Escrow: Mahakama Imedhalilishwa! Imedharauliwa! Imefedheheshwa!- Ili Kulinda Heshima Yake

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,443
113,452
Wanabodi,

Najua wengi wetu, tumehamanika na mjadala wa Escrow na Ripoti ya PAC, kwetu sisi wengine wenu, ile Ripoti ya PAC ya jana, tunaiona hakina kitu wala haina jipya bali ni sehemu tuu ya mihemuko ile ile kuhusu sakata hili tangu mwanzo.

Escrow ni matokeo tuu, watu humu wanashangilia matokeo tuu, nikadhani ripoti hiyo ingetupeleka kwenye chanzo cha jinamizi hili la IPTL ili tung'oe tangu mizizi!, IPTL ni rushwa mwanzo mwizo!, hivi mnamjua ni nani aliyewaleta?!.

Hayo ya Ripoti ya PAC ni cha mtoto, kikubwa kwangu Escrow: Mahakama Imedhalilishwa!. Imedharauliwa!, Imefedheheshwa!-Ili Kulinda Heshima Yake inabidi Mahakama itoe statement, kwanza kukitafsiri Ibara ya 100 ya Katiba ya JMT, kuhusu nani yuko right kati ya Mahakama kutoa amri halali kulizuia Bunge kujadili issue iliyoko mahakamani, au mahakama ndio iliyokosea kutoa amri kwa Bunge, uwezo ambao mahakama haina.

Na ili kuilinda heshima yake, kama ni Jaji alikurupuka, then mahakama itamke wazi kwa kumvua ujaji jaji huyo aliyopelekea Mhimili wa Mahakama kudhalilishwa!, kudharauliwa! na kufedheheshwa!, hali itakayopelekea stop orders za mahakama zitakuwa zinadharauliwa kila siku. Vinginevyo wakitamka zuio lile lilikuwa ni amri halali, then Mahakama italifanya nini Bunge kwa kuidhalilishwa!, kuidharauliwa! na kuifedhehesha Mahakama?!.

Kwa watu wote wanaojua utawala wa sheria, "the doctrine of separations powers!", kati ya mihimili hii mitatu ya dola, hawawezi kuiacha hali hii ikapita tuu hivi hivi!.

Paskali

NB-Mode, hii mada inahusu hoja za kisheria na sio hoja za kisiasa!.
 
A rubbish not to talk, as it is against but the way to quench your thirst of self egoistic and money chasing, even Charles De Montesque wouldn't allow this ----, if he would to be alive up to date.......
 
Wewe mwenyewe hujaongea kisheria umeongea kisiasa halafu unataka watu wapoteze muda wao kuongea kisheria. Nenda kwanza ukasome constitutional na administrative law ndio uje tuongee kisheria
Wanabodi,

Najua wengi wetu, tumehamanika na mjadala wa Escrow na Ripoti ya PAC, kwetu sisi wengine wenu, ile Ripoti ya PAC ya jana, tunaiona hakina kitu wala haina jipya bali ni sehemu tuu ya mihemuko ile ile kuhusu sakata hili tangu mwanzo.

Escrow ni matokeo tuu, watu humu wanashangilia matokeo tuu, nikadhani ripoti hiyo ingetupeleka kwenye chanzo cha jinamizi hili la IPTL ili tung'oe tangu mizizi!, IPTL ni rushwa mwanzo mwizo!, hivi mnamjua ni nani aliyewaleta?!.

Hayo ya Ripoti ya PAC ni cha mtoto, kikubwa kwangu Escrow: Mahakama Imedhalilishwa!. Imedharauliwa!, Imefedheheshwa!-Ili Kulinda Heshima Yake inabidi Mahakama itoe statement, kwanza kukitafsiri Ibara ya 100 ya Katiba ya JMT, kuhusu nani yuko right kati ya Mahakama kutoa amri halali kulizuia Bunge kujadili issue iliyoko mahakamani, au mahakama ndio iliyokosea kutoa amri kwa Bunge, uwezo ambao mahakama haina.

Na ili kuilinda heshima yake, kama ni Jaji alikurupuka, then mahakama itamke wazi kwa kumvua ujaji jaji huyo aliyopelekea Mhimili wa Mahakama kudhalilishwa!, kudharauliwa! na kufedheheshwa!, hali itakayopelekea stop orders za mahakama zitakuwa zinadharauliwa kila siku. Vinginevyo wakitamka zuio lile lilikuwa ni amri halali, then Mahakama italifanya nini Bunge kwa kuidhalilishwa!, kuidharauliwa! na kuifedhehesha Mahakama?!.

Kwa watu wote wanaojua utawala wa sheria, "the doctrine of separations powers!", kati ya mihimili hii mitatu ya dola, hawawezi kuiacha hali hii ikapita tuu hivi hivi!.

Pasco.

NB-Mode, hii mada inahusu hoja za kisheria na sio hoja za kisiasa!.
 
Huu ni mwendelezo wa kile walichoanzisha.

Walishindwa kutoa amri wakati wa bunge la katiba. Eti lipo kisiasa zaidi!

Sasa, hata hili la Escrow lipo kisiasa/maisha ya watanzania. Bora wakae kimya!
 
Tatizo lako Pasco unataka kututoa kwenye mstari.Subiri basi tumalize issue moja ya sakata hili tutarejea na uchambuzi wako.

wakati nikihaidi kutorejea katika thread yako na kuomba tusiijadili zaidi nakuomba unitafute kifungu katika katiba kinachopingana na hiki hapa chini -Nasisitiza kwenye katiba siyo kwenye sheria.tunaanza na katiba kabla ya sheria.

Ibara ya 100.-(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika
Mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema
au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lako Pasco unataka kututoa kwenye mstari.Subiri basi tumalize issue moja ya sakata hili tutarejea na uchambuzi wako.

wakati nikihaidi kutorejea katika thread yako na kuomba tusiijadili zaidi nakuomba unitafute kifungu katika katiba kinachopingana na hiki hapa chini -Nasisitiza kwenye katiba siyo kwenye sheria.tunaanza na katiba kabla ya sheria.

Ibara ya 100.-(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika
Mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema
au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo
Bila kuathiri masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika!.

Jee unazizua hizo sheria nyingine zozote zinazohusika?, jee unayajua masharti yake?!.

Pasco
 
Ile ripoti ya PAC ni ripoti ya kihuni tu ambayo haina chembe ya ukweli hata kidogo ni ripoti ya kihuni kabisa.
 
Wanabodi,

Najua wengi wetu, tumehamanika na mjadala wa Escrow na Ripoti ya PAC, kwetu sisi wengine wenu, ile Ripoti ya PAC ya jana, tunaiona hakina kitu wala haina jipya bali ni sehemu tuu ya mihemuko ile ile kuhusu sakata hili tangu mwanzo.


Sijui tatizo liko wapi-hoja imefika mbele wa Wenye Nchi-Wabunge kupitia Wananchi ,kwa nini mhitimishe wakati kila upande utapata nafsi ya kutetea hoja zake.
Hasa ninachokiona ni muendlezo wenu ule ule waliopata Mgawo kufanya upotoshaji.Mmepewa nafasi ya kusikika hizi kelele za nini!




Escrow ni matokeo tuu, watu humu wanashangilia matokeo tuu, nikadhani ripoti hiyo ingetupeleka kwenye chanzo cha jinamizi hili la IPTL ili tung'oe tangu mizizi!, IPTL ni rushwa mwanzo mwizo!, hivi mnamjua ni nani aliyewaleta?!.


Kumbe unaelewa kuwa kuna tatizo?

Hayo ya Ripoti ya PAC ni cha mtoto, kikubwa kwangu Escrow: Mahakama Imedhalilishwa!. Imedharauliwa!, Imefedheheshwa!-Ili Kulinda Heshima Yake inabidi Mahakama itoe statement, kwanza kukitafsiri Ibara ya 100 ya Katiba ya JMT, kuhusu nani yuko right kati ya Mahakama kutoa amri halali kulizuia Bunge kujadili issue iliyoko mahakamani, au mahakama ndio iliyokosea kutoa amri kwa Bunge, uwezo ambao mahakama haina.

Kwanza ni vizuri umetambua hilo kuwa mtuhumiwa hawezi kujichunguza!



