BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,370
- 8,103
Mchekeshaji Eric Omondi kutoka Kenya ameonesha kukerwa na kitendo cha Mgombea Urais kupitia Azimio nchini Kenya, Raila Odinga kumwalika Diamond Platinumz kufanya show kwenye kampeni zake leo.
Diamond ameingia Kenya leo akitokea Afrika Kusini alikoenda kusherehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wake "Latifa" a.k.a Tiffa na mara baada ya kutua Kenya kwa private jet, alienda kufanya show kwenye kampeni za Raila Odinga kitendo ambacho kimeonesha kumkwaza mchekeshaji Eric Omondi.
Omondi amewatupia lawama wasanii wa Kenya kwa kushindwa kufanya kazi nzuri kiasi cha kupitwa na wasanii wa nchi nyingine pia amelalamikia utaratibu wa mamlaka za nchi hiyo kushindwa kutetea wasanii wa ndani ambapo ambapo ameahidi kwenda Bunge baada ya serikali mpya kuingia madarakani na kulitaka Bunge kuweka sheria ya kulazimisha matumizi ya 75% ya kazi za wasanii wa Kenya na 25% ndio iwe ya kazi za wasanii wa nje.
Diamond ameingia Kenya leo akitokea Afrika Kusini alikoenda kusherehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wake "Latifa" a.k.a Tiffa na mara baada ya kutua Kenya kwa private jet, alienda kufanya show kwenye kampeni za Raila Odinga kitendo ambacho kimeonesha kumkwaza mchekeshaji Eric Omondi.
Omondi amewatupia lawama wasanii wa Kenya kwa kushindwa kufanya kazi nzuri kiasi cha kupitwa na wasanii wa nchi nyingine pia amelalamikia utaratibu wa mamlaka za nchi hiyo kushindwa kutetea wasanii wa ndani ambapo ambapo ameahidi kwenda Bunge baada ya serikali mpya kuingia madarakani na kulitaka Bunge kuweka sheria ya kulazimisha matumizi ya 75% ya kazi za wasanii wa Kenya na 25% ndio iwe ya kazi za wasanii wa nje.