Enyi wanaume acheni kuwapiga mawe wanawake wakati ninyi ndio mnaowazalisha

Omela Odongo

Member
Mar 26, 2021
47
66
Nawasalimia Wana jf wote nikitumai mu wazima na weekend hii tulivu. Mimi ni member mpya katika jukwaa hili kwa kuandika na kuchangia maada lakini nimeanza kuichungulia Jamii forum tangu mwaka 2010.

Niende kwenye maada moja kwa moja, nimekuwa nikisoma maada humu kwenye jukwaa za kuwakejeli hawa wanaoitwa "Single mother" na kadiri siku zinavyozidi maada hizi zinaongezeka kuna uwezekano hata wao wanaongezeka kila kukicha. Sasa swali la kujiuliza ni nani anayesababisha hali hii kuongezeka kwa kasi namba hii?Je wanazaa peke yao? Kwa nini wanaume muwazalishe wanawake(mabinti)halafu muwatelekeze na kisha muanze kuwasimanga kwa kiwango hiki tunachokishuhudia nyakati hizi.

Wanaume kama mumeamua kuwaita single mothers basi na wanaume mliowazalisha mnatakiwa kuitwa single fathers kama wasivyoaminika kama wakiolewa hata ninyi pia humuamiki kwenye ndoa na huu ni ubaguzi wa hali ya juu na roho mbaya kutoka kwa wanaume unaofanana na kisa hiki:.

John 8:3-11 Waandishi na Mafarisayo wakamleta mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi,wakamweka katikati.Wakamwambia mwalimu, mwanamke huyu amefunaniwa alipokuwa akizini.Basi kwa torati,Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii, nawe wasemaje?.............

Mwanaume aliyekuwa akizini naye aliachiwa huru Ila mwanamke alitakiwa kupigwa mawe.Sasa tujiulize mwanamke alikuwa anazini peke yake? Kwanini kwa mwanamke ni kosa lakini so kwa mwanaume?Enyi wanaume acheni kuwapiga mawe wanawake wakati ninyi ndio mnaowazalisha.
 
Naona umeandika kifungu katika biblia!! Kuna umuhimu haya maandiko tuyasome vizuri, tutafute elimu baswa, tusimuacbe elimu akaenda zake.

Iko hivi
Mwanamke/mwanume mzinifu anapigwa mawe mpaka afe kama tu atazini hali ya kuwa ana ndoa..

Na mwanaume/mwanamke mzinifu ni viboko mie kama hayuko kwenye ndoa..

Haya singo faza nimepita kutia saini hapa.
 
Nawasalimia Wana jf wote nikitumai mu wazima na weekend hii tulivu. Mimi ni member mpya katika jukwaa hili kwa kuandika na kuchangia maada lakini nimeanza kuichungulia Jamii forum tangu mwaka 2010. Niende kwenye maada moja kwa moja,nimekuwa nikisoma maada humu kwenye jukwaa za kuwakejeli hawa wanaoitwa "Single mother" na kadiri siku zinavyozidi maada hizi zinaongezeka kuna uwezekano hata wao wanaongezeka kila kukicha.Sasa swali la kujiuliza ni nani anayesababisha hali hii kuongezeka kwa kasi namba hii?Je wanazaa peke yao? Kwa nini wanaume muwazalishe wanawake(mabinti)halafu muwatelekeze na kisha muanze kuwasimanga kwa kiwango hiki tunachokishuhudia nyakati hizi. Wanaume kama mumeamua kuwaita single mothers basi na wanaume mliowazalisha mnatakiwa kuitwa single fathers kama wasivyoaminika kama wakiolewa hata ninyi pia humuamiki kwenye ndoa na huu ni ubaguzi wa hali ya juu na roho mbaya kutoka kwa wanaume unaofanana na kisa hiki:. John 8:3-11 Waandishi na Mafarisayo wakamleta mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi,wakamweka katikati.Wakamwambia mwalimu,mwanamke huyu amefunaniwa alipokuwa akizini.Basi kwa torati,Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii,nawe wasemaje?.............

Mwanaume aliyekuwa akizini naye aliachiwa huru Ila mwanamke alitakiwa kupigwa mawe.Sasa tujiulize mwanamke alikuwa anazini peke yake?kwanini kwa mwanamke ni kosa lakini so kwa mwanaume?Enyi wanaume acheni kuwapiga mawe wanawake wakati ninyi ndio mnaowazalisha.
Kwanza kabla sijachangia mada hii,naomba unipe maana ya "Single Father" ? Yaanu unamaanisha nini hasa.

Shukrani.
 
Kwa hili povu ni dhahili kuna mwanaume ameumiza mtu huku.

Pole mtoa mada. Kumbuka watoto wanaolelewa bila malezi ya Baba, Mungu huwa anawabariki sana. Roll mode wao ni Diamond.
 
NIDA , ukitaka kuangalia namba yako , unaulizwa jina la mama na si baba.
Kwenye sensa ya kufahamu uzao wa jamii(taifa) Fulani , wanaangalia wastani wa mwanamke mmoja ana watoto wangapi, Wala si mwanaume.
Kwahiyo mwanamke ni Kila kitu katika jamii na maendeleo.
Watalaumiwa tu , haitabadilika.
Na kwa nini iwe hivyo ?
 
Ukiona jina halipo jua hata type ya watu wa hivyo haipo.

Ukisema single father na haulei mtoto, hiyo imekaaje??!
 
Back
Top Bottom