SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Wana MMU nawasalimu.
Kuna watu wana tabia hii ambayo ni hatari sana kwa ndoa za
marafiki wao.
Tabia hii inachochewa na kusababishwa na:
1. Kufananisha watu
2. Kujifanya wewe ni mwanahabari mzuri
Tuanze.
Kufananisha watu: Uko kwenye shughuli zako unakatiza mitaa. Kwa mbaali kwenye kona fulani unamwona jirani yako Huseni ameongozana na mwanamke. Sura ya huyo mwanamke hujaiona vizuri ila kwa mawazo yako ya haraka unafikiri ni mkewe Huseni.
Siku mbili tatu baada ya tukio hili unamtembelea Huseni.
Ile unafika huko, unamkuta Huseni na mkewe wapo wakitezama tv,
Baada ya kusalimiana unaanza na Huseni: "Vipi bwana, nilikuona ukiwa na shemeji pale kwenye kona ya mtaa wa xyz mkiwa kwenye mishe.
Mke wa Husein anakukazia macho kwa mshangao kisha anamtazama mumewe kwa hasira.
Ni kweli mwanaume uliyemwona siku ile alikuwa Huseni lakini hakuwa ameongozana na mkewe.
Kwa maneno yako hayo tayari umewapandia mbegu ya ugomvi mkubwa. (Huseni alikuwa kwenye mchepuko!)
Kujifanya mwanahabari mzuri. Bw Huseni ni rafiki yako mkubwa.
Mnaelezana mipango yenu ya maisha
na mambo meengi tu mnaelezana. Siku moja Huseni akakutolea ya moyoni mwake kwamba amechoka na kazi anayofanya, anataka aache ahamie mji mwingine.
Ukiwa kwenye pitapita zako ghafla unakutana na mkewe Huseni.
Unaanza kazi yako ya kupasha habari. "Huseni kaniambia anataka kuacha kazi kisha ahame mji.Mtahamia wapi shem?"
Tayari hapo umeshazua ugomvi kwenye nyumba ya Huseni.
Tabia za aina hii wengi huita umbea. Usiwe mmbea wa aina hii tafadhali, utabomoa nyumba za watu!
Kuna watu wana tabia hii ambayo ni hatari sana kwa ndoa za
marafiki wao.
Tabia hii inachochewa na kusababishwa na:
1. Kufananisha watu
2. Kujifanya wewe ni mwanahabari mzuri
Tuanze.
Kufananisha watu: Uko kwenye shughuli zako unakatiza mitaa. Kwa mbaali kwenye kona fulani unamwona jirani yako Huseni ameongozana na mwanamke. Sura ya huyo mwanamke hujaiona vizuri ila kwa mawazo yako ya haraka unafikiri ni mkewe Huseni.
Siku mbili tatu baada ya tukio hili unamtembelea Huseni.
Ile unafika huko, unamkuta Huseni na mkewe wapo wakitezama tv,
Baada ya kusalimiana unaanza na Huseni: "Vipi bwana, nilikuona ukiwa na shemeji pale kwenye kona ya mtaa wa xyz mkiwa kwenye mishe.
Mke wa Husein anakukazia macho kwa mshangao kisha anamtazama mumewe kwa hasira.
Ni kweli mwanaume uliyemwona siku ile alikuwa Huseni lakini hakuwa ameongozana na mkewe.
Kwa maneno yako hayo tayari umewapandia mbegu ya ugomvi mkubwa. (Huseni alikuwa kwenye mchepuko!)
Kujifanya mwanahabari mzuri. Bw Huseni ni rafiki yako mkubwa.
Mnaelezana mipango yenu ya maisha
na mambo meengi tu mnaelezana. Siku moja Huseni akakutolea ya moyoni mwake kwamba amechoka na kazi anayofanya, anataka aache ahamie mji mwingine.
Ukiwa kwenye pitapita zako ghafla unakutana na mkewe Huseni.
Unaanza kazi yako ya kupasha habari. "Huseni kaniambia anataka kuacha kazi kisha ahame mji.Mtahamia wapi shem?"
Tayari hapo umeshazua ugomvi kwenye nyumba ya Huseni.
Tabia za aina hii wengi huita umbea. Usiwe mmbea wa aina hii tafadhali, utabomoa nyumba za watu!