JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,306
- 5,452
Goli la dakika 90 mfungaji akiwa ni Harry Kane wa Tottenham limekatisha furaha ya Chelsea ambapo limesababisha mechi baina ya timu hizo kumalizika kwa sare ya 2-2 katika Premier League, leo Agosti 14, 2022 kwenye Uwanja wa Stamford Bridge.
Kalidou Koulibaly na Reece James ndio waliofunga magoli ya Chelsea wakati lile la kwanza la Tottenham likifungwa na Pierre-Emile Hojbjerg.
Aidha, katika mchezo huo makocha wa timu hizo, Antonio Conte wa Chelsea na Thomas Tuchel walipewa onyo na mwamuzi kutokana na kurushiana maneno wakati mchezo ukiendelea.