Enzi zetu: Mpenzi wangu nikupendaye kwa dhati

KAFA.cOm

JF-Expert Member
Jun 22, 2013
1,301
738
ENZI ZETU

Mpenzi wangu nikupendaye kwa dhati.

Salamu nyingi sana zikufikie huko ulipo. Utakapo kujua khali yangu mie ni bukheri kabisa. Hofu na mashaka ni juu yako ewe mpenzi wangu uliye mbali na upeo wa macho yangu.

Dhumuni la barua yangu ni kutaka kukusabahi na kukushukuru kwa barua yako niliyoipata leo mchana. Ahsante sana kwa barua yenye maneno matamu kweli mpenzi wangu. Ama hakika moyo wangu ulijawa shauku kubwa niliposikia jina langu likiitwa pale assemble wakati barua zikigawiwa. Wajua ni namna gani nakupenda ewe kidani cha moyo wangu, chakula cha ubongo wangu, na tulizo la nafsi yangu.

Umeniambia kuwa shuleni kwenu huwa wanafungua barua wakiona ina mwandiko wa kiume. Safari hii nitamwomba monitress wetu aniandikie juu ya bahasha ili nisikuponze mpenzi wangu ukafukuzwa shule. Najua jinsi baba yako alivyo mkali mithili ya mbogo asije akakuchapa bure kishtobe wangu nikupendaye kiasi cha kukosa usingizi kwa ajili yako hadi naiona taswira yako kwenye bilauri ninywapo maji.

Mwezi ujao shule yetu itakuja shuleni kwenu kwenye debate. Ingawa mimi sijui mambo hayo ya debate nitafanya mchongo na msela wangu kiongozi wa debate aniandike jina ili nami nije. Nimekukumbuka sana. Nakumbuka wakati wa likizo tulivyokuwa tunakaa juu ya jiwe lile pembeni ya mto huku nikivichezea vidole vyako nawe ukiniimbia nyimbo za taratibu. Yaani sauti yako ni tamu utadhani kinanda. Kila siku huwa naisikia sauti yako ikiniimbia kwa mahaba ya dhati.

Nisikuchoshe kwa barua ndefu mpenzi wangu. Ila fahamu kuwa mwenzio juu yako sina hali. Nakupenda hadi nimepitiliza maana yenyewe ya neno kupenda. Daima umo mawazoni mwangu.

Msalimie sana yule rafiki yako uliyekuwa naye siku ile. Kuna rafiki yangu anampenda sana. Nitakuja naye kwenye debate.

Ndimi nikupendaye daima,
Mahabuba wako.

UJUMBE:
If you love three, you are not free,
If you love two, you are not true,
Love only one, that one is ME.

DEDICATION:
Always Be My Baby by Mariah Carey
I Swear by All 4 One

*Zamani raha sana*
 
Copy&Paste.

Mpenzi wangu nikupendaye kwa dhati.

Salamu nyingi sana zikufikie huko ulipo. Utakapo kujua khali yangu mie ni bukheri kabisa. Hofu na mashaka ni juu yako ewe mpenzi wangu uliye mbali na upeo wa macho yangu.

Dhumuni la barua yangu ni kutaka kukusabahi na kukushukuru kwa barua yako niliyoipata leo mchana. Ahsante sana kwa barua yenye maneno matamu kweli mpenzi wangu. Ama hakika moyo wangu ulijawa shauku kubwa niliposikia jina langu likiitwa pale assemble wakati barua zikigawiwa. Wajua ni namna gani nakupenda ewe kidani cha moyo wangu, chakula cha ubongo wangu, na tulizo la nafsi yangu.

Umeniambia kuwa shuleni kwenu huwa wanafungua barua wakiona ina mwandiko wa kiume. Safari hii nitamwomba monitress wetu aniandikie juu ya bahasha ili nisikuponze mpenzi wangu ukafukuzwa shule. Najua jinsi baba yako alivyo mkali mithili ya mbogo asije akakuchapa bure kishtobe wangu nikupendaye kiasi cha kukosa usingizi kwa ajili yako hadi naiona taswira yako kwenye bilauri ninywapo maji.

Mwezi ujao shule yetu itakuja shuleni kwenu kwenye debate. Ingawa mimi sijui mambo hayo ya debate nitafanya mchongo na msela wangu kiongozi wa debate aniandike jina ili nami nije. Nimekukumbuka sana. Nakumbuka wakati wa likizo tulivyokuwa tunakaa juu ya jiwe lile pembeni ya mto huku nikivichezea vidole vyako nawe ukiniimbia nyimbo za taratibu. Yaani sauti yako ni tamu utadhani kinanda. Kila siku huwa naisikia sauti yako ikiniimbia kwa mahaba ya dhati.

Nisikuchoshe kwa barua ndefu mpenzi wangu. Ila fahamu kuwa mwenzio juu yako sina hali. Nakupenda hadi nimepitiliza maana yenyewe ya neno kupenda. Daima umo mawazoni mwangu.

Msalimie sana yule rafiki yako uliyekuwa naye siku ile. Kuna rafiki yangu anampenda sana. Nitakuja naye kwenye debate.

Ndimi nikupendaye daima,
Mahabuba wako.

UJUMBE:
If you love three, you are not free,
If you love two, you are not true,
Love only one, that one is ME.

DEDICATION:
Always Be My Baby by Mariah Carey
I Swear by All 4 One

*Zamani raha sana*
 
images(1).jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom