Ethiopia wana Ndege, fly-overs, treni za kisasa n.k lakini hali ya maisha ya wananchi wa kawaida ikoje?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Ni kweli hivi vitu tunavihitaji lakini sidhani kama ni sahihi kuvifanya viwe ndio vipaumbele vyetu vikuu kwa sasa tena kwa kuvitekeleza vyote kwa pamoja na pengine kwa gharama ya kukwamisha mambo mengine.

Sidhani kama ni sahihi kuelekeza fedha nyingi katika haya maeneo huku maeneo mengine nyeti kama kilimo,elimu na uhamasishaji na uendelezaji wa viwanda yakionekana kudorora.

Tanzania tunahitaji kuwekeza zaidi katika kilimo kinachogusa watu wengi pamoja na kuendeleza na kufufua viwanda mbalimbali ambavyo vitatoa ajira kwa watu wengi na kuongeza pato la Taifa hasa tukiwa na viwanda vingi vitakavyotumia mazao ya kilimo kama malighafi sambamba na viwanda vingine vitakavyotumia malighafi tofauti na mazao ya kilimo.

Ndugu zangu,ndege,fly over,treni za kisasa,n.k bila ustawi wa viwanda, kilimo, elimu, n.k,vitu hivi haviwezi kuleta tija inayokusudiwa.Hivi vitu ili viwe na tija ni lazima viambatane na uwepo wa shughuli nyingi za kiuchumi tofauti na hapo watu wengi watatumia miundombinu hii kusafiri kwenda kusalimia ndugu na jamaa na zaidi kusafirishia wagonjwa.

Hivi vitu ni vichocheo tu vya uchumi lakini huwezi kuchochea moto pasipo kuwa na kuni na kuni zetu hapa ni viwanda pamoja na kilimo huku tukiwa na sera za kutoa ruzuku kwa wakulima na mambo mengine ya aina ikwamo kutoa mafunzo kwa maafisa kilimo na wakulima wenyewe pamoja na kuwa na mipango na sera zitazovutia watu kujenga viwanda hapa nchini.

Kwa mfano,treni zitasafirisha nini kama hakuna mazao au bidhaa za viwandani zinazohitaji kusafirishwa kwa wingi ili treni iwe na tija?

Tukiwa na viwanda vingi maeneo mbalimbali ndani ya nchi,hatuoni watu watalazimika kusafiri kwa wingi kwenda makazini na kuongeza abiria watakaotaka kupanda treni kuwahi makazini?

Tumetenga fedha kiasi gani kutangaza utalii ili hata hizo ndege ziweze kupata abirai wa kutosha ambao watakuwa ni watalii wanaokuja hapa nchini?Lakini pia tunazingatia ukweli kuwa biashara ya utalii ni biashara ya msimu?

Au tunasubiri ndege ziwasili ndio tuanze kutangaza utali kwa nguvu kubwa?

Labda tujiulize wenzetu Ethiopia wenye ndege, treni za umeme,fly over,n.k hali ya maisha ya wananchi wake ikoje?

Sio ndio hawa hawa kila siku wanakamatwa hapa nchini kama wahamiaji haramu wanaotaka kuvuka mipaka kutafuta maisha katika nchi nyingine?

Ni kweli tunahitaji ndege,fly-overs, treni za kisasa,n.k, lakini ni lazima pia tu-balance mambo ili hivi vitu viweze kutuletea tija tunayoitaka.

Badala ya kununua ndege sita kwa wakati mmoja,nunua ndege tatu kwanza(ATCL ilikufa taratibu,tuifufue taratibu)na hizo fedha zingine zielekezi kwenye kilimo,kufufua viwanda, kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji,n.k

Mfano mwingine ni Kujenga reli ya kisasa kutoka Dar kwenda Kigoma.Hili ni jambo jema na lenye logic kabisa, ingawa nalo lina madhara yake, lakini hili la kujenga SGR kutoka Dar mpaka Dodoma kwa sasa sidhani kama ni jambo la zima na kwa mtazamo wangu ni bora hizo fedha zikaelekezwa katika maeneo mengime muhimu kwa sasa ikiwemo sekta ya Afya,umeme vijijini,mikopo ya elimu ya juu,n.k.

Bwana mkubwa mmoja alishauriwa kuwa makini na sera zake za ubinafsishaji wa mashirika ya umma lakini hukusikiiza la mtu na kila aliempinga alionekana si mzalendo ila baadae ukweli ulikuja dhihirika hivyo na huyu wa sasa nae ni swala la muda tu kabla mambo hayajadhihirika.

Tunachokifanya kwa sasa ni sawa na mtoto anaejaribu kutembea kabla ya kutambaa.

Kupanga ni kuchagua.

Kwaherini.
 
Nyinyi jamaa nyinyi. Daah! Hadi mnatia huruma. Hivi ni kweli mmekosa kabisa hoja mpk mnapinga hadi vitu vya msingi katika kuboost maendeleo ya nchi kama chachu ya kukuza uchumi wa nchi kiujumla.

Mimi nadhani kuna mtu ka hack misingi iliyo jiwekea chadema enzi za Dr slaa. Hii siyo bure.

Kama kweli wewe ni chadema, basi kama nchi tunasafari ndefu upata mbadala wa CCM kama chama tawala.
Nimeshituka ujue!
 
Hakika mkuu ni ajabu sana kuwekeza katika mambo ambayo sio ya msingi kabisa. Unawekeza kununua mandege biaashara isiyo na uhakika kabisa wala gurantee ya faida yake.

Mi nachojiuliza kwa nini wasiwekeze hata kwenye madawa na tiba.Wawekeze kwenye elimu na research?Kwa nini tusiwekeze kwenye miradi ya kuinua kwanza maisha ya watanzania wa hali ya kawaida?
 
Ni kweli hivi vitu tunavihitaji lakini sidhani kama ni sahihi kuvifanya viwe ndio vipaumbele vyetu vikuu kwa sasa tena kwa kuvitekeleza vyote kwa pamoja na pengine kwa gharama ya kukwamisha mambo mengine.

Sidhani kama ni sahihi kuelekeza fedha nyingi katika haya maeneo huku maeneo mengine nyeti kama kilimo,elimu na uhamasishaji na uendelezaji wa viwanda yakionekana kudorora.

Tanzania tunahitaji kuwekeza zaidi katika kilimo kinachogusa watu wengi pamoja na kuendeleza na kufufua viwanda mbalimbali ambavyo vitatoa ajira kwa watu wengi na kuongeza pato la Taifa hasa tukiwa na viwanda vingi vitakavyotumia mazao ya kilimo kama malighafi sambamba na viwanda vingine.

Ndugu zangu,ndege,fly over,treni za kisasa,n.k bila ustawi wa viwanda, kilimo, elimu, n.k,vitu hivi haviwezi kuleta tija inayokusudia.

Hivi vitu ni vichocheo tu vya uchumi lakini huwezi kuchochea moto pasipo kuwa na kuni na kuni zetu ni viwanda pamoja na kilimo bila kusahau elimu na mambo mengine.

Kwa mfano,treni zitasafirisha nini kama hakuna mazo au bidhaa za viwandani zinazohitaji kusafirishwa kwa wingi ili treni iwe na tija?

Tukiwa na viwanda vingi na maeneo mbalimbali ndani ya nchi,hatuoni watu watalazimika kusafiri kwa wingi kwenda makazini na kuongeza abiria watakaotaka kupanda treni kuwa makazini?

Tumetenga fedha kiasi gani kutangaza utali ili hata hizo ndege ziweze kupata abirai ambao watakuwa ni watalii wanaokuja hapa nchini?

Au tunasubiri ndege ziwasili ndio tuanze kutangaza utali kwa nguvu kubwa?

Labda tujiulize wenzetu Ethiopia wenye ndege,treni za umeme,fly over,n.k hali ya maisha ya wananchi wake ikoje?

Sio ndio hawa hawa kila siku wanakamatwa hapa nchini kama wahamiaji haramu wanaotaka kuvuka mipaka kutafuta maisha katika nchi nyingine?

Ni kweli tunahitaji ndege,fly-over,treni za kisasa,n.k, lakini ni lazima pia tu-balance mambo ili hivi vitu viweze kutuletea tija tunayoitaka.

Tunachokifanya kwa sasa ni sawa na mtoto anaejaribu kutembea kabla ya kutambaa.


Kupanga ni kuchagua.

Kwaherini.
upload_2017-10-28_9-52-50.jpeg





 
Ethiopia ni kama India, sababu ya idadi kubwa ya watu kunakuwepo na idadi kubwa ya matajiri na masikini vile vile.

Licha ya changamoto za hapa na pale, kwa sasa watanzania hawana sifa ya kuzurura nchi za watu kama waethiopia.
 
Ni kweli hivi vitu tunavihitaji lakini sidhani kama ni sahihi kuvifanya viwe ndio vipaumbele vyetu vikuu kwa sasa tena kwa kuvitekeleza vyote kwa pamoja na pengine kwa gharama ya kukwamisha mambo mengine.

Sidhani kama ni sahihi kuelekeza fedha nyingi katika haya maeneo huku maeneo mengine nyeti kama kilimo,elimu na uhamasishaji na uendelezaji wa viwanda yakionekana kudorora.

Tanzania tunahitaji kuwekeza zaidi katika kilimo kinachogusa watu wengi pamoja na kuendeleza na kufufua viwanda mbalimbali ambavyo vitatoa ajira kwa watu wengi na kuongeza pato la Taifa hasa tukiwa na viwanda vingi vitakavyotumia mazao ya kilimo kama malighafi sambamba na viwanda vingine.

Ndugu zangu,ndege,fly over,treni za kisasa,n.k bila ustawi wa viwanda, kilimo, elimu, n.k,vitu hivi haviwezi kuleta tija inayokusudia.

Hivi vitu ni vichocheo tu vya uchumi lakini huwezi kuchochea moto pasipo kuwa na kuni na kuni zetu ni viwanda pamoja na kilimo bila kusahau elimu na mambo mengine.

Kwa mfano,treni zitasafirisha nini kama hakuna mazo au bidhaa za viwandani zinazohitaji kusafirishwa kwa wingi ili treni iwe na tija?

Tukiwa na viwanda vingi na maeneo mbalimbali ndani ya nchi,hatuoni watu watalazimika kusafiri kwa wingi kwenda makazini na kuongeza abiria watakaotaka kupanda treni kuwa makazini?

Tumetenga fedha kiasi gani kutangaza utali ili hata hizo ndege ziweze kupata abirai ambao watakuwa ni watalii wanaokuja hapa nchini?

Au tunasubiri ndege ziwasili ndio tuanze kutangaza utali kwa nguvu kubwa?

Labda tujiulize wenzetu Ethiopia wenye ndege,treni za umeme,fly over,n.k hali ya maisha ya wananchi wake ikoje?

Sio ndio hawa hawa kila siku wanakamatwa hapa nchini kama wahamiaji haramu wanaotaka kuvuka mipaka kutafuta maisha katika nchi nyingine?

Ni kweli tunahitaji ndege,fly-over,treni za kisasa,n.k, lakini ni lazima pia tu-balance mambo ili hivi vitu viweze kutuletea tija tunayoitaka.

Tunachokifanya kwa sasa ni sawa na mtoto anaejaribu kutembea kabla ya kutambaa.


Kupanga ni kuchagua.

Kwaherini.


Ndugu samahani lkn hauna akili, sijakutukana ila ndiyo ukweli, huwezi kujenga Uchumi endelevu bila ya miundo mbinu ya uhakika, ili ufanye biashara ambayo ni muhimu kiuchumi ni lazima uweze kutoa bidhaa kutoka eneo A kwenda B kwa urahisi na kwa haraka!

Mfano mdogo kama tusingejenga barabara leo hii watu waishio kwenu Moshi au Iringa wangewezaje kusoma Gazeti linalochapishwa leo hii sawa na Dar?

Ndiyo maana industrial revolution ilianzia na Reli, kwanza bila ya Reli kusingekuwa na Mapinduzi ya viwanda Dunia hii!
 
HAKIKA MKUU NI AJABU SANA KUWEKEZA KATIKA MAMBO AMBAYO SIO YA MSINGI KABISA.UNAWEKEZA KUNUNUA MANDEGE BIAASHARA ISIYO NA UHAKIKA KABISA WALA GURANTEE YA FAIDA YAKE.
MI NACHOJIULIZA KWA NINI WASIWEKEZE HATA KWENYE MADAWA NA TIBA.WAWEKEZE KWENYE ELIMU NA RESEARCH?KWA NINI TUSIWEKEZE KWENYE MIRADI YA KUINUA KWANZA MAISHA YA WATANZANIA WA HALI YA KAWAIDA?
Ni kweli kabisaaa....
Hayo ma fly overs sijui tren etc..ni dependent variables.....kilimi bora, kuwekeza katika elimu, research, na kuwajengea watu uwezo ni independent variable maana ni kwamba kama kilimo tija kitashamiri, ufugaji, elimu bora na utaalamu....moja kwa moja hayo ma fly overs yatajengwa, ndege zitakuja tu....sababu watu watakua na uwezo wa hata kulipia hizo ndege....
Sis tunakimbilia mbele then tunaanza kurudi nyuma....so sad....
Kisa watu wakienda ulaya na huko Asia wanaona hizo flyovers....wanapanda mandege makubwa makubwa....wanafikiri ni kitu rahisi tu kuwa na jamii ya watu wanaoweza kupanda ndege kama daladala....Hao wazungu ukifuatilia maendeleo yao yameenda hatua kwa hatua....walifanikiwa kwenye kilimo..watu wakawa na chakula etc..then taratibu hao wakaingia kwenye industrialization....sisi ni mchanganyiko wa hatari.....
Serikali iwekeze katika elimu, technical education etc.Research,afya bora, uwezeshwaji wa viwanda vidogo vidogo etc....
 
Ni kweli hivi vitu tunavihitaji lakini sidhani kama ni sahihi kuvifanya viwe ndio vipaumbele vyetu vikuu kwa sasa tena kwa kuvitekeleza vyote kwa pamoja na pengine kwa gharama ya kukwamisha mambo mengine.

Sidhani kama ni sahihi kuelekeza fedha nyingi katika haya maeneo huku maeneo mengine nyeti kama kilimo,elimu na uhamasishaji na uendelezaji wa viwanda yakionekana kudorora.

Tanzania tunahitaji kuwekeza zaidi katika kilimo kinachogusa watu wengi pamoja na kuendeleza na kufufua viwanda mbalimbali ambavyo vitatoa ajira kwa watu wengi na kuongeza pato la Taifa hasa tukiwa na viwanda vingi vitakavyotumia mazao ya kilimo kama malighafi sambamba na viwanda vingine.

Ndugu zangu,ndege,fly over,treni za kisasa,n.k bila ustawi wa viwanda, kilimo, elimu, n.k,vitu hivi haviwezi kuleta tija inayokusudia.

Hivi vitu ni vichocheo tu vya uchumi lakini huwezi kuchochea moto pasipo kuwa na kuni na kuni zetu ni viwanda pamoja na kilimo bila kusahau elimu na mambo mengine.

Kwa mfano,treni zitasafirisha nini kama hakuna mazo au bidhaa za viwandani zinazohitaji kusafirishwa kwa wingi ili treni iwe na tija?

Tukiwa na viwanda vingi na maeneo mbalimbali ndani ya nchi,hatuoni watu watalazimika kusafiri kwa wingi kwenda makazini na kuongeza abiria watakaotaka kupanda treni kuwa makazini?

Tumetenga fedha kiasi gani kutangaza utali ili hata hizo ndege ziweze kupata abirai ambao watakuwa ni watalii wanaokuja hapa nchini?

Au tunasubiri ndege ziwasili ndio tuanze kutangaza utali kwa nguvu kubwa?

Labda tujiulize wenzetu Ethiopia wenye ndege,treni za umeme,fly over,n.k hali ya maisha ya wananchi wake ikoje?

Sio ndio hawa hawa kila siku wanakamatwa hapa nchini kama wahamiaji haramu wanaotaka kuvuka mipaka kutafuta maisha katika nchi nyingine?

Ni kweli tunahitaji ndege,fly-over,treni za kisasa,n.k, lakini ni lazima pia tu-balance mambo ili hivi vitu viweze kutuletea tija tunayoitaka.

Badala ya kununua ndege sita kwa wakato mmoja,nunua ndege tatu na hizo fedha zingine zielekezi kwenye kilimo,kufufua viwanda, kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji,n.k


Tunachokifanya kwa sasa ni sawa na mtoto anaejaribu kutembea kabla ya kutambaa.


Kupanga ni kuchagua.

Kwaherini.
Hata Mbowe ana magari, helikopita, mahoteli na mabilioni ya pesa ameficha ulaya ,

Lakini je maisha ya bavicha wa kawaida yakoje??
 
Nyinyi jamaa nyinyi. Daah! Hadi mnatia huruma. Hivi ni kweli mmekosa kabisa hoja mpk mnapinga hadi vitu vya msingi katika kuboost maendeleo ya nchi kama chachu ya kukuza uchumi wa nchi kiujumla.
Mimi nadhani kuna mtu ka hack misingi iliyo jiwekea chadema enzi za Dr slaa. Hii siyo bure.
Kama kweli wewe ni chadema, basi kama nchi tunasafari ndefu upata mbadala wa CCM kama chama tawala.
Nimeshituka ujue!
Hakuna anayepinga maendeleo ngugu! Watu wanachohoji ni mkuu kutaka kufanya vitu vingi kwa mara moja tena vingine bila kupangiwa bajeti na bunge! Maendeleo yaende sambamba na ustawi wa watu! Huwezi kuwanyima wananchi haki zao za msingi kama nyongeza ya mwaka ya mshahara na kupanda madaraja kwa kisingizio cha maendeleo! Talishachelewa na waliotuchelewesha ni hao hao ccm! Dereva aende kwa staha asijesababisha ajali!
 
52 Reactions
Reply
Back
Top Bottom