Eti hakuna dawa ya mapenzi! hii ilikua ni kitu gani?

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
Ni rafiki yangu wa karibu sana ambaye tulikua siku zote tuko pamoja katika mihangaiko na harakati ya kuisaka shilingi na kuijenga nchi. Jamaa alimpenda sana mkewe mama Irene(sio jina lake halisi). Hamuwezi mkaongea mazungumzo ya nusu saa bila kumtaja, tena ni kwa mazuri tu ya kumsifia. Wala haikua ndoa mpya wakati huo kusema labda ni extended honeymoon, maana walikua tayari wana watoto wawili na mmoja alikua amemaliza darasa la saba

Siku zote alikua akisisitiza hakuna mwanamke wa nje anaeweza kumzuzua alale nje hata kwa usiku mmoja, sembuse kuitelekeza familia yake. Alikua akiwashangaa na kuwadharau sana wanaume anaosikia wanazembea kutimiza majukumu yao kwenye familia kwa kuendekeza penzi la nyumba ndogo. Yeye pia hakua limbukeni wa mapenzi, alikua kiwembe hasaa na alikua amewapangishia wanawake wawili nyumba katika maeneo tofauti ya hapa Dar(Asante Mkapa, asante Kikwete wakati huo iliwezekana),Na saa moja jioni mara nyingi alikua kasharudi kwake

Mkewe alikuja kuugua akapata stroke! Jamaa alikua anamhudumia mkewe kwa upendo wa ajabu sana. Pamoja na kua na mfanyakazi na mtoto mkubwa tu lakini chakula cha mkewe alikua anapika mwenyewe na hata kumfulia na alizunguuka nae sana kwenye hospitali nyingi nchini kwa matibabu ingawa hali yake haikua inatengemaa, kwa miaka miwili mfululizo alimtumikia with passion na alikua anaona fahari sana kutuhadithia anavojitahidi kumfanya mkewe mgonjwa awe na furaha

Ilianza kama utani. Aliachana na mmoja ya wale wanawake aliowapangishia baada ya dem kutaka kumuendesha mshikaji, ingawa sababu nyingine mwanamke alikua anataka kuolewa na raia wa kigeni. Baada ya hapo akapata dem mwingine wa kawaida tu, bint wa Kinyiramba/Mnyaturu sikumbuki exact kabila. Na yeye akampangishia nyumba. Mienendo yake kidooogo ikaanza kubadilika maana muda mwingi alikua anautumia akiwa na huyu binti hadi sehemu ya kazi!

Siku akasafiri kwenda Singida na huyo dada. Alipofika akanipigia simu akanambia 'Kaka nimekuja huku Singida huyu mtoto bana tuki sex hasikii raha, yaani anakua hayuko wet kabisaa hata nimuandae vipi, sasa kanileta kwa mtaalamu wa jadi tumepewa dawa toka juzi, naona leo tume kwichkwich imekua bomba sana, dem kasema hajawahi ku enjoy sex kama leo. Huko kwa mganga wakapewa na mbuzi jamaa aje kumfuga nyumbani kwake anapoishi yeye na mkewe!

Siku chache baada ya kurudi napigiwa simu na shangazi yake niende haraka nyumbani kwa rafiki yangu kuna tatizo, tukakutana hapo kwake mimi, brother wake wa tumbo moja na huyo shangazi yake. Tatizo jamaa anataka mkewe yule mgonjwa aliekua anampenda sana sana arudi nyumbani kijijini akajiuguze huko mpaka apone! Hapo ni baada ya mamam huyo kushtukia kua mumewe ana mahusiano na mwanamke mwingine na alikua anajisahau sasa anaongea nae mbele ya mkewe, na mama Irine alipokua anamuuliza ndio jamaa akaja juu na kumtaka aende kwao.
Tulifanikiwa kumzuia jamaa asimuondoe mkewe hapo home lakini baada ya pale akakata mguu kabisa kwenda kwake na huduma akawa hapeleki akahamia kabisaa kwenye nyumba aliyompangishia Mnyiramba/Mnyaturu! Kuna saa anakwambia 'Kaka mwanamke mzuri yule! unamuuliza nani? Anasema Anna(sio jina hali la Msingida). dah, nikaona ama kweli rafiki yangu kashikika na kakwama

Siku moja mama Irine ananipigia simu ananambia 'Shemeji naomba msinirudishe kijijini nitaenda kufa tu jamani, hakuna huduma kule, mwambie mwenzio nimekubali amlete tu huyo Anna akae nae hapa nyumbani mimi nitakaa banda la uani tu yule mbuzi watoto wamjengee banda ila msirudishe nyumbani shem'. Sikuweza maliza kuisikiliza simu ile machozi yalinidondoka. It was so emotional! Bahati mbaya hatukuweza kufanya lolote, Mama Irine alirushwa kijijini kwa kuchangiwa hela maana mumewe hakukanyaga tena pale kwake na baada ya miezi mitatu tukapata taarifa alifariki R.I.P

Rafiki yangu nayeye alikuja fariki mwaka mmoja baadae(R,I,P), lakini siku zake za mwisho za uhai wake zilikua ngumu sana kwa manyanyaso kutoka kwa Anna na sio kusudi la mada ya leo. Nauliza tu wanajamvi kama hakuna dawa ya mapenzi au hilo limbwata hiki kilikua ni kitu gani sasa?
 
umenikumbusha kipindi kileee, pale ikungi ukifika unamwaga upepo saa sita za usiku, unapiga wali kuku, na chai kidogo, unaosha rungu unasepa, vi antena adimu sana mitaa ile ya 32
 
Ni rafiki yangu wa karibu sana ambaye tulikua siku zote tuko pamoja katika mihangaiko na harakati ya kuisaka shilingi na kuijenga nchi. Jamaa alimpenda sana mkewe mama Irene(sio jina lake halisi). Hamuwezi mkaongea mazungumzo ya nusu saa bila kumtaja, tena ni kwa mazuri tu ya kumsifia. Wala haikua ndoa mpya wakati huo kusema labda ni extended honeymoon, maana walikua tayari wana watoto wawili na mmoja alikua amemaliza darasa la saba

Siku zote alikua akisisitiza hakuna mwanamke wa nje anaeweza kumzuzua alale nje hata kwa usiku mmoja, sembuse kuitelekeza familia yake. Alikua akiwashangaa na kuwadharau sana wanaume anaosikia wanazembea kutimiza majukumu yao kwenye familia kwa kuendekeza penzi la nyumba ndogo. Yeye pia hakua limbukeni wa mapenzi, alikua kiwembe hasaa na alikua amewapangishia wanawake wawili nyumba katika maeneo tofauti ya hapa Dar(Asante Mkapa, asante Kikwete wakati huo iliwezekana),Na saa moja jioni mara nyingi alikua kasharudi kwake

Mkewe alikuja kuugua akapata stroke! Jamaa alikua anamhudumia mkewe kwa upendo wa ajabu sana. Pamoja na kua na mfanyakazi na mtoto mkubwa tu lakini chakula cha mkewe alikua anapika mwenyewe na hata kumfulia na alizunguuka nae sana kwenye hospitali nyingi nchini kwa matibabu ingawa hali yake haikua inatengemaa, kwa miaka miwili mfululizo alimtumikia with passion na alikua anaona fahari sana kutuhadithia anavojitahidi kumfanya mkewe mgonjwa awe na furaha

Ilianza kama utani. Aliachana na mmoja ya wale wanawake aliowapangishia baada ya dem kutaka kumuendesha mshikaji, ingawa sababu nyingine mwanamke alikua anataka kuolewa na raia wa kigeni. Baada ya hapo akapata dem mwingine wa kawaida tu, bint wa Kinyiramba/Mnyaturu sikumbuki exact kabila. Na yeye akampangishia nyumba. Mienendo yake kidooogo ikaanza kubadilika maana muda mwingi alikua anautumia akiwa na huyu binti hadi sehemu ya kazi!

Siku akasafiri kwenda Singida na huyo dada. Alipofika akanipigia simu akanambia 'Kaka nimekuja huku Singida huyu mtoto bana tuki sex hasikii raha, yaani anakua hayuko wet kabisaa hata nimuandae vipi, sasa kanileta kwa mtaalamu wa jadi tumepewa dawa toka juzi, naona leo tume kwichkwich imekua bomba sana, dem kasema hajawahi ku enjoy sex kama leo. Huko kwa mganga wakapewa na mbuzi jamaa aje kumfuga nyumbani kwake anapoishi yeye na mkewe!

Siku chache baada ya kurudi napigiwa simu na shangazi yake niende haraka nyumbani kwa rafiki yangu kuna tatizo, tukakutana hapo kwake mimi, brother wake wa tumbo moja na huyo shangazi yake. Tatizo jamaa anataka mkewe yule mgonjwa aliekua anampenda sana sana arudi nyumbani kijijini akajiuguze huko mpaka apone! Hapo ni baada ya mamam huyo kushtukia kua mumewe ana mahusiano na mwanamke mwingine na alikua anajisahau sasa anaongea nae mbele ya mkewe, na mama Irine alipokua anamuuliza ndio jamaa akaja juu na kumtaka aende kwao.
Tulifanikiwa kumzuia jamaa asimuondoe mkewe hapo home lakini baada ya pale akakata mguu kabisa kwenda kwake na huduma akawa hapeleki akahamia kabisaa kwenye nyumba aliyompangishia Mnyiramba/Mnyaturu! Kuna saa anakwambia 'Kaka mwanamke mzuri yule! unamuuliza nani? Anasema Anna(sio jina hali la Msingida). dah, nikaona ama kweli rafiki yangu kashikika na kakwama

Siku moja mama Irine ananipigia simu ananambia 'Shemeji naomba msinirudishe kijijini nitaenda kufa tu jamani, hakuna huduma kule, mwambie mwenzio nimekubali amlete tu huyo Anna akae nae hapa nyumbani mimi nitakaa banda la uani tu yule mbuzi watoto wamjengee banda ila msirudishe nyumbani shem'. Sikuweza maliza kuisikiliza simu ile machozi yalinidondoka. It was so emotional! Bahati mbaya hatukuweza kufanya lolote, Mama Irine alirushwa kijijini kwa kuchangiwa hela maana mumewe hakukanyaga tena pale kwake na baada ya miezi mitatu tukapata taarifa alifariki R.I.P

Rafiki yangu nayeye alikuja fariki mwaka mmoja baadae(R,I,P), lakini siku zake za mwisho za uhai wake zilikua ngumu sana kwa manyanyaso kutoka kwa Anna na sio kusudi la mada ya leo. Nauliza tu wanajamvi kama hakuna dawa ya mapenzi au hilo limbwata hiki kilikua ni kitu gani sasa?
Story yako inasikitisha mkuu.. uchawi upo tuwe makini Makamanda.
 
aiseeee hilo balaaa inshort jamaa aligeuzwa kuwa mbuzi tena akawa anajifuga yeye mwenyew ..manina wallah wenzake waliovurugwa huwa wanakwenda kwa waganga kufuata ndagu za utajiri yeye kafuata ndagu ya kugongana daahh
 
aiseeee hilo balaaa inshort jamaa aligeuzwa kuwa mbuzi tena akawa anajifuga yeye mwenyew ..manina wallah wenzake waliovurugwa huwa wanakwenda kwa waganga kufuata ndagu za utajiri yeye kafuata ndagu ya kugongana daahh
Sasa hiyo sijui ni dawa ya penzi au sumu ya penzi maana hadi mtu anaonekana wa ajabu katika jamii
 
Inasikitisha sana...

Hakuna dawa ya mapenzi popote...

Ila kuna upendo na uvumilivu kwenye mapenzi...

Uvumilivu ukifikia tamati, upendo huondoka na kutokujali hukaribishwa... Shida huanzia hapo...


Cc: mahondaw
 
Na wanawake wengine wanajua sana kucheza na saikolojia za wanaume
Ni kweli kabisa...

Wanawake wapo vizuri sana kwenye kucheza na saikolojia ya mwanaume...

Mwanaume anaweza akamtaka mwanamke na kama mwanamke hataki hata afanyaje hawezi kumpata...

Ila mwanamke anapoamua kumtaka na kumpata mwanaume fulani, ni wachache sana wanaoshindwaga...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom