Enyi wazanzibari daini nchi yenu ndani ya jumuia ya a. Mashariki

Congo

JF-Expert Member
Mar 13, 2008
2,064
2,301
Nimekuwa nikisikiliza mambo mengi yahusuyo madai ya Wazanzibari kudai nchi yao. Wakitaka muungano ujadiliwe na ikiwezekana zaidi uvunjike. Mimi nawashauri jambo moja la ziada, daini pia ushiriki wa nchi yenu (Zanzibar) kama nchi kamili ndani ya Jumuia ya Afrika Mashariki. Sababu yangu ni kuwa, kulingana na mchakato wa Shirikisho la Afrika Mashariki kuna uwezekano wa mambo yaleyale ambayo Tanganyika na Zanzibar imeungana nayo yakawa ndio hayohayo yatakayokuwa mambo ya muungano wakati wa shirikisho. Mambo kama ulinzi, mambo ya ndani, fedha, forodha, mambo ya nje n.k. yanaweza kuwa ndio yatakayokuwa mambo ya muungano wa Shirikisho la Afrika Mashariki. Ikiwa hivyo umuhimu wa muungano wetu wetu hautakuwepo utakuwa ni ujirani kwa kuwa Waziri wa ulinzi atakuwa wa Shirikisho na sio wa muungano hivyo mambo tuliyoungana nayo yatakuwa yanaongozwa na Shirikisho. Nawashauri Wazanzibari watafakari wadai kiti chao ndani ya Jumuia ya Afrika Mashariki kama nchi kamili.
 
  • Thanks
Reactions: lum
hapa suluhisho tuvuunje tanzania twende EAC basi, kila nchi peke yake Tanganyika,Zanzibar. kama ni suala la muungano huu ni bora na una nchi nyingi zaidi ..ukimuona mtu anakataa hili ujue shida yake si muungano( umoja) anataka ukoloni wa tanganyika kwa zanzibar uendelee... JAMBO AMBALO WAZANZIBAR HATUWEZI TENA KULIVUMILIA kuambiwa nchi yetu si nchi inamaana tanganyika iliungana na wilaya au mkoa .........?
 
hapa suluhisho tuvuunje tanzania twende EAC basi, kila nchi peke yake Tanganyika,Zanzibar. kama ni suala la muungano huu ni bora na una nchi nyingi zaidi ..ukimuona mtu anakataa hili ujue shida yake si muungano( umoja) anataka ukoloni wa tanganyika kwa zanzibar uendelee... JAMBO AMBALO WAZANZIBAR HATUWEZI TENA KULIVUMILIA kuambiwa nchi yetu si nchi inamaana tanganyika iliungana na wilaya au mkoa .........?



Hapo katika hiyo red iliyokuwa bolded mojawapo ni jibu sahihi, kwahiyo chagua jibu sahihi hapo kati ya a au b:-
SWALI: Katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar ni:
a) Wilaya
b)Mkoa
 
Back
Top Bottom