Leo mchana kupitia TBC1, wamemtangaza kijana mmoja aliyesafiri kwa baiskeli kutoka Geita hadi Dar kwa lengo la kumpongeza JK kwa ushindi wake....! Great Thinkers, hii imekaaje? Mbona mimi naona kama imepikwa?
ETi hilo ni jina la mtangazaji wa TBC1 na kuhusu huyo kijana thread imeshaanzishwa tangu hajafika hapa dar usiwe mvivu kupitia forum kabla ya kuanzisha thread zako especial habari zinazoripotiwa na vyombo ya habari hapa nchini.
Jk hana washauri maikini, waliomshauri hii technique kwamba itapunguza hasira za watu kwa kile alichofanyiwa na NEC, ndiyo hao hao wanaomshauri katika masuala mazito ya nchi yetu na yeye bila hiana hufanya maamuzi. Kwa mtu makini asingekubaliana na huu upumbavu. Hapa unaweza ukaiona kwa usahihi kabisa tofauti ya JK na Mkapa
Huu ni uongo usio hata na soni.
Kwanini?
1. Tutajuaje kama kweli ametoka huko?
2. Je, alimwabia nani kuwa yeye anakuja Dar kwa baiskeli hivyo apokelewe?
Hebu watuache jamani mbona haya mambo ni ya kizamani sana enzi za mwaka 47? tulipokuwa tunaandamana kuunga mkono hotuba ya Kiongozi aliyotoa huko Kigoma, Arusha n.k.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.