Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wadau, katika hali ya kuonesha kuwa wabunge wamechoshwa na fujo za Mchungaji Msigwa Bungeni, Mbunge wa Viti Maalum Chadema, ESTHER MATIKO amemuonesha Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai mbunge anayefanya fujo Bungeni. Matiko amemnyooshea mkono Mchungaji Msigwa na kumuomba Naibu Spika amuondoe sehemu alipokaa ambapo alikaa karibu na Godbless Lema. Kuona kuwa Msigwa anaumbuliwa, taratiibu alijiweka kando na Lema na sasa katulia tuliii kana kwamba amemwagiwa maji. Aidha, Naibu Spika amemuonya Msigwa kutokana na utovu wa nidhamu anaouonesha.
Hii ni fedheha kwake na ni wazi kuwa ndani ya Upinzani hakika wamechoshwa na vituko vya Mchungaji Msigwa na wenzake kama akina Lema, Wenje na Sugu
==========================
Hii ni fedheha kwake na ni wazi kuwa ndani ya Upinzani hakika wamechoshwa na vituko vya Mchungaji Msigwa na wenzake kama akina Lema, Wenje na Sugu
==========================
Ni baada ya kumtaja Msigwa kwa kuvuja taratibu za bunge kwa makosa badala ya Lema
Haya yametokea baada ya Msigwa kuomba mwongozo wa spika muda mfupi kabla ya kuahirisha kikao cha bunge usiku huu!