekuwa haiishiwi na visingizio na
kutoa matumaini kwa kutumia takwimu. Tulitarajia kuwa
hali ingekuwa mbaya mwaka jana baada ya msukosuko
uliotokana na kukosekana kwa umeme. Lakini wakati wa
tatizo hilo, serikali yenyewe iliwatoa Watanzania
wasiwasi na kuwaeleza kuwa kila kitu kilikuwa
kimedhibitiwa ipasavyo.
Na kama kawadia yao wakatumia takwimu, zilizoonyesha
kupanda kwa makusanyo ya kodi ya kila mwezi
kuhalalisha kauli yao kuwa kila kitu kipo sawa.
Hamkujua kuwa kutoyumba kwa uchumi wa nchi kulitokana
na misingi ya kuweka akiba ya kutosha fedha za kigeni
kulikofanywa na Mkapa.
Leo hii uchumi wa nchi upo matatizoni. Hakuna kiongozi
wa serikali au chama anayetaka kukiri hili hadharani.
Wengi wanauchukulia uchumi kama sehemu ya siasa
wanazopiga majukwaani. Na ndiyo maana tunaumia na
tutaendelea kuumia iwapo viongozi wetu wataacha kuuona
uchumi kama siasa.
Ndio wanauona uchumi kama siasa. Hii inatokana na
jinsi wanavyotukoga. Haiwezekani mtu apange safari,
akiwa ametinga magwanda ya kijani kibichi na nyeusi,
akitumia gari la serikali, alafu anasema kuwa
anaelezea uzuri wa bajeti huku hotuba yake ikianza na
salamu za kidumu chama.
Uchumi haujui chama, unajua mipangilio na mambo
kimahesabu. Ni utaalamu wa kimahesabu, si ujuzi wa
kupiga domo jukwaani. Wanaweza kuwa mabingwa wa
kuelezea uzuri wa bajeti kwa lugha tamu,
zinazonakshiwa na vikorombwezo na vichekesho, lakini
kama hesabu za kiuchumi hazijakaa sawa, kesho yake
itajionyesha wazi kwa mfumko wa bei kupanda.
Hayo maneno matamu hayawezi kuifanya thamani ya
shilingi isishuke. Thamani ya shilingi itaendelea
kushuka na tofauti kati ya riba ya kuweka na kukopa
kupanuka iwapo tutaishia kutoa maneno matamu jukwaani
bila kuchukua hatua za kuidhibiti hali hiyo.
Iwapo watafanya mambo yanayotakiwa kudhibiti viashiria
vya uchumi, wala hawatahitaji wajuzi wa kutunga
mashairi ili kuwashawishi watu. Kila kitu kitaonekana
dhahiri; hali ya mambo itabadilika, maisha yatazidi
kuwa bora na hapo hata wasipowaambia Watanzania
lolote, watafahamu kwa kweli serikali yao ipo kazini.
Miaka miwili iliyopita, asilimia 80 ya Watanzania
waliichagua serikali hii ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
iliyopo madarakani. Huu ni ushindi ambao hadi hii leo
bado umewalevya baadhi ya watu ndani ya CCM, kiasi
kwamba hawaachi kuutajataja kana kwamba shida za
Watanzania zitamalizwa na asilimia 80.
Hivi hawa viongozi wameshawahi kujiuliza kwa nini hao
asilimia 80 waliowachagua juzi tu, leo wanaanza
kuwazomea majukwaani? Yanatokea haya mara nyingi sana,
na yanapaswa kuwa somo kwa viongozi wetu.
Lakini wao inaelekea wameamua wasiyaone. Inatisha sana
kuwa wanaozomewa ni wao, lakini wakitoka hapo
wanakanusha kuwa hawakuzomewa! Hivi ni kuwa wamelewa
sana madaraka kiasi kwamba kelele za kuzomewa wao
wanaziona kama za kushangiliwa? Siamini.
Kuzomea huku ni aina fulani ya wananchi kutoa hasira
zao. Na namna yao ya kueleza manunguniko yao. Lengo
lao ni kutaka kilio chao kisikiwe na viongozi. Lakini
viongozi wasiposikia kuzomea huko, na hata kufikia
hatua ya kukanusha kuwa hawakuzomewa, wananchi watajua
kuwa salamu zao hazijafika.
Watatafuta njia na mbinu nyingine ya kufikisha kilio
chao. Na huu ndio utabiri ambao CCM siku zote imekuwa
wakiambiwa lakini hawataki kuamini. Kwamba ipo siku,
wananchi ambao wanajihisi kudharauliwa kwa kiasi cha
juu na viongozi wao, ambao wakiwafikishia ujumbe na
kilio chao hawakisikii, wataamua kutafuta njia na
mbinu nyingine ya kufikisha kilio chao. Watafanya
nini? Ni vigumu kujua sasa.
Lakini ni dhahiri kuwa chaguo la watakachokifanya
litakuwa si kuwakumbatia viongozi wasiowasikia.