Mama siyo hamnazo (empty set ama clean slate) ana ufahamu na anawafahamu wanaccm. Anajua kwamba ninyi si watu wazuri, kwa unafiki na ukigeugeu hamjambo.
Kwa namna mlivyo geuka (u- turn) kutoka kuunga mkono sera za ukandamizaji za Magufuli hadi kuunga mkono sera za uungwana. Hakika nawaonya mama naye anawashangaa.
Leo mmegeuka na mnaimba yale yale kwa mama Samia mkijisahaulisha dharau zenu kwake akiwa VP. Mkidhani kashushwa toka sayari nyingine halafu akatua Tanzania na kuwa rais.
Mama naye zimo. Na ninaamini anatumia kauli mbiu ya Rais Mstaafu Kikwete ---"akili za kuambiwa, changanya na zako".
Kwa namna mlivyo geuka (u- turn) kutoka kuunga mkono sera za ukandamizaji za Magufuli hadi kuunga mkono sera za uungwana. Hakika nawaonya mama naye anawashangaa.
- Mliimba sifa na mapambio ya kila aina kuunga mkono ukandamizaji.
- Mlisimama kwa kusujudu kila majina yenu yalipotajwa na Magufuli.
- Kuna mmoja mwanaume rijali kabisa (sikumbuki ni nani) alipiga magoti alipokuwa anapokea (sijui ni hela ile?). Nitaomba mwenye picha ailete hapa.
- Mlitaka aongezewe muda madarakani (kinyume kabisa na katiba).
- Huyu mama akiwa msaidizi wa rais (vp) mlimuona kama taka ktk jaa (huko bara mnaita jalala).
- Mlikata mauno mbele ya rais (mnamkumbuka Lugola?) na kumlinganisha na Yesu ili kumfurahisha.
Leo mmegeuka na mnaimba yale yale kwa mama Samia mkijisahaulisha dharau zenu kwake akiwa VP. Mkidhani kashushwa toka sayari nyingine halafu akatua Tanzania na kuwa rais.
Mama naye zimo. Na ninaamini anatumia kauli mbiu ya Rais Mstaafu Kikwete ---"akili za kuambiwa, changanya na zako".