Na ili kuilinda heshima yake, kama ni Jaji alikurupuka, then mahakama itamke wazi kwa kumvua ujaji jaji huyo aliyopelekea Mhimili wa Mahakama kudhalilishwa!, kudharauliwa! na kufedheheshwa!, hali itakayopelekea stop orders za mahakama zitakuwa zinadharauliwa kila siku. Vinginevyo wakitamka zuio lile lilikuwa ni amri halali, then Mahakama italifanya nini Bunge kwa kuidhalilishwa!, kuidharauliwa! na kuifedhehesha Mahakama?!.

Kwa watu wote wanaojua utawala wa sheria, "the doctrine of separations powers!", kati ya mihimili hii mitatu ya dola, hawawezi kuiacha hali hii ikapita tuu hivi hivi!.

Pasco.

NB-Mode, hii mada inahusu hoja za kisheria na sio hoja za kisiasa!.

Hapa ndipo nafikia kuwa na wewe umeleta ushabiki kama wengine!
Kama unatambua kuwa hii ni isuue ya Kisheria .je umeleta hoja hii kama mwanasheria au member mwingine humu asiye na ujuzi wa fani ya Sheria.
Je hoja yako ni ipi?

Na hiyo haitoshi je Bunge haingedhalilika?

Rekodi -Wabunge 360 VS Jaji Mmoja- kwa uelewa wangu wa shule ya Kata tayari kulikuwa na kosa la msingi na la kiufundi kufikia uaamuzi wa kutoa Court Order kwa Bunge.

Kwa uzito uleule unaotaka kulinda heshima ya Mahakama akili ya kawaida inatuelekeza Mahakama Kuu chini ya Jaji Mkuu (Full Bench) ingekaa kwa dharura kusikiliza hoja ya wafungua madai,ili kupima madhara ya Kikatiba ya kufikia kuamuru/kushauri Bunge kutokuendelea na Mjadala wa Escrow .

Sidhani kama kuna mahali ndani ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 & 2000 Mahakama yetu ina Mamlaka ya kuuamuru shughuli za Bunge au Raisi kutokufanya Maamuzi


N>B usishau mgogoro wa Uteuzi wa Rais kukosa uhalali wa kimantiki

Majaji wa Ikulu- na hili ndiyo madhara yake-Mahakama kukosa uhalali wa kimantiki/nadharia mbele ya Umma ambao ndio msingi wa Dola.
 
Mgogoro wa kisheria kati ya mahakama na mihimiri mingine, mtoa tafsiri ya kisheria awe tena mahakama- huu ni ujinga.
Hekima lzm itumike the way i see leo mahakama itatoa maamuzi ya kujibeba, kesho bunge litabadilisha sheria ili kuibana mahakama.

NCHI IMEKOSA MTU WA KUTUONGOZA NA KUTUUNGANISHA
KILA MMOJA ANA NDEVU SIKU HIZI HAIJULIKANI BABA NANI, MAMA NANI, NA MTOTO NANI, WOTE WAMEFANANA.
SHAME
 
Niliipenda sana statement ya Spika juzi kwamba itafikia mahali kila mtu akifanya uchafu wake anakimbilia Mahamani kwenda kuweka zuilio. Hivi mambo yako bungeni unawezaje kukimbilia Mahakamani halafu unatafuta watu wasapoti...
 
Rejea miaka ya huko nyuma 1992. Valambia aliishitaki serikali. Valambia alishinda kesi na serikali iliamuriwa kumlipa Valambia $70 milioni. Serikali ilikaidi kulipa pamoja na juhudi zote alizofanya Valambia kupitia mahakama, serikali ilikaidi na mpaka Valambia alikutwa na umauti bila ya kulipwa pesa zake. Ukaidi umeanza siku nyingi. Tuone hili hatua gani itachukuliwa ili kuweka sawa haya mambo katika siku zijazo.
 
Bila kuathiri masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika!.

Jee unazizua hizo sheria nyingine zozote zinazohusika?, jee unayajua masharti yake?!.

Pasco

Pasco iyo phrase unaitoa wapi? Icho unachogang'ania 'bila kuathiri katiba hoi au sheria yoyote' kipo ibara ndogo ya pili inayohusu mbunge kutoshitakiwa, usipotoshe umma!!
 
