Epuka kujitibu mwenyewe kwa taarifa za mtandaoni. Muone mtaalam wa afya kila unapopata dalili mbaya za kiafya

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,799
Tiba Mtandaoni.jpg

(Picha: The Sheriff)

Umewahi kupata dalili ya afya ambayo haijawahi kutokea hapo awali na ukaanza kujiuliza ni nini kinachoweza kuwa tatizo? Of course, huenda jibu lako ni kama langu pia, "Kabisa!"

Sasa basi, inapotokea hivi hatua ya kwanza inayopaswa kufanyika ni kuwasiliana na mtoa huduma wa afya ili kupata ushauri au/na matibabu. Lakini mara nyingi hatupendi kufanya hivyo na badala yake tunaishia kujaribu kufumbua wenyewe kuhusu kinachotutatiza.

Mfano, jambo la kwanza tunalofanya, hususan katika enzi hizi za teknolojia, ni kutoa simu zetu na kuandika dalili zetu mtandaoni na kisha kujiridhisha na majibu tunayokutana nayo huko na dawa zinazopendekezwa kisha tunaanza kujitibu.

Wakati mwingine tunamtafuta Dkt. Google ili tu kupata faraja kwamba chochote kinachoendelea si tatizo kubwa.

Hii si sahihi kwani maelezo ya matibabu ya mtandaoni si sahihi kila wakati. Kuna sababu muhimu za kuonana na madaktari kwa huduma za afya: wao ni wataalam, na sisi sio.

Haya yanaweza kuwa madhara ya kutegemea mtandao kupata utatuzi wa changamoto za kiafya:

Wasiwasi wa kuwa na tatizo kubwa kuliko uhalisia
Vyanzo vya mtandaoni vinaweza kuleta magonjwa yoyote ambayo yana dalili zinazofanana. Hii ina maana kwamba, hata kama hali si ya kutisha sana, tunaweza kuishia kupata matokeo kuwa ni suala zito linalohatarisha maisha. Lakini pia, hakuna njia ya kujua kabisa kila kitu kinachoendelea bila kuonana daktari. Yeye anaweza kuona dalili tofauti au zaidi ya unazopata mtandaoni.

Majibu ya mtandaoni yanaweza kukupa mfadhaiko ambao utakusababishia madhara zaidi ya kiafya.

Wasiwasi wa kiafya (health enxiety) ni hali ambayo huathiri watu wengi. Wale walio na wasiwasi huu huhangaika kufikiria kwamba wana tatizo kubwa la kiafya ambalo halijatambuliwa. Wanaamini kwamba wao ni wagonjwa sana, hata kama wanaonyesha dalili ndogo tu. Ikiwa wana afya bila matatizo yoyote, wanaweza kusisitiza kwamba kuna kitu kibaya kinaendelea katika miili yao.

Kuchukua dawa zisizo na ufanisi au kuchanganya
Baada ya wagonjwa kuangalia dalili zao au kudhani kuwa wana hali fulani, wanaweza kuchukua hatua zaidi kwa kujaribu kujitibu wao wenyewe. Njia moja wanayoweza kufanya hivyo ni kwa kuchukua dawa za dukani au kujaribu matibabu ya nyumbani ili kusaidia suala lolote wanalofikiri kuwa wanasumbuliwa nalo.

Lakini dawa zina madhara, hivyo ikiwa hatuhitaji kutumia basi hatupaswi. Kutumia dawa isiyofaa kwa ugonjwa husika haitatui chochote kwani utaendelea kuugua maradhi yaleyale. Pia kunaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi au kusababisha matatizo makubwa zaidi.

Kupuuza dalili na kudhani tatizo ni dogo kuliko uhalisia
Jambo la kwanza nililosema ni kwamba kutegemea taarifa za mtandaoni ni hatari kwa sababu husababisha msongo wa mawazo na hofu; na kwamba watu wanaweza kuchukua hatua ambazo badala yake zitazidisha shida zao. Lakini wakati mwingine, ni kinyume chake. Wengine wanaweza kudhani ni jambo dogo tu na hivyo kutoona umuhimu wa kumuona daktari.

Pia, wanaweza kuona ni tatizo dogo tu linaloweza kutibiwa nyumbani bila maelezo ya daktari kumbe ni jambo zito ambalo linahitaji matibabu ya haraka. Kupuuza kabisa kunaweza kuifanya hali kuwa mbaya zaidi. Hii ndiyo sababu watu wanapaswa kuwasiliana na madaktari wao ikiwa wanakumbana na hali za kiafya zisizo za kawaida.

Ufafanuzi mbaya na mkanganyiko
Kwa sisi ambao si madaktari, inaweza kuwa vigumu kuelewa masharti ya matibabu ya matatizo tuliyo nayo. Tunaweza kutafsiri vibaya dalili, tatizo, na jinsi linavyoathiri afya zetu. Au tunaweza kutoelewa matibabu, taratibu, na chaguzi za dawa tunapojaribu kujitibu wenyewe.

Ni vyema kuzungumza na daktari kuhusu matatizo yoyote ili aeleze kwa njia ambayo unaweza kuelewa.

Kila mgonjwa ni tofauti na mwingine
Kunaweza pia kuwa na taarifa mtandaoni ambao ni ya kupotosha kwa sababu ya muktadha au ukosefu wa maelezo mengine. Afya ya kila mtu ni tofauti. Kila familia ina historia tofauti ya matibabu, na afya ya mtu binafsi hutofautiana na wengine.

Ndiyo maana ni muhimu sana kwa wagonjwa kuzungumza na madaktari ambao wana historia yao ya matibabu. Madaktari wanaweza kuamua jinsi afya ya jumla ya mtu binafsi inavyohusiana na dalili anazopata. Hii inatoa ufahamu bora juu ya hali ambayo mtu anayo.

Hitimisho
Katika ulimwengu mkamilifu, maelezo ya afya ni ya kweli, sahihi na yanaweza kutoa majibu sahihi kwa kila mtu. Lakini sivyo ilivyo. Hatuishi katika ulimwengu mkamilifu. Taarifa za kupotosha zinajitokeza kila wakati katika utafutaji wetu mtandaoni, na inaweza kuwa vigumu kutambua tofauti ya ukweli na uongo.

Hii inafanya kuwa hatari kwa wale wanaojaribu kushughulikia afya zao peke yao bila kuwashirikisha wataalamu wa afya. Wanaweza kupata msongo wakijaribu kutatua matatizo yao wenyewe, au kupuuza kwamba wanahitaji huduma kabisa. Hii inafanya kuwa vigumu kwa madaktari kutoa huduma muhimu.

Ahsanteni!
 
Tena dalili za HIV, kila kitu google inalink hapo.. Mtu anaweza kufa kabla ya siku zake kumbe hamna kitu. Nilishawahi kuumwa macho, kugoogle ikaniletea vitu vigumu sana hadi uwezekano wa tatizo kuwa na connection na ubongo, kwenda hospitali wakaniambia tatizo nililonalo na kupewa eye drops na tabs chache, siku nne tu jicho linaona kama zamani.
 
Pia madaktari wawe wazi, anakuandikia dawa na hakuambii side effects zake sana sana atakusihi usitumie kinywaji au zingatia mlo kabla ya kumeza kitu ambacho si sahihi sana kuishia hapo.

Niliwahi andikiwa dawa kumbe moja masharti yake ni usitembee juani (ya kupakaa), either kaa ndani au jifunike na nguo ili kuepuka miale ya moja kwa moja ya jua,. kuwa na uelewa wa kutafuta taarifa ulinisaidia kwani kupitia tovuti ya masuala ya madawa ndio ilielezea hiko kipengele, na si hiyo tu, kuna baadhi ya dawa ukimeza kuna vipengele vinaweza kukutokea lakini daktari kukujuza inasaidia kupunguza wasiwasi.

Mpaka kesho nikijisikia homa au hali isiyo ya kawaida ntaenda hospitali kwanza, ila siwezi meza dawa bila kutafuta taarifa zake kiundani hasa hizi dawa ambazo sijawahi meza kamwe.
 
Nilichojifunza kwa watu wa afya kuhusu kuandika dawa, akikuuliza dawa nikuandikie utaenda kununua au unanunulia hapa just mwambie utaenda kununua mwenyewe au hata asipokuuliza mpe impression mapema kwamba hautachukulia pharmacy ya hospitali, ukichukulia kwao, atakuandikia dawa hadi zisizohitajika na dozi ndefu ilimradi wakuuzie.
 
Mkuu, Google imekukosea nini? Google ni search engine haishindani na madakatari tu bali inashindana na kila kada wakiwemo walimu, waganga, wanasheria, maengineer, wanasiasa n.k. Kazi yake kubwa ni kumpa mtu taarifa ila kazi ya kuamua kama taarifa ni sahihi au la ni ya mtafutaji.

Kutafuta taarifa zangu za kiafya mtandaoni sio kosa na kama nitaamua kwamba hata Dawa niandikiwe na Google pia sio tatizo mwisho wa siku naweza hata kuahiza hizo dawa kwa njia ya Google na nikaletewa nyumbani kwangu.

Hata hivyo ushauri wako ni mzuri "Maumvu yakizidi pata ushauri wa daktari"
 
Mtoto wangu alipozaliwa tu baada ya Kama wiki hivi kitovi kikawa hakifungi mara mwezi ukaisha kitovi hakifungi Kama kawaida nikagugu nikapata maelezo ya kina nikaambiwa na dawa ya kumpa, Lile tatizo nililimaliza kupitia google. Wife tu alikua anatatizo la ngozi, ngozi yake haisikii mafuta maupele Kama yote. Nilipogugu tu nikamtafutia dawa akapona. Google Ni nzuri ukijiua kuitimia vizuri
 
Mtoto wangu alipozaliwa tu baada ya Kama wiki hivi kitovi kikawa hakifungi mara mwezi ukaisha kitovi hakifungi Kama kawaida nikagugu nikapata maelezo ya kina nikaambiwa na dawa ya kumpa, Lile tatizo nililimaliza kupitia google. Wife tu alikua anatatizo la ngozi, ngozi yake haisikii mafuta maupele Kama yote. Nilipogugu tu nikamtafutia dawa akapona. Google Ni nzuri ukijiua kuitimia vizuri
Kwa hiyo hivi sasa GUGU ina-trend siyo mkuu.
Anyway pia watu wanalalamika kupewa mi-vitamin na midawa mingine ili miela ya kulipa iwe mingi sina uhakika lkn madai haya yapo
 
Wateja wamepungua kwenye hiyo zahanati yako ya binafsi. Mimi ntaendelea kuuliza utatuzi wa magonjwa mbalimbali humu kwenye mitandao, nilikuwa mhanga wa malaria zinazojirudia kila mara lakini baada ya kusoma ushauri wa wadau hapa JamiiForum, malaria imekuwa historia, na U.T.I ndiyo kabisaa nilishaisahau siku nyingi.
 
Don't Google your symptoms
Cha pili ni kwamba zile taarfa mnazopewa pale ni kwa ajili ya layman sio za kidaktari
Madaktari na wao wanagoogle lakini kuna majukwaa maalum kwa ajili ya taarfa za ugonjwa kitabibu kwa layman hawez kuaccess hivo ila madaktar they do

Sent from my SM-G960U1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom