Special thread; Tamthilia ya Siri za Familia Inayorushwa EATV

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Instagram: @sirizafamilia

Salaam Sana

Kwa wale wanaofuatilia tamthilia ya "Siri za Familia" (Family Secrets) inayorushwa EATV hii ni thread maalumu kuhusiana na Tamthilia hiyo.

Familia nyingi zina siri ingawa zinatofautiana. Baadhi ya siri zinaweza kujulikana na familia yote au wachache au hata mwanafamilia moja. Siri zinaweza kuhusiana na miiko, ukatili, mahusiano, magonjwa, uhalifu, mauaji, ubakaji nk. Jambo lolote ambalo mtu au familia inadhani linaweza kuleta tafarani linafanywa siri ya familia.

Hata hivyo hakuna siri ya watu wengi au ya muda mrefu kwani baadhi ya siri hatimaye hufichuka na siri zingine mtu anaweza kufa nazo. Je, ni nini kinatokea pale siri za familia zinapofichuka?

Fuatitlia thread hii ya Siri hizi katika SIRI ZA FAMILIA inayorushwa EATV kila siku ya Jumatatu hadi Alhamisi kuanzia saa 12.30 jioni hadi saa 1.00 jioni na kurudiwa kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa saa 4.30 asubuhi hadi saa 5 asubuhi. Marudio ya wiki nzima ni siku ya Jumapili kuanzia saa 8.

Sasa hivi tamthilia inayorushwa ni season 1 na ina episode 48. Season 2 iko katika maandalizi.

Kwa wale wapenzi tukutane hapa kwa maoni na hata wenye visa vya kweli ambavyo wangependa viwepo katika Season 2. Visa vingi vilivyopo katika Season 1 ni visa vya kweli na vinatokana na utafiti uliofanywa na visa vya kweli ambavyo wadau wanavileta.

==============================================
Niaje wakuu,

Wabongo waliohusika kuitengeneza Tamthilia hii ya SIRI ZA FAMILIA walitulia na kuifanya kuwa tamthilia nzuri sana sio siri.

Inaeleweka na naona imebase katika matukio halisi yatokeayo katika jamii zetu.
Pia wamejitahidi kumatch couples, yaani wanaokuwa wapenzi wanaendana na dizain kama wameenda shule

Ila zaidi nimegundua kuna wanawake wazuri ninaowatamani sana mle, sio yule mama mzuri mwenye chura tu, bali hata Brenda na wengineo.

■Hongereni Waandaaji na Waigizaji.

Wakuu poleni na majukumu,

Imekuwa faraja sana kwa tamthilia ya siri za familia hasa kwa mida baada ya uchovu na pilika za mchana kutwa kutafuta riziki. Tangu ianze season one imekuwa kivutio pekee hadi sasa maandalizi ya season four.

Mimi nawapongeza sana wahusika wote.

Ombi tu wapunguze muda wa matangazo na muda wa kutoka season moja kwenda nyingine.

Wadau mnapendekeza nini au mna lolote juu ya hii series?
 
Mimi ni mdau namba moja wa siri ya familiaaaaa..Naipenda sanaaa...
Asante sana nalazuzu endelea kufuatilia.

Pia kama una maoni yoyote ili kusaidia kuiboresha tutafurahi kusikia. Tunatambua pia kuwa kuna mapungufu fulani fulani, tunaendelea kuyaboresha.

Pia si vibaya kushare sehemu zinazokuvutia zaidi na wengine. Kama una maswali pia unaweza kuuliza.
 
Hua sio mpenzi wa Tamhilia ki ujumla ila hii kidogo imenifurahisha hasa Mke wake na jacobo na mdogo wake bila kumsahau Obama wanacheza vizuri
 
Obama nimemkubali japo ndio mara ya kwanza kumuona lakini jamaa ananichekesha sana kwa styl yake ya kuigiza
Mi sikuwa naifahamu lakini mwanangu wa miaka mitatu alikua akimuona dada anamwagilia maua analilia mpira naye amwagilie huku akijiita Obama!! Sikumjua Obama anayezungumziwa mpaka siku nilipowakuta wakiitazama ndio nkaifahamu nami nikawa memba
Ni tamthilia nzuri kwakweli
 
Obama nimemkubali japo ndio mara ya kwanza kumuona lakini jamaa ananichekesha sana kwa styl yake ya kuigiza

Ni kweli Obama amekuwa na wapenzi wengi kutokana na uchezaji wake uliochanganyika na Comedy kidogo. House Boy mzoefu wa mjini.
 
Mi sikuwa naifahamu lakini mwanangu wa miaka mitatu alikua akimuona dada anamwagilia maua analilia mpira naye amwagilie huku akijiita Obama!! Sikumjua Obama anayezungumziwa mpaka siku nilipowakuta wakiitazama ndio nkaifahamu nami nikawa memba
Ni tamthilia nzuri kwakweli

Haaaa haaa umenifanya nicheke kwa sauti ya juu. Ni vema ukamkutanisha Mwanao na Obama apate kumbukumbu.

Obama na Dayana ni majipu katika Tamthilia hii haaaaa haaa

Endelea kuifuatilia kwa karibu.
 
Nangoja marudio saa 10:30am hapa EATV ...kwa waliokosa jana basi leoo ni siku murua kwa ajili yenu....
 
Haaaa haaa umenifanya nicheke kwa sauti ya juu. Ni vema ukamkutanisha Mwanao na Obama apate kumbukumbu.

Obama na Dayana ni majipu katika Tamthilia hii haaaaa haaa

Endelea kuifuatilia kwa karibu.
Yani kwakweli kijana wangu kamkubali kweli Obama..mi mara ya kwanza nlidhani anajiita Obama Rais nlipomjua Obama anaezungumziwa nilicheka sana..watoto bwana
 
Hua sio mpenzi wa Tamhilia ki ujumla ila hii kidogo imenifurahisha hasa Mke wake na jacobo na mdogo wake bila kumsahau Obama wanacheza vizuri

Haaa haaa Mkuu Mke wake na Jacobo na mdogo wake ni nani? Au una maana Carlos na Sheila?

Karibu endelea kuifuatilia.
 
hiyo tamthilia naona wote ni wasaliti hakuna ailye salama, halafu ni katika mzunguko wao tu, hongera kwa aliyebuni ni nzuri kwakweli

Kaka haya mambo yako sana katika familia lakini wengi wanauchuna kama hayapo. Vyombo vya habari kila mara vinareport matukio kama haya. JF napo pamejaa visa vingi kama hivi.

Hata hivyo yako matukio mengine mbeleni zaidi ya mahusiano.
 
Yani kwakweli kijana wangu kamkubali kweli Obama..mi mara ya kwanza nlidhani anajiita Obama Rais nlipomjua Obama anaezungumziwa nilicheka sana..watoto bwana

Haaaa haaaa na huyu Obama anjiita hivyo baada ya watu wengi kumfananisha na Rais Obama kuwa kafanana naye kidogo. I am not sure.
 
Haaaa haaaa na huyu Obama anjiita hivyo baada ya watu wengi kumfananisha na Rais Obama kuwa kafanana naye kidogo. I am not sure.
Of course hata mi huwa naiona sura ya Rais Obama kwa huyu jamaa!! Hata home nliwaambia inawezekana jamaa amejiita hivyo kwakua wanafanana
 
Of course hata mi huwa naiona sura ya Rais Obama kwa huyu jamaa!! Hata home nliwaambia inawezekana jamaa amejiita hivyo kwakua wanafanana

Obama na Team yake!

IMG_2770.JPG
 
Back
Top Bottom