Ivi mleta mada ulimsikiliza mwanasheria ...waziri wa katiba na sheria alivoclear hii ishu? Mbona hautaki? Ulimsikiliza spika? Au wazo lako ndio kuu tu???
 
Tatizo lako Pasco unataka kututoa kwenye mstari.Subiri basi tumalize issue moja ya sakata hili tutarejea na uchambuzi wako.

wakati nikihaidi kutorejea katika thread yako na kuomba tusiijadili zaidi nakuomba unitafute kifungu katika katiba kinachopingana na hiki hapa chini -Nasisitiza kwenye katiba siyo kwenye sheria.tunaanza na katiba kabla ya sheria.

Ibara ya 100.-(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika
Mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema
au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo

Naomba kueleweshwa subsection 2 inaendana vipi na Escrow? was it hoja, muswada ama wizi wa fedha za Umma?
Confusion, pls help.
 
Last edited by a moderator:
Pasco;11250243]Wanabodi,

Hayo ya Ripoti ya PAC ni cha mtoto, kikubwa kwangu Escrow: Mahakama Imedhalilishwa!. Imedharauliwa!, Imefedheheshwa!-Ili Kulinda Heshima Yake inabidi Mahakama itoe statement, kwanza kukitafsiri Ibara ya 100 ya Katiba ya JMT, kuhusu nani yuko right kati ya Mahakama kutoa amri halali kulizuia Bunge kujadili issue iliyoko mahakamani, au mahakama ndio iliyokosea kutoa amri kwa Bunge, uwezo ambao mahakama haina.



Mkuu Pasco umeona Mafisadi wanaendelea na mkakati wao.


Sarakasi mpya ya Escrow Maombi
Mawakili hao wamewasilisha maombi likiwamola Mahakama Kuu kutangaza kwamba maazimio hayo ya Bunge ya Novemba 29/2014 nauamuzi wa Spika wa kuyakubali maazimio hayo ni kinyume na Katiba kwa kuwayanakiuka Ibara ya 13(1), 13(3), 13 (6)(a) (b)(e) na 24 na 26.



13.-(1) Watu wote nisawa mbele ya sheria, na wanayo haki,bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupatahaki sawa mbele ya sheria.

(3) Haki za raia, wajibu na maslahi yakila mtu na jumuiya ya watu yatalindwa na kuamuliwa na Mahakama na vyombo vinginevyovya Mamlaka ya Nchi vilivyowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


(6) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawambele ya sheria,Mamlaka ya Nchi itaweka taratibu zinazofaa au zinazozingatia misingikwamba -
(a) wakati haki na wajibu wa mtuyeyote vinahitaji kufanyiwa uamuzi wa mahakama au chombo kinginechokinachohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwaukamilifu, na pia haki ya kukata rufaa au kupata nafuu nyingine ya
kisheria kutokana na maamuzi yamahakama au chombo hicho kingenecho kinachohusika;
(b) ni marufuku kwa mtu aliyeshtakiwakwa kosa la jinai kutendewa kama mtu mwenye kosa hilo mpaka itakapothibitikakuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwasababu ya kitendo chohote ambacho alipokitenda hakikuwa ni kosa chini ya sheria,na pia kwamba ni marufuku kwa
adhabu kutolewa ambayo ni kubwa kulikoadhabu iliyokuwapo wakati kosa linalohusika lilipotendwa;

24.-(1) Bila yakuathiri masharti ya sheria za nchi zinazohusika, kila mtu anayo haki yakumiliki mali, na haki ya hifadhi kwa mali yake aliyonayo kwa mujibu wa sheria.

26.-(1) Kila mtu anawajibu wa kufuata na kutii Katiba hii na sheria za Jamhuri ya Muungano.
(2) Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibuuliowekwa na sheria, kuchukua hatua za kisheriakuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi.
Uhuru wa majadiliano na utaratibu wa shughuli Sheria ya 1984 Na.15 ib.14
100
.-(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika Mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.





Sidhani kesi hii ina nguvu yoyote kisheria wacha tusibiri hoja ya Jaji atakaye sikiliza ombi hili.


 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom