Eti fiesta ni tamasha la kitaifa duh!

JF Never supports the freaks,
siendi kwenye upumbavu bora nikaogelee na Familia yangu bwawani Mindu
Hahaha

Bora ulivyoamua hivyo,kwani fiesha ni tamasha la kuhalalisha ujinga kwa vijana wa tanzania we huoni mtandao wa ngona wanaoongoza kina nani kama si hao wanaojiita wasanii...!
 
Mtake radhi mama wa watu.. kwa nini umhukumu kwa makosa ya bintie???? Wema ni mtu mzima and she is responsible for her own actions

kweli, hata mimi nimeshtuka sana!! Mama wema anahuka nini hapa? Atutake radhi wanwake wote, au labda yeye haya maneno yake sasiyo na mpangikio amerithi?
 
Japow ote tunaishi tanzania lakini tunaishi tofauti sana, kila kundi lina ishu na mitazamo yake, so kwa mtazamo wao, ni tamasha la taifa lao, ni mtazamo sahihi kwa wahusika. Ni kama tamasha la kitaifa la injili, wanaohusika ni asilimia ndogo tu, ila kwa wao, taifa lote limehudhuria.
Pia mimi naona starehe kwa kipimo si mbaya hata kidogo. Shida tu ni kujipimia
 
.. Bora kuwa Mzanzibari Hakuna haya mambo.
Usifananishe nchi ya TANGANYIKA na wilaya moja inayoitwa ZENJ hapa, kumbe hujui eeeeeeeeeh!!!!!!!!!!!!! zenj ni sawa na wilaya moja huku bara, anayebisha atoe ushahidi wa kidemografia, na sio longo longo
 
Jamani wanajamvini nimemsikia mkurugenzi wa Clouds Entertainment kuwa tamasha la Fiesta ni la kitaifa kwa kuwa wamepata ushirikiano wa nguvu kutoka kwa polisi coz wanakuwa na Polisi 500 kwa ulinzi.

swali hili tamasha la fiesta lina Utaifa gani zaidi ya Maovu kibao kule na wanatangaza kuwa kila kipindi kitakuwa na Bar yake ili watu wanywe na kusazaa.

duhuuuuu hii ndo tanzania bwana Polisi wanaacha mambo ya msingi wanashabikia ujinga Bora kuwa Mzanzibari Hakuna haya mambo.

yeye ameongelea kama clouds director promoting his product... kuchukulia hilo kama issue sioni kama ina tija yoyote!!
 
Licha ya kukosa mapato,,,,FIESTA HUENDA IKAWA CHANZO KIPYA CHA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU IKISHIRIKIANA NA MBIO ZA MWENGE NA MIKESHA YAKE
 
Nahisi huyo bosi anamipango ya kufanya Fiesta iingizwe kwenye matamasha yanayodhaminiwa na Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Vijana na Michezo. Nasema hivyo kwa kuwa amewahi kuichukua studio aliyotoa Raisi chini ya mwavuli wa THT.
 
Hatuwaachi ikiwa kama wanazika wafu wao na kutuletea majonzi kama vile VVU, kutolipa kodi, kudhulumu wasanii wa ndani n.k
 
sasa mleta mada unachobisha ni nini kama mkuu wa kaya ndiyo promota kwanini tamasha hilo lisipewe heshima ya kitaifa au ujui kazi ya raisi wako kama vipi ongea na domo jamba huwa anampa michogo kibao ya kwenda usa.
 
Usifananishe nchi ya TANGANYIKA na wilaya moja inayoitwa ZENJ hapa, kumbe hujui eeeeeeeeeh!!!!!!!!!!!!! zenj ni sawa na wilaya moja huku bara, anayebisha atoe ushahidi wa kidemografia, na sio longo longo

Bora kitongoji che uongozi thabiti kuliko nchi inayojiendesha ona sasa clouds wameamua kuliita la kitaifa na mwakani si ajabu likawekwa kwenye kalenda..
 
Sikieni, suala zima hapa ni unemployment. Hawa watu wangekuwa na vitu vya maana vya kufanya sidhani kama wangeenda huko Fiesta. Mambo kama haya alikuwa anayafanya rais Mobutu Zaire wakati wa utawala wake. Mashushushu wakimwambia wananchi wanalalamika mitaani kuwa hakuna kazi, basi anashawishi vijana wajiingize kwenye muziki ili wajipatie ajira. Mara nyingi alikuwa analeta wanamuziki wa nje kuja kutumbuiza Kinshasa ili wananchi wafurahi hatimaye wasahau matatizo yao. Leo hii wananchi wa Congo ndo mambumbumbu Afrika. Nchi yao tajiri lakini utajiri wao unaliwa na viongozi na wawekezaji na sisi tunakwenda huko huko siku si nyingi kwani dalili zote zipo!
 
Bora kitongoji che uongozi thabiti kuliko nchi inayojiendesha ona sasa clouds wameamua kuliita la kitaifa na mwakani si ajabu likawekwa kwenye kalenda..


Unakosea, mwakani wataomba lipigiwe kura ili liwe kwenye wonders of the world maana kwamba ni greatest show on earth! I bet kama Kikwete angekuwa hapa nchini lazima angeenda kumpokea Rick Ross.
 
yaani nilipe...niambiwe nirushe mikono juu....niambiwe nipige kelele....niitwe machizi wangu....niangalie mtu kashikilia katikati ya paja zake...kha!
 
Back
Top Bottom