Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,612
- 864
Wizara ya Fedha huko nuyma hadi kwa mwaka wa fedha 2011/2012 ilikuwa ikitumia mfumo wa malipo Epica7 ambao baadae ulipendekezwa ubadilishwe ili kurekebisha baadhi ya kasoro ilizokuwa nazo. Mfumo huo mpya unaitwa Epica9. Mfumo huo mpya unaotajwa kuwa umeboroshwa kwa kuhusisha;
1. Fedha kwenda moja kwa moja Hazina badala ya awali kutoka BoT - Hazina kisha BoT kama mlipaji.
2. Mfumo huo umgehusisha malipo ya moja kwa moja kupitia akaunti ya mlipwaji au wenyewe kuiita TIS
3 Mfumo huo unadaiwa kudhibiti mianya ya wizi yaani upo "secured" zaidi.
Kabla ya kuanza kutumika mfumo huo Wizara ya Fedha ilifanya seminar nyingi ili kuwaelimisha wafanyakazi wake ambao ndiyo watumiaji wakuu.
Nije kwenye mada sasa,
Tokea mfumo huo uanze umeleta shida kubwa sana kwa kukwamisha malipo ya karibu taasisi zote zinazotegemea malipo toka serikali kuu kupitia hazina!!!!!
Ingawaje ni mfumo mpya lakini matatizo yake yamevuka mipaka, mfano ni mishahara ya askari polisi ambao bado hawapitii bank baadhi ya mikoa au vituo mpaka leo bado hawajapata!!!!! Ukitoa hilo, hata wadau wengine ambao fedha zao ambazo zimeingizwa huko wanalia kilio maana hawajui lini watapata uhakika wa malipo hayo!!!! Uchunguzi ambao nimeufanya karibu mikoa tisa ya Tanzania Bara umebainisha matatizo yanayofanana,
1.Taasisi nyingi za serikali huletewa fedha kwa karatasi inayoitwa "Warrant of Fund". Pindi zinapopelekwa hazina karibu zote hazionekani mpaka kwa mbinde sana, jambo ambalo halikuwepo kwenye Epica7!!!!
2. Hata kama zikionekana bado mfumo huo hautoi uhakika wa kuweza kuprint hundi!!!!
3. Kucacpture voucher moja hadi nyingine kama mtandao ukiwepo ni rahisi mtu anayetoka Dar - Moro kufika kabla ya mtu wa hazina kukamilisha transaction moja!!!! (Hakuna chumvi katika hilo). Hapo bado huja aprove transaction hiyo!!!!
4. Pamoja na matatizo yake lakini bado mfumo huo unadaowa kutokuwa "friend user"
Taarifa ambazo hazina mawaa zinasema hata kuchelewa kupatikana kwa mishahara kwa watumishi wa umma kabla ya sikukuu ya Iddy Mubarak hasa ambao wanategemea kupitia bank kunatokana na mfumo huo mpya kukataa kufanya kazi na kusababisha bank ya NMB kushindwa kugawa fedha kwenye mabanki na akaunti za watu.
Kutokana na yote hayo nini maoni yangu?????
Mfumo huo unajenga chuki kubwa sana kwa watu hawaoni sababu ya kupata tabu kwa jambo ambalo wao wanaliita ufisadi wa Epica9. Wadau wanajiuliza kwa nini mfumo huo usifanyiwe kazi kabla ya kuanza kutumika???? Zaidi ya yote, inasadikiwa mafungu ya serikali bado hayajaanza kutoka kama inavyokusudiwa lakini system inasumbua namna hiyo na bado baadhi ya vitu havijawa implemented kama TIS lakini matatizo ni haya je itakuwaje vitavyokuwa intergrated???
Namalizia kwa kusema "Je Epica9 ni ufisadi mwingine ndani ya Wizara ya Fedha????
Matatizo ya system hiyo yalizungumziwa kidogo na Raia Mwema - Hazina wakwama kulipa
1. Fedha kwenda moja kwa moja Hazina badala ya awali kutoka BoT - Hazina kisha BoT kama mlipaji.
2. Mfumo huo umgehusisha malipo ya moja kwa moja kupitia akaunti ya mlipwaji au wenyewe kuiita TIS
3 Mfumo huo unadaiwa kudhibiti mianya ya wizi yaani upo "secured" zaidi.
Kabla ya kuanza kutumika mfumo huo Wizara ya Fedha ilifanya seminar nyingi ili kuwaelimisha wafanyakazi wake ambao ndiyo watumiaji wakuu.
Nije kwenye mada sasa,
Tokea mfumo huo uanze umeleta shida kubwa sana kwa kukwamisha malipo ya karibu taasisi zote zinazotegemea malipo toka serikali kuu kupitia hazina!!!!!
Ingawaje ni mfumo mpya lakini matatizo yake yamevuka mipaka, mfano ni mishahara ya askari polisi ambao bado hawapitii bank baadhi ya mikoa au vituo mpaka leo bado hawajapata!!!!! Ukitoa hilo, hata wadau wengine ambao fedha zao ambazo zimeingizwa huko wanalia kilio maana hawajui lini watapata uhakika wa malipo hayo!!!! Uchunguzi ambao nimeufanya karibu mikoa tisa ya Tanzania Bara umebainisha matatizo yanayofanana,
1.Taasisi nyingi za serikali huletewa fedha kwa karatasi inayoitwa "Warrant of Fund". Pindi zinapopelekwa hazina karibu zote hazionekani mpaka kwa mbinde sana, jambo ambalo halikuwepo kwenye Epica7!!!!
2. Hata kama zikionekana bado mfumo huo hautoi uhakika wa kuweza kuprint hundi!!!!
3. Kucacpture voucher moja hadi nyingine kama mtandao ukiwepo ni rahisi mtu anayetoka Dar - Moro kufika kabla ya mtu wa hazina kukamilisha transaction moja!!!! (Hakuna chumvi katika hilo). Hapo bado huja aprove transaction hiyo!!!!
4. Pamoja na matatizo yake lakini bado mfumo huo unadaowa kutokuwa "friend user"
Taarifa ambazo hazina mawaa zinasema hata kuchelewa kupatikana kwa mishahara kwa watumishi wa umma kabla ya sikukuu ya Iddy Mubarak hasa ambao wanategemea kupitia bank kunatokana na mfumo huo mpya kukataa kufanya kazi na kusababisha bank ya NMB kushindwa kugawa fedha kwenye mabanki na akaunti za watu.
Kutokana na yote hayo nini maoni yangu?????
Mfumo huo unajenga chuki kubwa sana kwa watu hawaoni sababu ya kupata tabu kwa jambo ambalo wao wanaliita ufisadi wa Epica9. Wadau wanajiuliza kwa nini mfumo huo usifanyiwe kazi kabla ya kuanza kutumika???? Zaidi ya yote, inasadikiwa mafungu ya serikali bado hayajaanza kutoka kama inavyokusudiwa lakini system inasumbua namna hiyo na bado baadhi ya vitu havijawa implemented kama TIS lakini matatizo ni haya je itakuwaje vitavyokuwa intergrated???
Namalizia kwa kusema "Je Epica9 ni ufisadi mwingine ndani ya Wizara ya Fedha????
Matatizo ya system hiyo yalizungumziwa kidogo na Raia Mwema - Hazina wakwama kulipa