Ester Bulaya: Vikokotoo vya Mafao, Serikali haikusikiliza maoni ya wadau. Kuwasilisha muswada binafsi

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,897

"Kama Waziri Kivuli na timu yangu tutahakikisha tunaandaa muswada binafsi na kuupeleka Bungeni, ili sasa wananchi wajue nani wanatetea wafanyakazi na wastaafu, wanaowanyonga ni wakina nani, na wenye dhamira njema kwa wafangakazi ni kina nani" Mhe Ester Amos Bulaya

KikokotooNaMafao "Serikali haikusikiliza maoni ya wadau muhimu wakiwemo wafanyakazi. Bunge lichukue nafasi yake katika jambo hili kuwaponya wastaafu." Mhe Ester Amos Bulaya

#KikokotooNaMafao "Nimesoma tweets za Kigwangala amesahau kuna maisha baada ya uwaziri,kuna wazee wametoka jimboni kwake wameleta ushahidi hawajalipwa mafao yao hadi leo wamekuja niwasaidie,akumbuke aliongoza mgomo kutetea maslahi ya madaktari,atetee wafanyakazi" Ester Amos Bulaya

=====

Mbunge wa Bunda Mjini, Eser Bulaya (Chadema), amesema anakusudia kuwasilisha muswada binafsi bungeni kupinga matumizi ya vikokotoo vya pensheni kwa madai kuwa vinamnyonya mfanyakazi.

Akizungumza jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 4, Bulaya amemtaka waziri husika kujitokeza na kusema kwanini mchakato wa uandaaji vikokotoo hivyo haukuzingatia ushirikishwaji wa wadau.

“Kwanini kumekuwa na malalamiko mengi… waache kutoa majibu mepesi kwenye hoja nzito. Mimi nikishikilia jambo huwa lina ukweli na nilikaa muda mrefu sijaongea nikifanya utafiti wa kina,” amesema Bulaya.

Kuhusu pongezi za Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema zimemuongezea nguvu ya kulishughulikia suala hilo.

“Pongezi za Spika nimezipokea na zimeniongezea kasi ya kukomaa na suala hili hadi dakika ya mwisho… na kufukuzwa bungeni nimezoea,” amesema Bulaya.

Chanzo: Mtanzania
 
Muswada umeshapitishwa ndio mnaanza kufanya press conference...mm nadhani cha muhimu ni wao kurudi bungeni wakarekebishe hiyo sheria kabla ya uchaguzi ujao la sivyo hiki kipengele ndio kitakuwa cha kuombea kura 2020
 
Acha kujitoa ufahamu, hujui huoni wabunge wa upinzani wanavyo nyanyasika bunge la ccm halina meno
Muswada umeshapitishwa ndio mnaanza kufanya press conference...mm nadhani cha muhimu ni wao kurudi bungeni wakarekebishe hiyo sheria kabla ya uchaguzi ujao la sivyo hiki kipengele ndio kitakuwa cha kuombea kura 2020
 
Kigwangala amesahau kuna maisha baada ya uwaziri,kuna wazee wametoka jimboni kwake wameleta ushahidi hawajalipwa mafao yao hadi leo wamekuja niwasaidie,akumbuke aliongoza mgomo kutetea maslahi ya madaktari,atetee wafanyakazi"


Kumbukeni kuwa kuhangaika na Kingwangwala ni kuhangaika na mwehu, huyo ana laana ya wazazi na ushahidi mnao

Kwanini msielekeze nguvu na akili kutafuta suluhu badala ya kumzungumzia mgonjwa wa akili ambaye hata iweje hamtakuja na matokeo chanya!?
 
Hii ccm mpya kutoka
kupora rambirambi za kagera mpaka kupora pension za wafanyakazi CCM mpya ya Dr.Bashiru Ally na Polepole .
 
Haki ya Mungu. Namuombea Mungu sana Ester Bulaya maana wanaweza wakamsindikiza kama walivyomkosa Lissu. Mungu simama na Katembee na Ester Amos Bulaya katika harakati zake za kutetea wazee wetu wanyonge ambao hawana mtetezi. Mungu pia katende sawasawa kwa Waziri wa kazi yule Mama kama anavyostahili kwa kupitisha kanuni kama hizi bila kujali utu wa wazazi wetu ambao pia ni wazaze wake. Wote tuseme Ameni/Amina/ Ameeen.
 
Serikali wajanja sana. Wamewafanya wafanyakazi kama hawaelewi kitu.

Hawajamuibia mtu wala kumdhurumu ILA kutokana na mifuko mingi ukiacha NSSF kuwa hoi kifedha ndiyo wamebudi kumlipa kidogo na kumlipa kidogo kidogo mpaka utakapokufa.

Kwa mstaafu ina madhara makubwa kwa maana jasho lako hutalifaidi kwa maana asilimia kubwa ya mafao yako 75% yatalipwa baadaya ya kufariki. Tukijua ukifika miaka 80 Mungu mkubwa lakini wengi tunaishia miaka 70-78.

Hiki ndicho kinachotia uchungu wafanyakazi kwamba pesa yote inabaki serikalini baada ya miaka 3 ya kufariki kwa mstaafu.

Tulipwe chetu 50 au 75% kudhoofika kipesa kwa mifuko hiyo ni uzembe wa serikali na si wafanyakazi.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom