Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 104
Baada ya kuuanza mwezi Februari kwa kichapo kizito cha goli 9-0 kutoka kwa Manchester United na kisha kupigwa tena 3-2 na Newcastle kwenye michezo ya ligi, Southampton hii leo inashuka tena dimbani kupepetana na Chelsea
The Blues itakayokuwa ugenini leo imepewa imani kubwa ya kushinda mchezo huo, imeshinda michezo 5 kati ya 6 tangu Tomas Tuchel asaini kandarasi ya kukinoa kikosi hicho cha Darajani
Mchezo mwingine ni Merseyside derby ambapo Liverpool inakutana na Everton katika Dimba la Anfield. Mara ya mwisho Everton kushinda Anfield ni mwaka 1999 na mara ya mwisho kushinda Derby hiyo ni mwaka 2010.
Liverpool itatakiwa kushinda mchezo huo na kuomba Chelsea ifungwe ili aweze kurejea katika nafasi nne za juu
Michezo mingine ni kati ya Burnley ambayo itakuwa nyumbani kuumana na West Brom, huku Fulham ikiwa mwenyeji wa Sheffield United.