Eti hatujui... kipimo gani kinatumika?

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Jana nimesoma makala ya Freddy Macha kwenye gazeti la Mwananchi iliyokuwa inaongelea mijadala inayoendelea kwenye mitandao mbali mbali ikieleza kuwa wanaume wa Kitanzania (na labda Waafrika wote) hatujui mahaba (romance)!

Nimeguswa sana na makala hiyo. Si kwa sababu napingana na hoja za hao wanaosema hivyo, bali nina wasi wasi kwamba vigezo vinavyotumiwa vinaweza kuwa siyo sahihi.

Inawezekana hii mada ilishajadiliwa hapa pia, ila naomba tu kupata maoni ya wadau wa jukwaa letu hili tukukufu kuhusiana na issue hii.

1. Ni kweli wanaume wa Kitanzania hawajui mahaba?

2. Kama hawajui, ni kosa lao peke yao au na wenzi wao (wanawake)?

3. Na vigezo gani vinatumiwa ku-judge kama mtu anajua mahaba au la?

Naomba maoni yenu!!

Babu DC
 
but nionavyo mimi ni kuwa tumegawanyika

wapo ambao hawajui au tuseme hawana mahaba ya tamthilia za akina alejandro
,hasa wa mikoani na vijijini......na hapa namaanisha romance...na sio love.....

dunia imebadilika mno.....juzi hapa kuna thread ilianzishwa na afrodenzi kuhusu siku ya ku propose

nikajiuliza....am i old fashioned guy or what?

kwangu mimi ku kneel down na ku propose imekaa ki hollywood zaidi...
but wadada wa sasa wanataka hizo pia....go figure....
 
but nionavyo mimi ni kuwa tumegawanyika

wapo ambao hawajui au tuseme hawana mahaba ya tamthilia za akina alejandro
,hasa wa mikoani na vijijini......na hapa namaanisha romance...na sio love.....

dunia imebadilika mno.....juzi hapa kuna thread ilianzishwa na afrodenzi kuhusu siku ya ku propose

nikajiuliza....am i old fashioned guy or what?

kwangu mimi ku kneel down na ku propose imekaa ki hollywood zaidi...
but wadada wa sasa wanataka hizo pia....go figure....
Tatizo ukilinganisha sana ndio unajikuta unaona nani ni best, mie pia
kuna mambo naona kabisa watu ni ya kuiga sana kama hilo la
kupiga magoti na kuomba mkono wa ndoa, ile ni mila yao, wanafata
na sie bila hata kuuliza ina maana gani utakuta jibaba la kibongo
eti nae anaiga hiyo, mie kwanza ukipiga tu goti natoka mbio, nitaona
aibu hata sielewi

Wanaume wetu wa kibongo wanajua sana mapenzi in their own way
kazi kwao wanaolinganisha na kina tom cruise
 
Tatizo ukilinganisha sana ndio unajikuta unaona nani ni best, mie pia
kuna mambo naona kabisa watu ni ya kuiga sana kama hilo la
kupiga magoti na kuomba mkono wa ndoa, ile ni mila yao, wanafata
na sie bila hata kuuliza ina maana gani utakuta jibaba la kibongo
eti nae anaiga hiyo, mie kwanza ukipiga tu goti natoka mbio, nitaona
aibu hata sielewi

Wanaume wetu wa kibongo wanajua sana mapenzi in their own way
kazi kwao wanaolinganisha na kina tom cruise


we mtoto umeandika pointi hapa
au ndo unanitega aisee lol
 
but nionavyo mimi ni kuwa tumegawanyika

wapo ambao hawajui au tuseme hawana mahaba ya tamthilia za akina alejandro
,hasa wa mikoani na vijijini......na hapa namaanisha romance...na sio love.....

dunia imebadilika mno.....juzi hapa kuna thread ilianzishwa na afrodenzi kuhusu siku ya ku propose

nikajiuliza....am i old fashioned guy or what?

kwangu mimi ku kneel down na ku propose imekaa ki hollywood zaidi...
but wadada wa sasa wanataka hizo pia....go figure....

Kweli mkuu,

Baada ya kusoma hiyo makala ya Macha, nilitamani kumuuliza bibi yangu (about 90yrs old) hilo swali. Bahati mbaya niko mbali naye...Whatever the case,....nadhani bado tuna safari ndefu ya kuji-define kama Watanzania wa karne hii!!
 
Tatizo ukilinganisha sana ndio unajikuta unaona nani ni best, mie pia
kuna mambo naona kabisa watu ni ya kuiga sana kama hilo la
kupiga magoti na kuomba mkono wa ndoa, ile ni mila yao, wanafata
na sie bila hata kuuliza ina maana gani utakuta jibaba la kibongo
eti nae anaiga hiyo, mie kwanza ukipiga tu goti natoka mbio, nitaona
aibu hata sielewi

Wanaume wetu wa kibongo wanajua sana mapenzi in their own way
kazi kwao wanaolinganisha na kina tom cruise

BB, umegonga home kabisa....

Hivi kweli mtu ukilikuta jitu kama Babu DC limepiga magoti linaomba uchumba wa mke wa 4 au liko pale kwenye viwanja vya Posta ya zamani linampiga piga busu mke wake utaliewa kweli???

May be kama alivyosema Boss, tunasumbuliwa na hang-over ya maisya yetu ya 1947!!
 
BB, umegonga home kabisa....

Hivi kweli mtu ukilikuta jitu kama Babu DC limepiga magoti linaomba uchumba wa mke wa 4 au liko pale kwenye viwanja vya Posta ya zamani linampiga piga busu mke wake utaliewa kweli???

May be kama alivyosema Boss, tunasumbuliwa na hang-over ya maisya yetu ya 1947!!

au unaongea kwa sauti laaini huku mdomoni unatafuna ncha ya miwani
na mrembo anakutazama kwa tabasamu hivi lol
 
au unaongea kwa sauti laaini huku mdomoni unatafuna ncha ya miwani
na mrembo anakutazama kwa tabasamu hivi lol

Ukifikia hapo itakuwa kasheshe...

Enzi zetu kijana wa namna hiyo alikuwa automatically anahesabiwa kuwa ni fungu la kukosa! Tulizoea kuwaona wachumba wakitafuna kucha au kuandika kwenye udongo maandishi ambayo hayasomeki.

Kumbe siku hizi vijana ndio wanafanya hivyo........???

Ngoja niishie hapo kwani ninaweza kutoa machozi nikipiga picha na kuwaona wajukuu zangu (boys) wanafanya upuuzi kama huo!!
 
Ukifikia hapo itakuwa kasheshe...

Enzi zetu kijana wa namna hiyo alikuwa automatically anahesabiwa kuwa ni fungu la kukosa! Tulizoea kuwaona wachumba wakitafuna kucha au kuandika kwenye udongo maandishi ambayo hayasomeki.

Kumbe siku hizi vijana ndio wanafanya hivyo........???

Ngoja niishie hapo kwani ninaweza kutoa machozi nikipiga picha na kuwaona wajukuu zangu (boys) wanafanya upuuzi kama huo!!

mkuu dunia imebadilika mno
ni kweli yapo mambo inabidi twende nayo but mengine mimi naona ni upuuzi...

ukitazama relationship za watoto wa shule wa siku hizi ni tamthilia tupu....

unakuta wengine wanatoka familia duni mno but wanaangushiana birthday party
za nguvu na kumbi zinakodishwa hadi unashangaa,wakati wazazi wao home wanakopa
mchele kwa wapemba madukani....yote kuiga wanachoona kwenye tv.....

its complicated......mfano sasa wadada kkama huna culture ya kumpigia simu kila siku
wana tafsiri humpendi...sasa jaribu kujiuliza hizi simu zimeanza lini?????/
 
Nilibahatika kuuona huu mjadala kupitia wanabidii.........it was hot. Watu wanajibu hoja kwa references jamani ah. kuna points zilizungumziwa kule nikabaki kumwomba mwenzi wangu abakie wa kibantu kama alivyo.
 
Nilibahatika kuuona huu mjadala kupitia wanabidii.........it was hot. Watu wanajibu hoja kwa references jamani ah. kuna points zilizungumziwa kule nikabaki kumwomba mwenzi wangu abakie wa kibantu kama alivyo.

Tupe basi uhondo kidogo ndugu yangu,

Hiki kizazi inawezekana kimeshatuacha mbali sana!
 
mjone zilete hizo pointi hapa...tujadili

wadada siku hizi mnataka wanaume wa kuwanunulia maua.....

hiyo ndo romantic kwenu....

wakati sisi tumefundishwa na mababu na mababu kuwa romantic ni kubeba kikapu
na kupitia ferry na kukijaza samaki wa kutosha halafu huyo unaelekea kwa mwenzio na kiroba cha mchele pembeni....lol
 
mjone zilete hizo pointi hapa...tujadili

wadada siku hizi mnataka wanaume wa kuwanunulia maua.....

hiyo ndo romantic kwenu....

wakati sisi tumefundishwa na mababu na mababu kuwa romantic ni kubeba kikapu
na kupitia ferry na kukijaza samaki wa kutosha halafu huyo unaelekea kwa mwenzio na kiroba cha mchele pembeni....lol
the boss naona una utani na wapemba wewe, hivi mkurya unaweza kumbebesha kikapu akakubali,zaidi ya kauli ya rara chini nikurenge mama wankuru,mura!
 
Tatizo ni mtazamo.

Kila mtu ana mtazamo wake wa nini haswa ni romantic na mwanamke/mwanaume wa aina gani ni romantic. Kuna mtu mumewe kumpikia ni romantic na mwingine anaona kwa kufanya vile mumewe anajishusha. Kuna mwanaume mkewe kumpigia simu three times a day ni romantic na mwingine anaona ni pure usumbufu. Kwahiyo kwa vyovyote vile...kwa kutumia kipimo chochote kile hamna mtu ambae atakubalika na kila mtu (watu wenye background na mategemeo tofauti ) kwamba yeye ni romantic universally.

Kujibu maswali yako
1. Wanaume wa Tanzania ni romantic. Just not to everybody.
2.Kama sio kwa baadhi ya watu sioni kwanini kosa liwe la yeyote yule. Ni vizuri kila mtu akawa vile alivyo...wanaopenda his kind of romantice watakuwepo na ikitokea bahati nzuri akawa na mahusiano na mmoja wao hakutakua na malalamiko kati yao.Akikutana na ambae ni tofauti basi ni jukumu la huyo mwenza kumjulisha mwenzake kwamba ningependa kitu fulani na fulani ili nifurahi na iwapo hicho kitu kiko ndani ya uwezo na matakwa ya mwanaume basi kitafanyika.
3. Vigezo vinaofautiana kati ya mtu na mtu/sehemu na sehemu.Hamna kipimo ambacho ni universal amabcho majibu yake kila mtu atakubaliana nayo.
 
Kwani na ww unategwa?hapo naelezea ukweli, kwa mfano eti kuna rafiki yangu kaachana na bf wake, kisa anaona shida anapoongea kiswahili wakati wa majambo, nikamshangaa sana, mie napenda full kiswahili,wasichana tunatofautiana
kwa hiyo wakati wa ku do kingereza kwake ndio mshiko? huyo shost wako mjinga sana inaelekea ni tamthilia hizi za akina marichui na second chance zimemharibu,lol! mpe pole zake manake siku akikutana na ambaye mizuka ikimpanda anaomgea kilugha sijui atasema ana mashetani.
 
BB, umegonga home kabisa....

Hivi kweli mtu ukilikuta jitu kama Babu DC limepiga magoti linaomba uchumba wa mke wa 4 au liko pale kwenye viwanja vya Posta ya zamani linampiga piga busu mke wake utaliewa kweli???

May be kama alivyosema Boss, tunasumbuliwa na hang-over ya maisya yetu ya 1947!!
Watu wanapenda mapenzi ya kuigiza sana
 
Tatizo ni mtazamo.

Kila mtu ana mtazamo wake wa nini haswa ni romantic na mwanamke/mwanaume wa aina gani ni romantic. Kuna mtu mumewe kumpikia ni romantic na mwingine anaona kwa kufanya vile mumewe anajishusha. Kuna mwanaume mkewe kumpigia simu three times a day ni romantic na mwingine anaona ni pure usumbufu. Kwahiyo kwa vyovyote vile...kwa kutumia kipimo chochote kile hamna mtu ambae atakubalika na kila mtu (watu wenye background na mategemeo tofauti ) kwamba yeye ni romantic universally.

Kujibu maswali yako
1. Wanaume wa Tanzania ni romantic. Just not to everybody.
2.Kama sio kwa baadhi ya watu sioni kwanini kosa liwe la yeyote yule. Ni vizuri kila mtu akawa vile alivyo...wanaopenda his kind of romantice watakuwepo na ikitokea bahati nzuri akawa na mahusiano na mmoja wao hakutakua na malalamiko kati yao.Akikutana na ambae ni tofauti basi ni jukumu la huyo mwenza kumjulisha mwenzake kwamba ningependa kitu fulani na fulani ili nifurahi na iwapo hicho kitu kiko ndani ya uwezo na matakwa ya mwanaume basi kitafanyika.
3. Vigezo vinaofautiana kati ya mtu na mtu/sehemu na sehemu.Hamna kipimo ambacho ni universal amabcho majibu yake kila mtu atakubaliana nacho.
hiyo point ya tatu imesimama sana lizy for sure hamna kipimo universal na sijui kingekuwepo SI unit yake sijui ingeitwaje
 
Back
Top Bottom