Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Katika Gazeti la Business Times( Aug 28-Spt 3, 2009), kuna habari kwamba pamoja na Jiji la Arusha kuitwa Geneva ya Afrika, yawezekana huko tuendako likabadilika na kuitwa jiji la wanywa bia(chapombe)!
Inaelezwa kwamba, kiasi cha hela za Kitanzania millioni 288.6 hutumika kwa ajili ya kununulia bia pekee tena zinazotengenezwa na TBL tu bila ya kuhusisha zile zinazotengenezwa na makampuni mengine au aina nyingine za vilevi ikichukuliwa wastani wa Tshs 1,300 kwa chupa. Na hii ni sawa na lita 111,000 za bia kwa siku.
Kwa mujibu wa bwana Fimbo Butallah ambaye ni Brand Manager wa bia aina ya Safari tawi la Arusha, kiasi cha lita million 70 sawa na bia 140million ambazo huzalishwa kwa mwaka, asilimia 57 hunywewa na wakazi wa Arusha pekee. Kiasi kinachobaki hutumiwa na mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Tanga na Singida.
Wakuu, hebu tujadili, hii inamaanisha nini? Kazi hufanywa saa ngapi na akina nani? Nawasilisha!
Inaelezwa kwamba, kiasi cha hela za Kitanzania millioni 288.6 hutumika kwa ajili ya kununulia bia pekee tena zinazotengenezwa na TBL tu bila ya kuhusisha zile zinazotengenezwa na makampuni mengine au aina nyingine za vilevi ikichukuliwa wastani wa Tshs 1,300 kwa chupa. Na hii ni sawa na lita 111,000 za bia kwa siku.
Kwa mujibu wa bwana Fimbo Butallah ambaye ni Brand Manager wa bia aina ya Safari tawi la Arusha, kiasi cha lita million 70 sawa na bia 140million ambazo huzalishwa kwa mwaka, asilimia 57 hunywewa na wakazi wa Arusha pekee. Kiasi kinachobaki hutumiwa na mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Tanga na Singida.
Wakuu, hebu tujadili, hii inamaanisha nini? Kazi hufanywa saa ngapi na akina nani? Nawasilisha!