beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Wakati Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete anaingia madarakani, wananchi wengi walikuwa wanaona ni sawa serikali kuwa na mamlaka ya kufungia magazeti hasa pale yanapotoa taarifa zenye utata.. Hawakuwa na neno ilionekana kawaida tu..
Nadhani pengine ni athari ya hulka ya Mstaafu aliyemtangulia, Mzee wetu BW Mkapa, ambaye tofauti yake na Ngosha ni kidogo tu ila wote ni 'wakali'..
Nachotaka kusema, pamoja na mambo mengine, inawezekana uelewa wananchi umekuwa ndani ya kipindi cha JK.. Kwamba watu wameelewa zaidi thamani ya Uhuru wa Maoni.
Au ni athari za kisiasa? Kwamba wananchi wengi wamenufaika na upevukaji wa siasa zetu za ndani wakati wa JK? Sina uhakika..
Ninachoamini.. Hizi namba zimeongezeka sio kwa bahati mbaya. Ipo kazi ilifanywa na serikali iliyopita ambayo naamini serikali ya sasa itazidi kuiendeleza kazi hiyo ya kuacha uhuru wa maoni utamalaki kama wananchi wanavyotaka..
Nimechochea? Sidhani..
Nadhani pengine ni athari ya hulka ya Mstaafu aliyemtangulia, Mzee wetu BW Mkapa, ambaye tofauti yake na Ngosha ni kidogo tu ila wote ni 'wakali'..
Nachotaka kusema, pamoja na mambo mengine, inawezekana uelewa wananchi umekuwa ndani ya kipindi cha JK.. Kwamba watu wameelewa zaidi thamani ya Uhuru wa Maoni.
Au ni athari za kisiasa? Kwamba wananchi wengi wamenufaika na upevukaji wa siasa zetu za ndani wakati wa JK? Sina uhakika..
Ninachoamini.. Hizi namba zimeongezeka sio kwa bahati mbaya. Ipo kazi ilifanywa na serikali iliyopita ambayo naamini serikali ya sasa itazidi kuiendeleza kazi hiyo ya kuacha uhuru wa maoni utamalaki kama wananchi wanavyotaka..
Nimechochea? Sidhani..